Roy, hili neno ni kweli kabisa.
Hebu angalia hapa ulione BOMA la kizamani. Utajua kwa nini hata Zizi liliitwa BOMA. Kwa jengo yanafanana sana. Inanikumbusha mwalimu wangu wa shule ya Msingi alikuwa akimwita Mzungu mmoja Von Little. Akacheka kuwa wazee zamani walikuwa wakisoma jina lake FON Little. Ukweli ni kuwa Wazee walikuwa sawa. Hili jina kwa KiDutch linasomeka FON na siyo VON kama linavyoandikwa. Ni sawa na gari la Volkswagen ambalo husomeka kama sikosei "Folks-Vagen" yaani gari la wanachi??? Kweli inabidi kuwa na heshima kwa wazee na kujifunza kutoka kwao.

Boma (enclosure - Wikipedia, the free encyclopedia)
 
Kuna mwenyeji mmoja wa Kigoma aliwahi kuniambia kuwa ktkt ziwa Tanganyika kuna samaki wawili mashuhuri sana ambao kwa kiha wanaitwa "Itanga" na "Nyika". Mmoja wao inasemekana ana umeme mkali.

K/hiyo, huenda neno "Tanganyika" limetokana na majina ya samaki hao.

Labda Mh. Zitto Kabwe anaweza kutueleza zaidi.

Mkuu Tz1,
Niliwahi kusikia historia hii ya jina Tanganyika (ziwa) kuhusishwa na samaki, lakini pia kuna wengine wanahusisha na maneno mawili ya TANGA na NYIKA.......
Je, inamaanisha kwamba nchi ya Tanganyika ilitohoa jina lake ziwa Tanganyika?
Kuna maelezo wikipedia ambayo hayaniingia sana akilini
The name 'Tanganyika' is derived from the Swahili words tanga meaning 'sail' and nyika meaning an 'uninhabited plain' or 'wilderness'. At its simplest it might therefore be understood as a description of the lake — 'sail in the wilderness'.
 
Mkuu Tz1,
Niliwahi kusikia historia hii ya jina Tanganyika (ziwa) kuhusishwa na samaki, lakini pia kuna wengine wanahusisha na maneno mawili ya TANGA na NYIKA.......
Je, inamaanisha kwamba nchi ya Tanganyika ilitohoa jina lake ziwa Tanganyika?
Kuna maelezo wikipedia ambayo hayaniingia sana akilini

Kwa kweli hata nami nilishawahi kusikia hayo khs Tanga na Nyika, lkn sijapata uthibitisho wowote kuhusiana na hilo, na hata hili la samaki.

Aidha, sifahamu khs utohoaji wa jina Tanganyika.
 
Moshi check rail kwenye rail cross wakapaita chekereni.

Kilimanjaro = Mlima cha Mungu kama ilivyo Oldonyo lengai?
 
Moshi check rail kwenye rail cross wakapaita chekereni.

Kilimanjaro = Mlima cha Mungu kama ilivyo Oldonyo lengai?

Kwa kimasai Oldonyo=mlima, Ngai=mungu...ni kweli kwamba oldonyo lengai ni 'mlima wa mungu' (Kwa hiyo hatupaswi kusema 'MLIMA OLDONYO LENGAI', labda?)

Kilimanjaro sidhani kama kuna mungu katika hili jina (i stand to be corrected) kwa wachaga (uwezekano mkubwa ni kwamba ni jina hili lilitokana na kichaga) mungu anaitwa ruwa. Nilishawahi kusikia kwamba Kilimanjaro ilitakiwa imaanishe 'kilichoshinda wengi' au 'kilelema kyaro', kwa maana wachaga walishindwa kuupanda mlima ule......
 
Moshi = ni Kijerumani Moschee = Msikiti. Huenda wajerumani waliukuta msikiti hapo. Ndiyo maana
kuna Old Moshi au kwa kijerumani "Alt moschee"

Arusha = Kimaasai La rusa = ng'ombe kijivu

Karatu = Kiyunani (the name of settler) (kratoo maana yake kutamalaki, kutawala)
 
Last edited:
Moshi = ni Kijerumani Moschee = Msikiti

Arusha = Kimaasai La- Arusha = ng'ombe kijivu

Karatu = Kiyunani (the name of settler) (kratoo maana yake kutamalaki, kutawala)

Mkuu asante....
Moshi/Arusha, I was clueless. Moschee (msikiti) na mji wa Moshi vina uhusiano gani?
But, once again thanx.
 
