sabasita
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 1,501
- 392
NIMETANGULIZA NENO MASIKINI SABABU NYIMBO YA SAIDA KAROLI IMETUMIKA KWENYE MOVIE YA TYLER PERRY IITWAYO PEEPLES ... NA CREDIT KWENYE WEBSITE YA IMDB ZINAONYESHA HIVI
Maria Salome
Written and Performed by Saida Karoli
Published by Westbury Music LTD
ATAKUWA KAPATA CHOCHOTE KWELI?
=============
PEEPLES: HII NDIO MOVIE AMBAYO WIMBO WA SAIDA KALORI ''CHAMBUA KAMA KARANGA'' UMETUMIKA
Wengi tulioangalia movie hii ya Marekani tumejiuliza wimbo wa Saida Kalori umewafikiaje. Maana ukiangalia movie hii mwanzoni mwanzoni kabisa wimbo chambua kama karanga unasikika na anaonekana mama akiucheza kama sehemu ya mazoezi.
Katika movie leo ya leo tena Zamaradi Mketema aliongea na Saida Kalori lakini hakuwa akijua chochote. Pia aliyewahi kuwa manager na producer wa Saida hakuwa akijua chochote zaidi ya kupigiwa simu kutoka Marekani na wanawe walioona hiyo movie.
Sitaki kuisimulia ni movie nzuri ya kuchekesha... Inamzungumzia kijana anayeenda ukweni kwa mpenzi wake na anakutana na changamoto nyingi kutoka kwa baba wa msichana na familia yake kwa ujumla.
Picha zinazopatikana katika movie hiyo.
Wale wa movies sijawasahau kama bado kuiona hii kaitafute ufurahi huku ukila popcorn, karanga na juisi.
Habari hii ni kwa hisani ya Mtangazaji Dina Marios