Asili na Chimbuko la Makabila Yote Tanzania na Africa

"If you do not know where you come from, then you don't know where you are, and if you don't know where you are, then you don't know where you're going"-Terry Pratchett

Watu wengi weusi hatutaki kujua historia yetu. Tunauana, kuchukiana na kubaguana bila sababu na wakati sisi wote asili yetu ni moja.

Wachangiaji wako busy kwenye page za udaku.
Huwezi ulaniletea historia hiyo alafu ukaniambia kabila fulani ni ndugu zangu, ndugu kivip
Ukitaka kuleta historia hiyo rudi nyuma kabisa ufikie kwa wanae nuhu na ugundue kwamba sisi sote ni ndugu na tuishi hivyo popote duniani kwa amani na upendo kabisa
 
Heri ya Mwaka Mpya Great Thinkers,

Leo nimeamua kuja na huu uzi mahususi kwasababu ni mwisho wa mwaka na wengi wetu tunapenda kurudi makwetu. Wapare na Wachaga wataenda kwao Kilimanjaro, Wameru, Wambulu na Wamasai wataenda kwao Manyara na Arusha. Wasukuma, Wahaya na Wanyamwezi wataenda kwao Shinyanga, Bukoba, Tabora na Mwanza. Vile vile ndugu zetu Wanyakyusa watarud kwao Mbeya n. k nk. Kwahyo si vibaya tukajua sisi wote chimbuko letu ni nini hasa.

Lakini wengi wetu tumekua tukijivunia kurud ma'kwetu bila kujua sisi wote asili yetu ni moja. Watu wote wanaoishi East West and South Africa asili yetu ni moja na asili hyo ni BANTU. With exception ya makabila machache kama Wamasai, Watutsi ambayo asili yao ni NILOTIC. Na ukitoa wachache South Africa ambayo asili yao ni KHOISAN. Na ukitoa PYGYMY watu wafupi wa Congo. Na ukitoa watu kama wambulu ambao asili yao hasa ni AFROSIATIC

Sisi wote tunatokea West Africa maeneo ya Nigeria na Cameroon. Kutokana na ongezeko la idadi ya watu na kutafuta opportunities nyingine za ardhi kwa ajili ya Chakula tungaanza the great migration kutoka West Africa kuja Central Africa hadi ukanda wa Bahari ya East Africa na wengine wetu wakashuka hadi South Africa. Hii Great Migration ya Bantu people kutokea West Africa ilianza miaka 3,500 iliyopita.

Baadhi yetu walibaki Congo na kujiendeleza hapo na kufanya intermarriage na PYGYMY people, wengine wakaja Tanzania na Kenya wakachanganyika na kuoana na NILOTIC people waliotokea Sudan, South Egypt na Uganda na kutengeneza makabila kama Chagga, Sukuma, Nyakyusa, Masai, Pare n. k.

Wengine wakashuka chini wakaoana na KHOISAN na kutengeneza makabila kama Zulu, Ngoni na Shona and Ndebele.

Lakini ukichunguza asili yetu kabisa wote tunatokea Nigeria na Cameron. Na wote ethnicity yetu hata ki'genetics ni Bantu people.

Amani iwe nanyi katika kipindi hiki cha sikukuuu mkifiria mnapotokea.

Link hii hapa na mwenye kuongezea aongezee

[Bantu peoples - Wikipedia]
Basi poa mchagga
 
Huyo mzee kwenye kabila la wasukuma na wanyamwezi kakudanganya ..huyo mnyamwezi ni msukuma na ktk wasukuma ndo unapata wanyamezi..kumbuka ktk wasukuma kuna matabaka km matatu au manne kutokana na mda sina nitakuja kukutajia aina za wasukuma
haya tirilika lingosha
 