Pangani: Mwaka 1873 Sultani wa Zanzibar alipotiliana sahihi na Serikali ya Uingereza mkataba wa kusimamisha biashara ya utumwa, eneo la Pangani ya sasa ilitumika kama soko la magendo la utumwa kwa kupitia Kisiwa cha Pemba ilikukwepa manowari za Kiiingereza. Hivyo wakati watumwa wanapangwa kwa kuuzwa waliamriwa "jipangeni" Tunaambiwa hiyo ndiyo asili ya Pangani.
 
Kuna mwenyeji mmoja wa Kigoma aliwahi kuniambia kuwa ktkt ziwa Tanganyika kuna samaki wawili mashuhuri sana ambao kwa kiha wanaitwa "Itanga" na "Nyika". Mmoja wao inasemekana ana umeme mkali.

Huyu huenda ndio wale samaki wanaoitwa "eel" kwa Kiingereza, ana umeme mkali sana huyu.
Asante kwa historia hii mkuu.
Kwa historia niliyoisoma, Jina Dar Es Salaam limebadilishwa ile "EL" na kuwekwa "ES". Jina halisi laKiarabu lilikuwa Dar El Salaam, likiwa na maana ya Bandari salama.
 
Roy,
Asante kwa neno BOMA. Nilikuwa sifikirii kuwa ni neno la kizungu. Utasikia hata zizi wengine husema BOMA la Ng'ombe.

SERENGETI:- Ni Ardhi isiyo na mwisho (Endless land). Wamasaai walitembea na mifugo yao bila ya kufika mwisho. Hivyo wakaiita hiyo Mbunga Serengeti.

Ni kweli kabisa mkuu, ila wao wamasai wanatamka "SIRINGET", sie wabantu tunasema "Serengeti"

Tukuyu
Nilivyosikia historia, ni kwamba eneo hilo ilikuwa ni eneo la watu kukutana (kama mnada vile) na palikuwa na miti ya mikuyu (sycamore) ambayo ilikuwa haikui. Sasa wenyeji wakwa wanaita hiyo miti ya mikuyu isiyokua, "Tukuyu" kwa sababu "Hatukui".

Makambako
Inasemekana palikuwa na zizi kubwa sana ambalo lilikuwa linahifadhi madume ya ng'ombe (ambayo wenyeji Wabena huita Makambako), kwa ajili ya kuuza. Hio ndio asili ya jina hilo.
 
asanteni wachangiaji wote, mnatufanya sasa tuwashauri watoto nao kutembelea JF kwani kuna kila kitu (mtazamo wa kimaadili)
 

Kwa historia niliyoisoma, Jina Dar Es Salaam limebadilishwa ile "EL" na kuwekwa "ES". Jina halisi laKiarabu lilikuwa Dar El Salaam, likiwa na maana ya Bandari salama.

Kiambata "al" ktk Kiarabu (ambacho wkt mwingine hutamkwa el) ni sawa na definite article "the" ktk Kiingereza. Kuna baadhi ya herufi, kutokana na ugumu wake kimatamshi, hazikubali kiambata hiki ("al") km kilivyo. "Al" ikikutana na herufi hizo, herufi yake "l" huondolewa, na "a" iliyobakia huunganishwa na herufi ya kwanza ya neno linalofuata, huku herufi hiyo ikiwekewa uzito (kwa kufanywa double). Kwa mfano, herufi "s" ya kiarabu haikubali kutanguliwa na "al". Kwahiyo, neno lolote la kiarabu linaloanza kwa herufi "s" likitanguliwa na kiambata "al", basi herufi "l" ya "al" huondolewa, na "a" iliyobakia huunganishwa na "s" mbili. Hivyo, al salaam huwa assalaam -- Km ktk Assalaamu Alaykum - (The) Peace (of God) be upon you.

