Asili ya jina Tanzania na mwasisi wake: Mohammed Iqbal Dar

Ni mtanzania mwenye asili ya asia-mhindi Mohammed Akberi.anasema alianza kwa jina la bismillah akachukua tan zan ia toka tanganyika na zanzibar!jee serikali yetu haioni umuhimu ya kumpa walau nishani ktk sherehe za muungano huyu mtu? maana yupo hai, jana nimemsikia bbcswahili
 
Ni mtanzania mwenye asili ya asia-mhindi Mohammed Akberi.anasema alianza kwa jina la bismillah akachukua tan zan ia toka tanganyika na zanzibar!jee serikali yetu haioni umuhimu ya kumpa walau nishani ktk sherehe za muungano huyu mtu? maana yupo hai, jana nimemsikia bbcswahili

Sidhani kama serikali yetu italikumbuka hilo! Eric Santonga Aliyetunga wimbo wa Nkhosi sikoleli afrika huko Afrika ya kusini hata kaburi lake halijulikani liko wapi! Na je unajua kirefu cha FIAT?
 
Sidhani kama serikali yetu italikumbuka hilo! Eric Santonga Aliyetunga wimbo wa Nkhosi sikoleli afrika huko Afrika ya kusini hata kaburi lake halijulikani liko wapi! Na je unajua kirefu cha FIAT?

..........fabrica italiano automobile torino !
 
Ni mtanzania mwenye asili ya asia-mhindi Mohammed Akberi.anasema alianza kwa jina la bismillah akachukua tan zan ia toka tanganyika na zanzibar!jee serikali yetu haioni umuhimu ya kumpa walau nishani ktk sherehe za muungano huyu mtu? maana yupo hai, jana nimemsikia bbcswahili

Umenikumbusha mbali mkuu, nakumbuka nilishawahi kusoma gazeti moja juu ya huyu mzee aliyebuni jina la Tanzania, katika maelezo yake anasema ilitolewa kama shindano na yeye ndiye aliyeshinda.Kutokana na ubunifu wake huo alilipwa Tsh 200.Kweli watu kama hawa ni wa kukumbukwa.
 
Takbiiir-Allahu akbar nilikua sijui hii kumbe nchi yetu ya tanzania ina jina la mtume?...AHMAD....
 
Jamaa yupo sahihi mfumo kristo unataka historia ipotee msishangae mbona hata waasisi wa taa na tanu hawatajwi eti historia ya tanu wanaanzia kwa nyerere wakat nyerere kaingia tanu mwaka 1952 taa imeanzshwa mwaka 1929 wanapotosha tu historia ye2.
 
kweli kabisa uyu jamaa nilimsikia bbc siku moja anasema ilikuwa mwaka 1964 alipokuwa mwanafunzi wa mzumbe
kwa sasa anaishi london
 
Huyu mkuu namkubali niliona FIAT moja imeandikwa Italy Frame, na upande wa pili wakaandika I belong to Italy. nadhani maana hii inaweza kuwa kweli.
 
Sidhani kama serikali yetu italikumbuka hilo! Eric Santonga Aliyetunga wimbo wa Nkhosi sikoleli afrika huko Afrika ya kusini hata kaburi lake halijulikani liko wapi! Na je unajua kirefu cha FIAT?


Hall of Fame
Those who have expanded our horizons.
The stuff of legends.
https://www.jamiiforums.com/print/sontonga.htm

Enoch Mankayi Sontonga
circa 1873 - 18 April 1905
The humble and obscure life of Enoch Sontonga is an antithesis of the dreams he inspired in generations of Africans through his famous composition "Nkosi Sikelel' iAfrika". Details of his short life are hard to come by. He was born in Uitenhage (Eastern Cape), in about 1873. Trained as a teacher at the Lovedale Institution, he was sent to a Methodist Mission school in Nancefield, near Johannesburg. He married Diana Mgqibisa, the daughter of a prominent minister in the African Methodist Episcopal Church and had one son.