unachoongea ni kweli nina story nyingi zinazothibitisha hili na kwakweli ni vizuri baraza la sanaa likaratibu hii kitu.
nilikaa na mzee mmoja siku moja akanieleza kuwa hakuna kabila linaitwa wachaga, wengi ni wanasai waliochanganyika na makabila mengine ikiwemo wakamba,wajerumani,wahindi nk
asili ya wasukuma na wanyamwezi ni wasumbwa ambao asili yao ni senegal hivyo mpaka wanafika hapa wamepita na kuzaliana na mataifa mengi ikiwemo waarabu,wakongo,watusi,waganda nk. makabila haya yaligawanyika kwa wengine kuwa wafugaji na wengine wakulima na kabila kubwa ni wanyamwezi waliwakimbiza wasukuma mpaka ziwa nyanza najua mengi yatafuata baada ya hapa.
lakini swali la kizushi je ni kweli chief maliare ni mchaga au mjerumani? hili si swali zuri lakini tunapoendelea kutafuta ukweli na haya tuyajue.
Ina maana unasema kabla ya kuja wajerumani na wahindi hakukuwa na kabila la wachaga???? Sioni huo mwingiliano labda kwa sababu ya ule weupe wa wachaga ukadhani kuna huo mwingiliano.
 
Ina maana unasema kabla ya kuja wajerumani na wahindi hakukuwa na kabila la wachaga???? Sioni huo mwingiliano labda kwa sababu ya ule weupe wa wachaga ukadhani kuna huo mwingiliano.
Walikuwepo wamasai waliochanganyika na makabila mengine hakujawahi kuwa kabila la wachaga pekee
 
Kwa nilivosoma. Nadharia ninayohisi ni kuwa huyu mtu wa kale alianzia hapa Tz pale Olduvai wengine wakaenda kusini ndo hao wa Khoisan na wengine wakaanza kupanda kwenda kaskazini kufuata mto nile na kuanzisha himaya huko kama Misri, Kushi,Punt,Nubia,etc. Then wengine wakaendelea kwenda kaskazini na kusambaa na kuzaliana na binadama wa aina nyingine yaani Neanderthal na Denisovans...hapa ndo tukaanza kuwapata watu weupe sasa. KUMBUKA huyu alietoka afrika alikua ni homo sapiens. Hawa Neanderthal na Denisovans wameshapotea ila vinasaba vyao vipo kwa DNa za watu weupe bado.
 
Watu wa asili kabisa Tanzania ni wahazhabe na wasandawe, hawa ndo native people of Tanzania, kwa South Africa ni San na Khosa people ndo maana san-dawe na San majina yao yanaendana, na wanapatikana cental part of Tanzania
Mbona tunaaminishwa kuwa wenye asili ya Tanzania ni wagogo ss tuelewe vp?
 
Binadamu wa kwanza alitokea kwenye jamii ya nyani.

Ila ukitaka kujua kiini kabisa maisha yote duniani kuanzia mimea na wanyama wote duniani.

Baba yetu ni mmoja na hao baba zetu ni bacteria walioishi chini ya bahari miaka billion kadhaa iliyopita.

Common descent - Wikipedia
Sasa hapo kwenye binadamu wa kwanza ni nyani ndo pananifanya nikae kimya yani we ulikuwa nyani na nyani chanzo chake ni nini?
 
Hii nayo kali aiseee..... watu weusi walilaaniwa na Mungu wa Israel!!?? mpaka leo Africa haija recover?? hahaha sasa mbona si Biblia si Qur'an imeelezea juu ya hiyo historia?? wewe umeitoa wapi?

Na mbona hapo naona tu historia ya waafrika, waarabu na waebrania..... sijamuona Muzungu hao kipindi chote hicho alikua bado hajazaliwa?? lol... na je yeye ametokana na nani katika uzao wa hao watoto watakatifu.


Halafu sijaelewa kwani Noah na Abraham nani alianza kuja duniani???