K/hiyo, Dar El Salaam, kutokana na kanuni zilizoelezwa hapo juu, si sahihi; bali Dar Es Salaam (kutokana na Kiarabu Daru Ssalaam -- badala ya Daru El Salaam) ndilo neno sahihi.
 
Dar es Salaam is derived from Bandar-ul-Salaam (the harbour of peace) or from Dar-ul-Islam or Dar-ul-Salaam (the land of peace, or since Dar means a country or a large house (the Abode of peace).
 
Kijiji cha Chekeleni.

Kuna reli imepita katikati ya barabara baada ya Mombo kupita kama unaelekea Moshi. Kuna kijiji kinaitwa Chekeleni sehemu hiyo. Historia ya jina ni kuwa, kuna reli ina pita pale katikati ya barabara, sasa kiliwekwa kibao kinasema Check Rail , ila ndugu zetu iliwawia ugumu pale, wakaja na Chekeleni!

Kisura kuna kijiji cha Chekereni (Check Train) na Kijiji cha Chekelei (Check Rail)
 
Kiambata "al" ktk Kiarabu (ambacho wkt mwingine hutamkwa el) ni sawa na definite article "the" ktk Kiingereza. Kuna baadhi ya herufi, kutokana na ugumu wake kimatamshi, hazikubali kiambata hiki ("al") km kilivyo. "Al" ikikutana na herufi hizo, herufi yake "l" huondolewa, na "a" iliyobakia huunganishwa na herufi ya kwanza ya neno linalofuata, huku herufi hiyo ikiwekewa uzito (kwa kufanywa double). Kwa mfano, herufi "s" ya kiarabu haikubali kutanguliwa na "al". Kwahiyo, neno lolote la kiarabu linaloanza kwa herufi "s" likitanguliwa na kiambata "al", basi herufi "l" ya "al" huondolewa, na "a" iliyobakia huunganishwa na "s" mbili. Hivyo, al salaam huwa assalaam -- Km ktk Assalaamu Alaykum - (The) Peace (of God) be upon you.

K/hiyo, Dar El Salaam, kutokana na kanuni zilizoelezwa hapo juu, si sahihi; bali Dar Es Salaam (kutokana na Kiarabu Daru Ssalaam -- badala ya Daru El Salaam) ndilo neno sahihi.

Mwanazuoni tafsiri hii ina tofauti gani na ya ule mji wa Brunei Darusalaam?
 
Kijiji cha Chekeleni.

Kuna reli imepita katikati ya barabara baada ya Mombo kupita kama unaelekea Moshi. Kuna kijiji kinaitwa Chekeleni sehemu hiyo. Historia ya jina ni kuwa, kuna reli ina pita pale katikati ya barabara, sasa kiliwekwa kibao kinasema Check Rail , ila ndugu zetu iliwawia ugumu pale, wakaja na Chekeleni!

Mkuu ni CHECK TRAIN na sio CHECK RAIL.
 
Kilimanjaro
Kwamba wazungu walipouliza jina la ule mlima wachaga wakasema Kilelema kyaro (maana yake kilichoshinda wengi), wazungu wakaandika Kilimanjaro... (Hii naomba kama kuna mtu anaweza kuthibitisha.
Manyara
Inatokana na minyaa?

BOMA
British Overseas Management Administration (hii niliipata kwa bwana mmoja wa makumbusho ya pale BwagaMoyo)

BTW: Nitaanza kuiita Carrier Corps badala ya Kariakoo....asante Kisura na Kitia ila historia mlizotoa zinatofautiana. But thanx.

Mkuu hiyo ya Kilimajaro imekaa vizuri.
Kilemakyaro = iliyoshindikana kupanda = Kilimanjaro
 
Basotu = Ziwa Jeusi
Basodesh = Ziwa Jeupe
Basodawe = ?

Haya maeneo yako huko Katesh, mkoani Manyara
 
Nafikiri kuna uhusiano wa maneno haya na jina KONDOA.
Mfano:-jaribu kuwa unaondoa herufi ya mwanzo mwa kila neno linalobaki.Nayo itakuwa kama ifuatavyo:-
KONDOA
ONDOA
NDOA
DOA
OA
A

yaaani hapo kwenye "A" unashangaa aaah kumbe ni kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom