dongo jeusi
JF-Expert Member
- Feb 9, 2017
- 248
- 210
Tumenyonywa vya kutosha
Nimekupata vizuri sana Mkuu ahsante kwa weledi wako mzuri kwa kufafanua bila jazba.UFAFANUZI MUHIMU KUHUSU USAJILI WA ACCACIA.
Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.
Kwa kutumia kigezo cha usajili, Tanzania tunazo aina kuu mbili za kampuni. Kampuni za ndani(Local companies) na kampuni za kigeni ( foreign companies).
Kampuni za ndani ni zile zote zilizoanzishwa hapa nchini na kusajiliwa hapa nchini. Hata kama wanahisa wake wote ni raia wa kigeni kwasababu tu ya kuanzishwa hapa na kusajiliwa hapa zinakuwa ni kampuni za ndani.
Kampuni ya kigeni ni ile iliyoanzishwa na kusajiliwa nje ya Tanzania lakini ikaanzisha ofisi/biashara/tawi hapa Tanzania. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni kifungu cha 433 kinasema hivyo. Kampuni kama imeanzishwa nje hata kama wanahisa wake wote ni Watanzania, hapa kwetu hiyo bado ni kampuni ya kigeni.
Kampuni ya ndani inaposajiliwa hupatiwa cheti cha usajili kiitwacho "Certificate of Incorporation" kwa mujibu wa kifungu cha 15(2) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya ndani inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na inatambulika rasmi kama kampuni ya ndani.
Kampuni ya kigeni inaposajiliwa hapa Tanzania hupatiwa cheti kiitwacho "Certificate of Compliance" kwa mujibu wa kifungu cha 435(1) Sheria ya Makampuni. Kampuni ya kigeni inapopata cheti hiki basi usajili wake huwa umekamilika na hutambulika rasmi kama kampuni ya kigeni.
Acacia ni kampuni ya kigeni. Kwa maana kuwa ilianzishwa nje ya Tanzania na kufungua shughuli zake hapa nchini. Kwa hiyo ili ihesabike imesajiliwa Tanzania ilitakiwa kuwa na cheti kiitwacho"Certificate of Compliance". Kutokuwa na cheti hiki maana yake ni kuwa haijasajiliwa Tanzania na haitambuliki.
Nimesikia mjadala BBC SWAHILI leo wanaojadili wakijiuliza inawezekanaje kampuni kubwa kama hii ikafanya biashara bila usajili. Watanzania wengi pia wanajiuliza swali hili.
Jibu lake ni hili. Acacia ni kampuni tanzu(Subsidiary Company) ya Barrick. Kampuni inakuwa tanzu pale ambapo zaidi ya nusu ya hisa zake zinamilikiwa na kampuni nyingine. Ile inayomiliki huitwa "holding company" na inayomilikiwa huitwa "subsidiary company". Kwahiyo Barick ni " holding" wakati Acacia ni "subsidiary".
Barrick inamiliki hisa za Acacia 63.9%. Kwa kusema hivi maana yake Barrick ndiye mwenye Acacia. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizi zinahesabika kampuni mbili tofauti na kila moja inabeba wajibu na hatia zake yenyewe(its own responsibility& liability).
Basi kumbe kilichotokea ni kuwa Acacia walikuwa wakifanya biashara kwa jina la Acacia lakini wakibebwa na mgongo wa Barrick. Walijificha hapa na wakaweza kuishi bila usajili wa kwao kama wao. Walijibeba kwenye usajili wa Barrick.
Barrick wao wanao usajili na wanayo " Certificate of Compliance" ya kwao ambayo tayari wameitoa hadharani. Kwakuwa haya ni makampuni mawili tofauti kila moja inatakiwa kuwa na cheti chake kwa mujibu wa kifungu cha 487 Sheria ya Makampuni na kutokufanya hivyo ni kosa kabisa. Kwa hiyo hivi ndivyo ilivyowezekana kampuni hii kufanya biashara bila usajili miaka hii yote.
Adhabu ya kosa kama hilo ni kifungo jela. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2002, kifungu cha 472 kinasema hivyo.
Simple :ACACIA waliwa
honga Wafanya kazi wa serikali
Hawa Acacia ndio African Barick Gold Mine, walibadili jina mwaka 2014.
Hapo Kuna magazijuto mengi sana...
What is acacia,
What is Barrick
What is bulyanghulu gold mine limited
What is buzwagi gold mine
Who and what is pangea gold mine
Kuna uhusiano au muingiliano gani Kati ya hivyo vitu hapo juu kisheria...
Mimi na muunga mkono Raisi,ila namaswali mengi sana kichwani kwangu.Kama haikusajiliwa kwa nini serekali haijaenda kuwashtaki mahakamani kwa uvunjaji wa sheria?Je tumeangalia sheria zetu zinasemaje kuhusu usajili wa makampuni?loopholes za usajili wa makampuni ya kigeni na uwekezaji upo?na tunarekebishaje.Je kwa nini tunawaomba Accacia watubu ndio tuwasamehe waendelee na uchimbaji.Je tuna create mazingira ya kiwatishia na hofu ili waogope?kwa nini kama wamevunja sheria zote hizo za nchi isifutwe kabisa na kushitakiwa.Mwenye majibu anisaidia jana nilokuwa busy sana natafuta mlo wa familia sikusikiliza sana
Hili nchi la ajabu sana.
Lissu ndo aliwaambia msifanye kazi yenu diligently? BRELA, TRA, TMAA, DSE hawa woote hawakuona ACACIA wanafanya kazi kinyume cha sheria?Umesomeka Mkuu. Umemzidi uwezo Tundu Lissu kwa mbali sana
Ni nani sasa anayefungwa jela? Kampuni au shareholders au ni nani? Naomba kueleweshwa maana mie mweupe kwenye sheria.Adhabu ya kosa kama hilo ni kifungo jela. Sheria Na. 12 Sheria ya Makampuni iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2002, kifungu cha 472 kinasema hivyo.
Mimi na muunga mkono Raisi,ila namaswali mengi sana kichwani kwangu.Kama haikusajiliwa kwa nini serekali haijaenda kuwashtaki mahakamani kwa uvunjaji wa sheria?Je tumeangalia sheria zetu zinasemaje kuhusu usajili wa makampuni?loopholes za usajili wa makampuni ya kigeni na uwekezaji upo?na tunarekebishaje.Je kwa nini tunawaomba Accacia watubu ndio tuwasamehe waendelee na uchimbaji.Je tuna create mazingira ya kiwatishia na hofu ili waogope?kwa nini kama wamevunja sheria zote hizo za nchi isifutwe kabisa na kushitakiwa.Mwenye majibu anisaidia jana nilokuwa busy sana natafuta mlo wa familia sikusikiliza sana