A choirmaster and photographer, he wrote the first verse and chorus of "Nkosi Sikelel' iAfrika" when he was 24 (1897), one of many songs he wrote for his pupils. Later the same year, he composed the music. The song is a prayer for God's blessing on the land and all its people. Sontonga's choir sang the song around Johannesburg and KwaZulu-Natal, and other choirs followed them. It was first sung in public in 1899 at the ordination of Rev Boweni, a Shangaan Methodist Minister.

Most of Sontonga's songs were sad, witnessing the suffering of African people in Johannesburg, but they were so popular that after his death choirs used to borrow them from his wife. According to sources, she eventually sold the rights to the song for a mere sixpence. She died in 1929.

Sontonga died of unknown causes at the young age of 32, in 1905. He was buried in Braamfontein, Johannesburg and his grave has only recently been discovered after intensive research. This was the announcement of the death of Enoch Sontonga:
Translation of original Xhosa item in the newspaper "Imvo Zabantsundu", dated 27 June 1905.
SONTONGA, E. Johannesburg. On 18 April 1905 ENOCH M. SONTONGA passed away. He was not sick this time. He, however, suffered at times from stomach ache to the extent that he would predict that these were his last days on this earth. One Sunday he requested to take a photograph of his wife. The wife refused because she was suffering a toothache that particular day. This young man was a composer for the Church of Rev. P.J. Mzimba at one location in Johannesburg. He was also a photographer and a lay preacher. He is survived by his wife and one child. He was born in Uitenhage and was 33 years old.

Sontonga wrote his songs down in an exercise book, which was lent out to other choirmasters and eventually became the property of a family member, Boxing Granny. She never missed a boxing match in Soweto, hence the nickname. She died at about the time Sontonga's grave was declared a heritage site in 1996, but the book was never found.

Solomon Plaatje, one of South Africa's greatest writers and a founding member of the ANC, was the first to have the song recorded, accompanied by Sylvia Colenso on the piano. This was on 16 October 1923, in London. In 1925 the ANC adopted the song as the closing anthem for their meetings. In 1927 seven additional Xhosa stanzas were added by Samuel Mqhayi, a poet. The song was published in a local newspaper in the same year, and was included in the Presbyterian Xhosa hymn book "Ingwade Yama-culo Ase-rabe" in 1929. A Sesotho version was published in 1942 by Moses Mphahlele.

The Rev J L Dube's Ohlange Zulu Choir popularised "Nkosi Sikelel' iAfrika" at concerts in Johannesburg, and it became a popular church hymn that was also adopted as the anthem at political meetings. For decades Nkosi Sikelel' iAfrika was regarded as the national anthem of South Africa by the oppressed and it was always sung as an act of defiance against the apartheid regime. There are no standard versions or translations of "Nkosi Sikelel' iAfrika" so the words vary from place to place and from occasion to occasion. Generally the first stanza is sung in Xhosa or Zulu, followed by the Sesotho version. The song spread beyond the borders of South Africa and has been translated and adapted into a number of other languages. It is still the national anthem of Tanzania and Zambia and has also been sung in Zimbabwe and Namibia for many years.

A proclamation issued by the State President on 20 April 1994 stipulated that both "Nkosi Sikelel' iAfrika" and "Die Stem" (the Call of South Africa), written by Afrikaans poet CJ Langenhoven in 1918, would be the national anthems of South Africa. In 1996 a shortened, combined version of the two anthems was released as the new National Anthem. On 18 April, 2005 Minister of Arts and Culture, Pallo Jordan said at the unveiling of the Enoch Sontonga Memorial:
"There is a saying that goes 'those whom the gods love died young' - Sontonga was one of those. His work will be immortalised as South Africa's and other African countries' national anthems."

And so today, we celebrate Enoch Sontonga's gift to us, a heroic message of calm, written in the eye of the storm. Today it forms part of South Africa's national identity; and along with "Die Stem", it brings together all the different strands of the country's past in a union of inclusiveness, symbolizing the oneness of South Africa's people.
The first two stanzas with its translation:
Nkosi sikelel' iAfrika
Nkosi sikelel' iAfrika
Maluphakanyisw' uphondo lwayo,
Yizwa imithandazo yethu,
Nkosi sikelela, thina lusapho lwayo.

Morena boloka setjhaba sa heso,
O fedise dintwa la matshwenyeho,
O se boloke, O se boloke setjhaba sa heso,
Setjhaba sa South Afrika - South Afrika.
God bless Africa,
Lift her horn on high,
Hear our prayers.
God bless us

Who are Your people.
God save our nation,
End wars and strife.
South Africa, South Africa.
Gallery:

Contact the Enoch Sontonga Foundation:

Email: enoch@rsa.org.za

 
UNAPOTAJA historia ya nchi Tanzania, ni dhahiri kwamba hutaacha kutaja majina ya wapigania uhuru na viongozi mbalimbali walioiongoza tangu enzi za ukoloni, hadi kupata uhuru.Hata hivyo, katika kila historia ya taifa lolote iliyojengwa, kuna watu waliofanikisha historia hiyo, lakini kwa sababu moja au nyingine, michango ya baadhi yao imesahaulika na pengine kutotajwa kabisa kwenye historia hizo.
Wengi wa Watanzania tunafahamu kuwa jina la nchi yetu Tanzania, limetokana na majina ya nchi mbili zilizoungana na kuwa moja ambazo ni Tanganyika na Zanzibar. Hivi ndivyo tulivyofundishwa shuleni.
Wengine wanaamini kuwa Rais wa kwanza na muasisi wa taifa hili, Hayati Mwalimu Julius Nyerere ndiye aliyebuni jina la Tanzania.
Lakini ukweli ni kwamba, jina la Tanzania lilibuniwa na mmoja wa wananchi walioshiriki mchakato wa kutafuta jina la nchi hii, baadaya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.
Mohammed Iqbal Dar ndiye aliyebuni jina la Tanzania, wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 akiwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzumbe.
Ilikuwaje?
“Nilikuwa maktaba najisomea, nilishika gazeti la Daily News, wakati huo likiitwa The Standard, ndipo nikaona tangazo hilo,” anaeleza Dar alivyopata hamasa na kuongeza:
“Siku hiyo hiyo, nikafanya majaribio ya kutafuta jina bila hata ya kuishirikisha familia yangu. Nilichuka karatasi na kalamu, lakini kabla sijaanza kufanya chochote, nilimwomba Mungu aniwezeshe kwa maana naamini Mungu, ndiye kila kitu wakati wa kufanya jambo lolote.”
“Kwa hiyo kwenye ile karatasi nikaandika Tanganyika na Zanzibar kisha, nikaandika majina yangu mawili; Iqbal na Ahmadiya,” anasema Dar na kufafanua kuwa Iqbal ni jina lake na jina la ubini na Ahmadiyya ndiyo dhehebu lake.
Kupata jina Tanzania
Akisimulia alivyopata jina Tanzania, anasema kuwa ilimchukua dakika tano tu kufikiria na kulipata jina hilo.
“Nilichukua Tan kutoka kwenye Tanganyika na kuongeza Zan kutoka kwenye Zanzibar na kupata Tanzan, niliona halitimii vizuri,”anasimulia Dar.
Anabainisha kuwa baadaye alifikiria na kugundua kuwa majina mengi ya nchi za Afrika yanaishia na IA mfano akitoa mfano wa Ethiopia, Gambia, Tunisia, Nigeria, Algeria, Somalia, Zambia, Namibia na kwamba baada ya kubaini hilo aliamua kuongezea herufi hizo mbili na kupata jina Tanzania.
“NIlituma maombi yangu katika shindano hilo, bila kumwambia mtu yeyote nyumbani,” anasema Dar.
Baada ya muda mfupi baba yake, mzee Tufail Ahmad Dar, alipokea barua kutoka Wizara ya Habari na Utalii (wakati huo), ambapo ndani yake kulikuwa na ujumbe wa pongezi ya kwamba kijana wake ameshinda katika shindano hilo.
“Wakati naandika, sikuwa na matumaini kama nitashinda kwa kuwa shindano hilo lilikua wazi kwa watu mbalimbali, hivyo sikuwa na tarajio lolote kama ningeshinda,
