Asia darwesh dada mpiga kinanda ambaye kaacha rekodi ya pekee toka alipofariki 1995

MT255

JF-Expert Member
May 3, 2012
3,381
4,648
Jina Asia Daruwesh, sio jina geni kwa mashabiki wa muziki Tanzania na pengine Afrika mashariki kwa ujumla. Huyu Dada anaweza kutajwa kama mpiga kinanda wa kwanza kabisa mwanamke kuwahi kutokea kwenye rhumba letu la kitanzania ingawa siku za nyuma kuliwahi kuwa na bendi ya akinamama watupu ikiitwa Women Jazz ambayo kuanzia magitaa, masaxphones na kuimba walikuwa akinamama watupu. Asia Daruwesh alizaliwa mwaka 1964. Ingawa alikuwa na asili ya Zanzibar, maisha yake kwa kiasi kikubwa yalikuwa Zambia kuanzia utotoni hadi anakua na huko ndiko alikopata inspiration ya kuwa mwanamuziki. Kwa hapa kwetu Tanzania, jina la Asia Daruwesh lilisikika kwenye safu ya mwanzo kabisa ya King Kikii mwaka 1984 akiwa na Kikii mwenyewe, Mumba Kisi, Kapelembe Coco, Samba Wa Mikalay, Zahoro Bangwe, Mohamed Idd Control, Matei Joseph na wengine. Alishiriki kupiga kinanda kwenye nyimbo kadhaa za bendi hii iliyokuwa ikitumia mtindo wa Embalasasa Shika Break kama Kinyume, Dodoma Capital, Njimina, Mimi na we, Kibwanange, Malalamiko na nyingine kadhaa huku nyimbo kama Lamanda na Kitoto chaanza tambaa akimuachia Ally Hemed Star huyuhuyu ambaye leo anajulikana kama muimbaji na mtunzi mzuri wa Taarab. Hata hivyo mwaka 1986 mwishoni aliihama bendi hiyo na kujiunga kwenye safu ya mwanzoni ya MK Group wakati huo. Nyimbo karibu zote za kuanzia toleo la kwanza hadi la tatu la MK Group amepiga kinanda yeye. Hassan Rehani sijui anakumbuka nini ukimtajia MK Group!! Mwaka 1989 alikuwa miongoni mwa wanamuziki wanne walioihama MK Group na kwenda kuasisi Bicco Stars. Angekuwemo na Joseph Mulenga katika group hii lakini alirudi nyuma. Akiwa Bicco aliungana na akina Kinguti System, Fresh Jumbe, Athuman Cholilo Mashida, Seif Rengwe, Sid Morris, Mafumu Bilal, Andy Swebe Ambassadeur na wengine Katika bendi hii ndiko alikotunga wimbo wake wa kwanza wa Bwana Kingo na pia akashiriki kuimba na ameimbisha wimbo huo. Mwaka 1992 alianzisha bendi yake mwenyewe akiita Zanzibar Sound ikitumia mtindo wa Wesaka Dance akiwa na akina Bob Gad William, Hezron Ludala ama Bob Ludala, Fariala Mbutu, na baadaye akina Mohamed Idd Control na Shaban Lendi. Wimbo Banana ambao baadaye Bob Gad alikuja kuurudia akiwa na Twanga Pepeta ulirekodiwa kwa mara ya kwanza na bendi hii. Aidha wimbo Hadija ambao Fariala alikuja kuurudia na Kilimanjaro Connections ulirekodiwa nao huku Ludala akiwa muimbaji Kiongozi. Kufariki dunia kwa Asia Daruwesh ama kwa jina la utani Super Mama mwaka 1995 ndiko kulikohitimisha safari ya bendi hii. Ni hayo tu

Asia Darwesh kwenye kinanda pembeni yake ni Johnny Rocks kwenye drums. Haba wakiwa Bandari Grill- New Africa Hotel-enzi za Ngoma za magorofani

Shukrani kwa David mosha.
 

Attachments

  • 1400779793760.jpg
    1400779793760.jpg
    42.6 KB · Views: 188
Betty Enock, Titi Shangarai ,Shem Karenga wako wapi hawa ? Je kuna dancer mmoja anye ndio wa miaka ile alijulikana kwa kujiita Queen Clouds yuko wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom