Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

Marahabaaaa!
Lugha ni sehemu ya jamii nayo huakisi maendeleo na mabadiliko ya jamii hiyo katika nyanja zote za maisha yake. Na kwa vile hakuna jamii ambayo imesimama tisti, lugha nayo hubadilika badilika ili kwenda sambamba na mabadiliko ya jamii. Kwa sababu hiyo maneno hubadilishiwa muktadha na mawanda ya matumizi yake.

Japo kietimolojia salamu hii ya shikamoo ina makandokando hayo ya kitumwa, leo hii imebadilishiwa muktadha na mawanda yake ya kimatumizi na kila mtumia lugha anajua kuwa lengo lake kuu ni kuonyesha heshima mathalani kwa wazee. Na kwa muktadha huu mimi sioni tatizo lolote.

Ukifanya uchunguzi wa kietimolojia kwa maneno mengi (hasa ya mkopo) ukayachunguza kwa makini yalikotoka na yalivyotumika hapo zamani utagundua kwamba maneno mengi tu yana matatizo na utakuwa na kazi ngumu sana ya kubadili kila neno lililokuwa likitumika vibaya hapo zamani. Na itabidi utafute neno jipya mbadala. Isitoshe lugha hai huwa haipendi kutungiwa misheria. Wewe unaweza kupiga marufuku neno unalodhani kuwa lina historia mbaya lakini jamii ikaamua kuendelea kulitumia tu katika matumizi yake mapya, na hakuna utakachofanya. Ndiyo maana BAKITA wanatunga misamiati rasmi kila siku lakini hakuna anayeitumia huku mitaani na misamiati hiyo wamebaki nayo katika makabrasha yao huko.

Shikamoo !!!
 
Shikamoo kaka Shimba(goti hadi ardhini huku na kichwa nimeinamisha)
Marahabaaaaaaa !!!

Yaani hapa nilipo nipo nimekunja na nne kabisa nashika shika midevu yangu. Na kwa vile ushaniambia kuwa mi si furushi basi najiona kama dunia yote ni yangu. Kabarikiwe sana ewe binti mwema
 
Ndio maana mtoto hawezi kumsalimia mtoto mwenzake "Shikamoo" au watu wenye umri unaolingana hawasalimiani shikamoo.....
SALAMU YA SHIKAMOO NI KWA AJILI YA KUMSALIMIA MTU ALIYEKUZIDI UMRI TUU.............
Kwahiyo Shikamoo kwa siku hizi ina maana gani? kama ina maana ya salamu mbona salamu nyingine za kibantu zina maana nzuri yenye uhalisia wa wakati.
 
Kwahiyo Shikamoo kwa siku hizi ina maana gani? kama ina maana ya salamu mbona salamu nyingine za kibantu zina maana nzuri yenye uhalisia wa wakati.
Mkuu, kiuhalisia SHIKAMOO si salamu. Huko Lamu ambako ndo chimbuko la lugha hii ya Kiswahili, hawasalimiani kwa kutumia neno hilo.
 
Kwa nilivyosikia mimi neno shikamoo maana yake ni "niko chini ya miguu yako.

Pia nimesikia hilo neno ni la kitumwa na lilikuwa linatumiwa na watumwa kuwaonyesha heshima wakuu wao.

Kuna baadhi ya watu nawajua hawapendi kupewa shikamoo na hata wakipewa hawajibu marahaba.

Je kama hili neno ni la kitumwa, kwanini sisi tuendelee kulitumia kama neno linaloashiria heshima?

Kama lilitumika kuwakandamiza mababu zetu kwanini na sisi tulipe nafasi? Au tunalitumia kama wenzetu Wamarekani weusi wanavyo tumia neno "nigga" ambalo lilitumika kudharau mababu zao na kulifanya la kwetu sasa?
Hii yote inatokana na kutokujua Maana yake na Nidhamu ya Uwoga.
 
Sidhani sasa ivi kila anae amkia anamaana ya kwamba niko chini ya miguu yako
Sahihi ila kiasili ni kuwa watoto huwaamuru wakubwa washike miguu yao. Neno hili nasikia ni la Kireno na lilitumika enzi hizo za utumwa kwa mtumwa akimkosea bwana wake basi kusamehewa aliamuliwa amshike kiganja cha mguu bwana mkubwa.
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom