Hivi umepata kujiuliza unapopita katika mitaa mbalimbali ya mjini Dar au mji mwingine wowote Tanzania, jina la mtaa au eneo husika limetokana na nini?
Kwa mfano, Kijito Nyama limetokana na nini? Au Mlalakuwa, Au Mtoni kwa Aziz Ali n.k, n.k. Labda utadhani imetokea tu ... just ipo ipo, hapana! Baadhi ya majina ya mitaa yana historia ndefu na yenye kukumbukwa hata kwa vizazi vijavyo.
Hapa napenda kuwahabarisha maana ya mtaa au eneo la nje kidogo ya jiji la Dar liitwalo Gongo la Mboto.Jina hili limetokana na nini? Nakumbuka nilipata kusimuliwa na mwalimu wangu mmoja miaka ile pale Tambaza Sekondari nikiwa kidato cha pili.
Alisema palikuwa na mzee mmoja mashuhuri ambaye alipata kuishi katika eneo hilo.Huyu jamaa alikuwa mkulima. Jina lake aliitwa Mboto. Siku moja alijilawa kwenda katika konde lake kwa ajili ya kujipatia riziki.
Wakati ule, maeneo yale yalikuwa na giza la mapori na vichaka kadhaa. Jioni yake asirudi nyumbani. Kesho yake hadi mchana Mboto haonekani.
Mbiu ikapigwa watu wakakusanyika,kilichofuata ni msako mkali wa kumtafuta mzee huyu.Baada ya siku kadhaa wakakuta nyayo za mnyama mkubwa mithili ya Simba na ishara ya purukushani kadhaa.
Walipochunguza zaidi wakafanikiwa kukuta Gongo ambalo alipenda kutembea nalo mzee huyu.Wakahisi kuwa Mboto huenda amekutwa na maafa ya kuliwa na Simba. Walichokiona pale ni Gongo lake,Ndipo hilo eneo hadi leo lajulikana kama Gongo la Mboto.
Tuhabarishane maana ya maneno mengine kama Msasani, Mikocheni,Mto wa Mbu n.k.
Kwa mfano, Kijito Nyama limetokana na nini? Au Mlalakuwa, Au Mtoni kwa Aziz Ali n.k, n.k. Labda utadhani imetokea tu ... just ipo ipo, hapana! Baadhi ya majina ya mitaa yana historia ndefu na yenye kukumbukwa hata kwa vizazi vijavyo.
Hapa napenda kuwahabarisha maana ya mtaa au eneo la nje kidogo ya jiji la Dar liitwalo Gongo la Mboto.Jina hili limetokana na nini? Nakumbuka nilipata kusimuliwa na mwalimu wangu mmoja miaka ile pale Tambaza Sekondari nikiwa kidato cha pili.
Alisema palikuwa na mzee mmoja mashuhuri ambaye alipata kuishi katika eneo hilo.Huyu jamaa alikuwa mkulima. Jina lake aliitwa Mboto. Siku moja alijilawa kwenda katika konde lake kwa ajili ya kujipatia riziki.
Wakati ule, maeneo yale yalikuwa na giza la mapori na vichaka kadhaa. Jioni yake asirudi nyumbani. Kesho yake hadi mchana Mboto haonekani.
Mbiu ikapigwa watu wakakusanyika,kilichofuata ni msako mkali wa kumtafuta mzee huyu.Baada ya siku kadhaa wakakuta nyayo za mnyama mkubwa mithili ya Simba na ishara ya purukushani kadhaa.
Walipochunguza zaidi wakafanikiwa kukuta Gongo ambalo alipenda kutembea nalo mzee huyu.Wakahisi kuwa Mboto huenda amekutwa na maafa ya kuliwa na Simba. Walichokiona pale ni Gongo lake,Ndipo hilo eneo hadi leo lajulikana kama Gongo la Mboto.