“Jioni wakati narudi nyumbani, baba mzazi alinifungulia mlango wakati si kawaida yake kwani mama ndiye alikuwa akinifungulia siku zote, hapo nikajua kuna kitu hakipo sawa. Lakini, nilikaribishwa na tabasamu la baba, pamoja na pongezi nyingi, nilifurahi sana,” anaeleza.
Tuzo
Dar anasema kuwa kwa ushindi huo, alitunukiwa ngao pamoja na fedha taslimu Sh200 kama zawadi ya ubunifu wake.
Pamoja na kuibuka mshindi wa ubunifu huo na hadi leo jina la Tanzania alilolibuni yeye linaendelea kutumika, lakini Dar anadai kuwa mchango wake huo kwa taifa ni kama hautambuliwi na Serikali imemsahau katika kuandika historia ya taifa la Tanzania.
“Sijui kwa nini sitambuliwi tangu wakati huo? Hakuna chochote kinachoelezea uhusika wangu katika kupata jina la Tanzania na ukiwauliza watu, wengi watakwambia ilikuwa ni Nyerere aliyeleta jina Tanzania, hii inaumiza,” anasema akilalamika.
Tanzania ya sasa
Baada ya miaka 13 tangu kufariki kwa Nyerere, Dar anasema kuwa Tanzania haimtendei haki mwasisi huyo wa Taifa, ambalo ni kisiwa cha amani.
“Ni kama imepita miaka mingi sana tangu kifo chake. Watanzania wamesahau kila kitu alichokiota Mwalimu Nyerere. Nakumbuka moja ya vita kubwa aliyopigana ni dhidi ya rushwa, yeye aliichuki rushwa lakini kwa sasa, rushwa imekua kama ndiyo tafsiri ya maisha ya Tanzania. Hakuna kitu kinachoweza kufanyika kwa urahisi hata kama ni haki ya mtu, bila kutoa rushwa,” anasema.
Anaongeza kuwa: “Mwalimu Nyerere alikua ni rafiki ya baba yangu na walikua wakionana na kuongea, nakumbuka siku moja kulikuwa na sherehe nyumbani na kwa kuwa tulikuwa watoto, nilimhudumia chai Mwalimu.
“Nakumbuka Mwalimu aliwahi kumuuliza baba yangu; Lini Malaria itaisha nchini hii? Baba alimjibu kuwa, kamwe malaria haitaisha ikiwa hakutakuwa na kujitolea kwa kila mmoja wetu, bila kumtegea mwengine,” anasema.
Katika kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Dar anaishauri Tanzania iendeleze misingi ya maisha ambayo Hayati Mwalimu Nyerere aliisimmamia, ikiwamo umoja na mashikamano, ili kuondoa tofauti kubwa kati ya maskini na matajiri.
“Tunaona namna ambavyo matajiri wanendelea kuwa tajiri zaidi, wakati maskini wanazidi kudidimia. Kama kungekuwa na ushirikiano kati ya watu hawa wawili, tofauti kati yao ingekuwa ndogo au isingekuepo kabisa,” anaeleza.
Anashauri pia kuwepo na sanamu za utambulisho ya Baba wa Taifa kila mahali, ili kulienzi jina lake liishi milele. “Kwa ninavyomjua Mwalimu natamani jina lake liishi milele na litangazwe lijulikane dunia nzima,”anasema.
Mohammed Iqbal Dar aliazaliwa mwaka 1944 jijini Tanga, ni mtoto wa tatu kati ya watoto saba wa Tufail Ahmad Dar.
Dar ni baba wa mtoto mmoja, ambapo kwa zaidi ya miaka 40 sasa amekuwa akiishi nchini Uingereza alikoenda kwa ajili ya kusoma kabla ya kuwa raia wa nchi hiyo.
Mbunifu huyo wa jina la Tanzania ni Mhandisi wa Masuala ya Redio, kazi anayoifanya nchini Uingereza, akieleza kuwa katika kuienzi nchi yake, nyumba yake iliyopo mjini Birmingham, ameipa jina la Dar es Salaam, ikiwakilisha ubini wake, pamoja na Jiji la Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi
 
UNAPOTAJA historia ya nchi Tanzania, ni dhahiri kwamba hutaacha kutaja majina ya wapigania uhuru na viongozi mbalimbali walioiongoza tangu enzi za ukoloni, hadi kupata uhuru.