Wazungu ni watoto wa Japheth. Noah ni babu wa mababu wa Abraham.
 
huu Uzi mbona unamadini mazito hivyo lakini ajabu hauna wachangiaji !!?
Huu uzi ulipaswa kuwa na ushahidi wa kisayansi hasa sayansi ya lugha kwa kumithilisha sarufi nzima ya lugha tajwa.
 
Mleta mada mi naweza kukubaliana na wewe, kwanza niweke wazi kuwa mi napenda kufuatilia mambo ya kale/historia. Katika kufuatilia historia ya ukoo wetu unaasili ya misitu ya Congo hadi ninavyo andika hili andiko nina masalia hai kwa mawasiliano ya ndugu Congo Brazaville, Congo Kinshasa, Burundi, Kigoma then wengine by 1800's wakatawanyika wengine wapo Tanga, Kilosa, Kilimanjaro n.k na hasa maeneo yalipokuwa mashamba makubwa ya Kikoloni (Katani na Kahawa). Na marehemu babu yangu aliibukia Ukinga alikomsindikiza rafiki yake mkinga kuhani msiba wa marehemu baba yake na hatimaye babu yangu akashindwa kurudi Tanga likawa chimbuko la uzao wangu!.
 
Kiongozi mfano lafudhi ya ya Watu wa Nigeria imefanana sana na lafudhi ya kichaga .wasikilize wanapokua wanaongea
 
Hapo kale nchi za afrika kaskazini zilikua za watu weusi. Waafrika weusi wa leo ndio uzao wa Ham (Mizraim, Cush and Phut). Leo hii wa canaan ni wachache sana au hawapo kabisa kwasababu wengi wao sana walishakufa zamani sana. Mizraim ni ancient Egypyt (wamisri wa kale), Cush ni ancient Ethiopia and Phut ni ancient Libya. Wahabeshi wa leo ni machotara wa kiafrika na kiarabu na hivyo hivyo wasomali. Uchotara huu unaweza ukawa wa miaka zaidi ya 2000.

Kibantu na ubantu ni very complex. Lugha ya kibantu ilikua lugha kuu (lingua franca) ya himaya hizo za kale za watu weusi kwa kipindi fulani kirefu sana. Kuna wabantu ambao ni ancient Egyptians, kuna wabantu ambao ni ancient Ethiopians na kuna wabantu ambao ni ancient Libyans. Kuna sehemu ya maneno ya kibantu ambayo ni maneno yaliyo tumiwa na Kizazi cha Noah kabla ya lugha kugawanywa kwenye mnara wa Babel.

Wabantu huenda inamaanisha watoto wa anu na antu, ambao ni miungu ya uwongo ya ancient Sumeria. Ancient Sumeria ipo Sehemu ya Iraq ya leo. Kumbuka kwamba himaya kama Assyria na Babylon zilikua na hamitic phase (Nimrod and company) na Semitic phase Senacherib na Nebuchadnezzar and company.

Makabila ambayo ni pure wafugaji kama wamasai ni direct vitukuu wa ancient Cush (ancient Ethiopians). Kuna uwezekano wamasai ni ancient sabeans, ancient sabeans ni sub-category ya ancient cush. Ancient Ethiopia ni Sudan ya leo, ingawa kuna vipindi vya kale zaidi ambapo ilikua pia sehemu za Iraq, sehemu ya Saudia na Yemen, saa ingine hadi sehemu ya India na sehemu ya cambodia.

Makabila ambayo yanachanganya kilimo na ufugaji na yana ishi karibia na mto Nile au Lake Victoria kama Waluo hawa watakua ancient Egyptians au ancient ethiopians. Kuna wabantu ambao ni ancient Egyptians (hususan wale wa river Nile and Lake Victoria area kama wahaya, wabaganda). Wachagga, Wakikuyu na Wakamba wanaweza kua ancient Egyptians au ancient Libyans, lakini kuna probability kubwa wakawa ancient Libyans. Mataifa ya ancient Libya, Egypt na Ethiopia yalikua na muingiliano mkubwa. Kuna vipindi virefu sana ambvyo mafarao wa Ethiopia na Libya walitawala Misri and vice-versa.

Kuna jamii za waafrika weusi (especially wamisri wa kale) ambazo huko zamani sana walikua wanamchukia na wanabishana sana na Mungu wa Israel (na watakatifu wake) na walikua na akili sana, mafanikio sana, utajiri mwingi sana na kiburi sana. Pia walikua wanapenda sana sensual sins.

Ina sadikika kwamba kutokana na ubishi na kiburi cha hawa jamaa, Mungu wa Israel ali waadhibu waafrika weusi kwa kuwashusha chini sana sana kimaendeleo kwa kipindi kirefu sana sana mpaka leo hii afrika haija recover sawa sawa. Kushushwa huko kulipelekea kuja kwa ukoloni, utumwa na kukaliwa kwa afrika kaskazini na watu wa jamii ya kiarabu (waarabu weupe, wa-semites).

Ham ndo alikua mtoto wa kwanza wa kuzaliwa na Noah, Shem alikua wa pili, Japheth alikua watatu. Canaan ndie aliefanya kosa lile, Noah akamlaani Caanan. Akampa Shem haki za mtoto wa kwanza na akambariki Japheth pia, Ham hakutajwa kwenye Baraka zile, lakini pia hakulaaniwa. So ikawa Shem, Ham and Japheth. Na Yesu akaja kupitia uzao wa Shem, Abraham, Isaac na Jacob. So the right of the first born son and the holy and royal line of the priest hood aliipata Shem. Wakristo kupitia Yesu ni warithi wa kiroho wa hiyo right of first born. Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles.

Japheth ni baba wa wazungu na Shem ni baba wa waebrania (waisraeli wa zamani), waarabu weupe na mataifa ya mashariki ya kati. Baada ya Kutawanywa kwa wajenzi wa mnara wa Babeli, Mungu wa Israel aliunda mataifa 70 ambayo yalitokana na Shem, Ham na Japheth. Na watu wote walioko duniani leo ni vitukuu vya hayo mataifa 70.


Utawala wa 'masiya wa kisiasa' wa Tanzania utakua na tabia zifuatazo
Nimependa bandiko lako ila nitofautiane kidogo sehemu inayosema watu weusi waliadhibiwa sijui kutokana sijui nini ...... na kuhitimisha kuwa ndio maana hata maendeleo yao yataendelea kuwa nyuma. Ukweli ni kwamba mtu mweusi hajawahipata changamoto kubwa kimaisha ukilinganisha na binadamu wengine au rangi zingine. Historia na sayansi vinatuambia binadamu alivyo kadri anavyo kumbana na changamoto ana tendency ya kubadilika kulingana na shida/adha/changamoto inayo mkabili. Nichukue mifano kidogo ya mashariki ya Kati na Tanzania. Jamii Kiyahudi ni jamii iliyopata shida sana upande wa maadui kwa tafsiri yao wajikuta wakiwa watu wazuri sana ktk mambo ya kiulinzi na kiuchumi hapa naomba pitia nyaraka/makala mbali mbali. Kwetu Tz tupitie jamii chache miaka ya nyuma zilizopitia changamoto mbali mbali hapa nitagusia baadhi ya makabila/jamii za Kichaga, Kinga, Waha, n.k, hapa hawa tutaangalia upande wa mambo ya kiuchumi. Jamii hizi kwa sasa zinakimbiza katika ujasiliamali kutoka na changamoto mbali mbali za nyuma walizokumbana nazo za kiuchumi hivyo lazima bongo zao zipo tuned kukabiliana na changamoto uchumi zilizokuwa zinakabili jamii hizo miaka hiyo!. Hivyo na basi binadamu anavumbua/fanya vitu kulingana na changamoto inayo mkabili kwa wakati huo.
 
Back
Top Bottom