Tuhabarishane maana ya maneno mengine kama Msasani, Mikocheni,Mto wa Mbu n.k.
- Dar Es Salaam-Bandar u salam-Bandari Salama
- Kariakoo -Carier crop-wabebaji wa mizigo sokoni kariakoo waswahili wakashindwa na kuamua kuunga
- Msasani-Musa Hassan-Mnyapara aliyekuwa akisimamia mashamba ya katani ambaye asili yake ni Ntwala hivyo wamakonde wengi wakaamua kuja kumuomba kazi na kwa kwa kuwa walikuwa hawajui anapoishi waliuliza kwa Mucha Hachani....Msasani imeungwa
- Mikocheni-Michael Chain Mmiliki wa mashamba ya katani yalliyokuwa yanaanzai palipo na Daraja la John Selander (Salenda Bridge)
- Kawe-actaully ni Cow Way, barabara maarfuru kwa kusagwa ng'ombe kufikishwa hapo Tangaynyika Packers kwa machinjo hence Cow-way (kawe imeungwa)
- Kigogo (ni kigogo kabisa cha kuvuka pale kigogo mwisho kila jumaosi walikuwa wanakusnayika kukiweka.."jamani leo siku ya kigogo"...(leo pamejengwa daraja)
- Tabata...Muarabu aliyekuwa ananunua korosho kwa mali kauli na kuwaahdi wachuuzi waje siku fulani watalipwa kwa kuwaambi "hapana tabu tabata (utapata pesa yako) akabatizwa jina la Mwarabau Tabata....
- Ilala..linatokana na makaburi ya pale Karume ambako hakukua na mengine hivyo kila alasiri watu walikuwa wakienda kuzika na wimbo wa Haila Illallah!!! (ILALA)
- UBUNGO, bungoni, MIKOROSHINI NA MABIBO NI MITI MINGI YA MATUNDA HAYO KUPATIKANA MAENEO HAYO
- Kunduchi....mtu aliyeonekana kutembea uchi maeneo hayo.
Chanzo: Halmashauri ya Jiji la DSM-hISTORIA
1.KIBORILONI & KIBOSHO[MOSHI].
Kiboriloni ni neno lililotokana na maneno mawili KIBO ALONE. Hii ilikuwa sehemu ambapo wazungu walisimama na kuona kilele cha Kibo pekee bila kukiona kilele cha Mawenzi, Kibo na Mawenzi ni vilele vya Mt. Kilimanjaro.Kibosho lilitokana na maneno KIBO SHOW, hii ni sehemu ambapo Kibo kilionekana vizuri zaidi.
2.KARIAKOO.
Inasemekana Kariakoo ilikuwa kituo cha Askari wa kikoloni CARRIER COP, Wabantu wakarahisisha kwa kupaita Kariakoo.
3.KOLOMIJE[BUNDA].
Inasemekana mahali hapo alifika Mzungu aliyeitwa James.Yule Mzungu akataka watu wamwiite 'J' badala ya kutamka jina lote. Hivyo akawaambia CALL ME J, wabantu wakatamka KOLOMIJE na kutengeneza jina la lile eneo.
4.CHEKERENI[MOSHI].
Hili ni eneo ambapo barabara inakatiza kwenye reli.Sasa wazungu waliweka alama ya bararani ya tahadhari kabla ya kuvuka reli CHECK THE LINE, watu wakatamka CHEKERENI na kuliita hivyo lile eneo hadi leo.
5.NEWALA [MTWARA].
Inasemekana kwamba waingereza walipofika Mtwara walikuta kisima kilichojengwa na wajerumani ambacho kilikuwa cha kizamani kwa wakati huo.Hivyo walijenga kisima kipya na kukiita NEW WELL, watanganyika wakatamka NEWALA, hatimaye likawa jina la ile sehemu.
N:B SOURCE yake ni HEARSAY STORIES....unaweza kusahihisha ama kuongeza majina mengine.