Hata hivyo, katika kila historia ya taifa lolote iliyojengwa, kuna watu waliofanikisha historia hiyo, lakini kwa sababu moja au nyingine, michango ya baadhi yao imesahaulika na pengine kutotajwa kabisa kwenye historia hizo.

Wengi wa Watanzania tunafahamu kuwa jina la nchi yetu Tanzania, limetokana na majina ya nchi mbili zilizoungana na kuwa moja ambazo ni Tanganyika na Zanzibar. Hivi ndivyo tulivyofundishwa shuleni.

Wengine wanaamini kuwa Rais wa kwanza na muasisi wa taifa hili, Hayati Mwalimu Julius Nyerere ndiye aliyebuni jina la Tanzania.

Lakini ukweli ni kwamba, jina la Tanzania lilibuniwa na mmoja wa wananchi walioshiriki mchakato wa kutafuta jina la nchi hii, baadaya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.

Mohammed Iqbal Dar ndiye aliyebuni jina la Tanzania, wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 akiwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzumbe.

Ilikuwaje?

"Nilikuwa maktaba najisomea, nilishika gazeti la Daily News, wakati huo likiitwa The Standard, ndipo nikaona tangazo hilo," anaeleza Dar alivyopata hamasa na kuongeza:

"Siku hiyo hiyo, nikafanya majaribio ya kutafuta jina bila hata ya kuishirikisha familia yangu. Nilichuka karatasi na kalamu, lakini kabla sijaanza kufanya chochote, nilimwomba Mungu aniwezeshe kwa maana naamini Mungu, ndiye kila kitu wakati wa kufanya jambo lolote."

"Kwa hiyo kwenye ile karatasi nikaandika Tanganyika na Zanzibar kisha, nikaandika majina yangu mawili; Iqbal na Ahmadiya," anasema Dar na kufafanua kuwa Iqbal ni jina lake na jina la ubini na Ahmadiyya ndiyo dhehebu lake.

Kupata jina Tanzania

Akisimulia alivyopata jina Tanzania, anasema kuwa ilimchukua dakika tano tu kufikiria na kulipata jina hilo.

"Nilichukua Tan kutoka kwenye Tanganyika na kuongeza Zan kutoka kwenye Zanzibar na kupata Tanzan, niliona halitimii vizuri,"anasimulia Dar.

Anabainisha kuwa baadaye alifikiria na kugundua kuwa majina mengi ya nchi za Afrika yanaishia na IA mfano akitoa mfano wa Ethiopia, Gambia, Tunisia, Nigeria, Algeria, Somalia, Zambia, Namibia na kwamba baada ya kubaini hilo aliamua kuongezea herufi hizo mbili na kupata jina Tanzania.

"Nilituma maombi yangu katika shindano hilo, bila kumwambia mtu yeyote nyumbani," anasema Dar.

Baada ya muda mfupi baba yake, mzee Tufail Ahmad Dar, alipokea barua kutoka Wizara ya Habari na Utalii (wakati huo), ambapo ndani yake kulikuwa na ujumbe wa pongezi ya kwamba kijana wake ameshinda katika shindano hilo.

"Wakati naandika, sikuwa na matumaini kama nitashinda kwa kuwa shindano hilo lilikua wazi kwa watu mbalimbali, hivyo sikuwa na tarajio lolote kama ningeshinda,

"Jioni wakati narudi nyumbani, baba mzazi alinifungulia mlango wakati si kawaida yake kwani mama ndiye alikuwa akinifungulia siku zote, hapo nikajua kuna kitu hakipo sawa. Lakini, nilikaribishwa na tabasamu la baba, pamoja na pongezi nyingi, nilifurahi sana," anaeleza.

