Asili ya Jina lako ni nini? Je, umeridhika nalo? Nilipigiwa kura

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,668
40,916
Hivi majuzi ikabuka hoja jamaa anadai mwanae anataka kubadili jina kisa hajavutiwa na aina ya matukio aliyokuwa nayo mwenye jina kama lake.

Mzazi anadai aliamua kumpa jina hilo mwanae baada ya kusoma hadithi za mhusika kwenye biblia.

Kwa muda mrefu sasa wazazi wamekuwa na haki ya kwanza ya kuwapa watoto wao majina.

Lakini je ni wote ambao wanayafurahia majina waliyopewa na wazazi wao? Je, kubadili jina ni kuwakosea wazazi heshima??

Mimi langu naambiwa kilifanyika kikao cha familia ikapigwa kura, jina lililopendekezwa na wengi ndio nililopewa, kwa kuzingatia hilo na kwa maana ya jina lenyewe nikaona ni sahihi kuwa nalo.

Majina hubeba maana kubwa sana kimaisha hivyo ni mihimu anayelibeba aridhike nalo. Je jamii iendelee na utaratibu huu huu wa kuwapa wazazi haki ya kuendelea kuwapa majina watoto wao, au majina wanayopewa watoto yawe ya muda tu kusubiria kuidhinishwa na mhusika pale anapofikia umri wa kufanya maamuzi??
 
Sijawahi sikia mtu anaitwa Yuda Iscariote hata kwa utani tu!

Sababu ni kuwa huyu jamaa ni msaliti. Lkn mmelishwa matango pori.

Huyo jamaa alikomboa ulimwengu. Asingekuwa huyu jamaa tusingepata Int. Bin msamaha wa dhambi.
 
Sijawahi sikia mtu anaitwa Yuda Iscariote hata kwa utani tu!

Sababu ni kuwa huyu jamaa ni msaliti. Lkn mmelishwa matango pori.

Huyo jamaa alikomboa ulimwengu. Asingekuwa huyu jamaa tusingepata Int. Bin msamaha wa dhambi.
lakini Yesu alisema ingalikuwa heri asingalizaliwA
 
I like my original name, siku nazaliwa Baba alipiga magoti kushukuru akawa anajiuliza ataniita nini likamjia wazo aniite N .. sifikirii kulibadilisha 😊😊😊
 
Kuna dada mmoja aliniita mtoto wake neighbour. Alikuwa hata maana yake hajui ila alisema hilo neno analipenda kwa kuwa la kizungu na lina sound perfect
 
lakini Yesu alisema ingalikuwa heri asingalizaliwA
Hapo kuna kigugumizi km alikuwa anaelekea kubaya kwa nini yesu hakutaka kumuokoa?

Akamuacha akaangamia? Tena alikuwa mpendwa zaidi ya wote.

Huyu bwana alitubu mpaka akafa hkn mtu Duniani aliyewahi kufikia hatua hii.

Na yuko mahali pake mpaka leo? "Ingelikuwa heri asingezaliwa" kwa majuto. Magumu yale aliyo pitia aliye muingia ni shetwani tu!

Hakuwa yeye ni ibilisi alimuingia. Ibilisi atakaa vipi karibu n nuru?

Yesu na sheitani ni watoto wa baba mmoja tatzo lenu wanadamu mnajichanganya sana.

Shtani na Mungu waaongea na kupiga swaga km kawa.

Kwanza mwenzenu alikuwaga ikulu ya mbinguni. Km ridhiwani na magogoni.

Sasa mtamtisha nini? Anamjua Mungu fika. Tatizo lenu mnafanya dhambi hata kumpita. yeye mpaka anawashangaa
 
Hivi majuzi ikabuka hoja jamaa anadai mwanae anataka kubadili jina kisa hajavutiwa na aina ya matukio aliyokuwa nayo mwenye jina kama lake.

Mzazi anadai aliamua kumpa jina hilo mwanae baada ya kusoma hadithi za mhusika kwenye biblia.

Kwa muda mrefu sasa wazazi wamekuwa na haki ya kwanza ya kuwapa watoto wao majina.

Lakini je ni wote ambao wanayafurahia majina waliyopewa na wazazi wao? Je, kubadili jina ni kuwakosea wazazi heshima??

Mimi langu naambiwa kilifanyika kikao cha familia ikapigwa kura, jina lililopendekezwa na wengi ndio nililopewa, kwa kuzingatia hilo na kwa maana ya jina lenyewe nikaona ni sahihi kuwa nalo.

Majina hubeba maana kubwa sana kimaisha hivyo ni mihimu anayelibeba aridhike nalo. Je jamii iendelee na utaratibu huu huu wa kuwapa wazazi haki ya kuendelea kuwapa majina watoto wao, au majina wanayopewa watoto yawe ya muda tu kusubiria kuidhinishwa na mhusika pale anapofikia umri wa kufanya maamuzi??
Sula la majina ya watoto kusema kweli ni kizungumkuti. Nilikutana na visa vya watu wawili wakielezea maana na jinsi walivyopata majina yao.

1. Mmoja anatoka Mashariki ya mbali, anasema jina lake alipewa jina la mpenzi wa kwanza wa mama yake. Nikabaki najiuliza, baba mzazi analichukuliaje jina hilo? na kama mama anaamua kumpa mtoto jina la mpenzi wake wa kwanza, siku wakitutana amri ya sita itabaki salama?

2. Mwingine anatoka katika mojawapo ya visiwa vya bahari ya hindi, yeye anadai jina lake lilitokana na makubaliano ya wazazi baada ya kuona boti iliyokua inapita baharini. Hali hii inilitokana na ugomvi uliokuwepo wa kumpa mtoto jina ambapo baba mzazi alipendekeza jina la ex-wake ambalo mama hakukubali. Mtoto alikaa bila jina kwa miezi kadhaa hadi boti ilipoleta muafaka.

NB. Kumekuwa na imani ya mtoto kurithi/kufuata matendo ya mtangulizi wa jina lake; Kama alikua ni mwizi au mlevi vilevile mtoto anaweza kufuata tabia hiyo hiyo.
 
Back
Top Bottom