Tuzo

Dar anasema kuwa kwa ushindi huo, alitunukiwa ngao pamoja na fedha taslimu Sh200 kama zawadi ya ubunifu wake.

Pamoja na kuibuka mshindi wa ubunifu huo na hadi leo jina la Tanzania alilolibuni yeye linaendelea kutumika, lakini Dar anadai kuwa mchango wake huo kwa taifa ni kama hautambuliwi na Serikali imemsahau katika kuandika historia ya taifa la Tanzania.

"Sijui kwa nini sitambuliwi tangu wakati huo? Hakuna chochote kinachoelezea uhusika wangu katika kupata jina la Tanzania na ukiwauliza watu, wengi watakwambia ilikuwa ni Nyerere aliyeleta jina Tanzania, hii inaumiza," anasema akilalamika.

Tanzania ya sasa

Baada ya miaka 13 tangu kufariki kwa Nyerere, Dar anasema kuwa Tanzania haimtendei haki mwasisi huyo wa Taifa, ambalo ni kisiwa cha amani.

"Ni kama imepita miaka mingi sana tangu kifo chake. Watanzania wamesahau kila kitu alichokiota Mwalimu Nyerere. Nakumbuka moja ya vita kubwa aliyopigana ni dhidi ya rushwa, yeye aliichuki rushwa lakini kwa sasa, rushwa imekua kama ndiyo tafsiri ya maisha ya Tanzania. Hakuna kitu kinachoweza kufanyika kwa urahisi hata kama ni haki ya mtu, bila kutoa rushwa," anasema.

Anaongeza kuwa: "Mwalimu Nyerere alikua ni rafiki ya baba yangu na walikua wakionana na kuongea, nakumbuka siku moja kulikuwa na sherehe nyumbani na kwa kuwa tulikuwa watoto, nilimhudumia chai Mwalimu.

"Nakumbuka Mwalimu aliwahi kumuuliza baba yangu; Lini Malaria itaisha nchini hii? Baba alimjibu kuwa, kamwe malaria haitaisha ikiwa hakutakuwa na kujitolea kwa kila mmoja wetu, bila kumtegea mwengine," anasema.

Katika kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Dar anaishauri Tanzania iendeleze misingi ya maisha ambayo Hayati Mwalimu Nyerere aliisimmamia, ikiwamo umoja na mashikamano, ili kuondoa tofauti kubwa kati ya maskini na matajiri.

"Tunaona namna ambavyo matajiri wanendelea kuwa tajiri zaidi, wakati maskini wanazidi kudidimia. Kama kungekuwa na ushirikiano kati ya watu hawa wawili, tofauti kati yao ingekuwa ndogo au isingekuepo kabisa," anaeleza.

Anashauri pia kuwepo na sanamu za utambulisho ya Baba wa Taifa kila mahali, ili kulienzi jina lake liishi milele.

"Kwa ninavyomjua Mwalimu natamani jina lake liishi milele na litangazwe lijulikane dunia nzima," anasema.

Mohammed Iqbal Dar aliazaliwa mwaka 1944 jijini Tanga, ni mtoto wa tatu kati ya watoto saba wa Tufail Ahmad Dar.

Dar ni baba wa mtoto mmoja, ambapo kwa zaidi ya miaka 40 sasa amekuwa akiishi nchini Uingereza alikoenda kwa ajili ya kusoma kabla ya kuwa raia wa nchi hiyo.

Mbunifu huyo wa jina la Tanzania ni Mhandisi wa Masuala ya Redio, kazi anayoifanya nchini Uingereza, akieleza kuwa katika kuienzi nchi yake, nyumba yake iliyopo mjini Birmingham, ameipa jina la Dar es Salaam, ikiwakilisha ubini wake, pamoja na Jiji la Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom