Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 45
Asasi zapinga kanuni batili katika Sheria ya Maadili
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,April 25, 2008 @17:03
Habari nyingine
Tabata Dampo waendesha zoezi kutambua wamiliki
Mkakati wa udhibiti wa mafua ya ndege keshokutwa
Watano kesi ya kuua Polisi waachiwa huru
Asasi zapinga kanuni batili katika Sheria ya Maadili
Ndege iliyokodishwa na ATC siyo mbovu Waziri
Wizara yaeleza faida za ziara ya Bush
Mbunge ataka elimu ya wanawake wa miaka 40
Nafasi ya wabunge wilayani yafafanuliwa
Mbunge ataka barabara Mnazi Bay iwekwe lami
Shekifu: Uopoaji maiti Mererani utaendelea
ASASI tano zisizokuwa za kiserikali jana zilifungua kesi ya msingi kupinga kanuni batili katika sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.
Kesi hiyo imefunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupinga kanuni ya 6 (1) na (2) na kanuni ya 7 (2) (c) ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.
Mashirika yaliyofungua kesi hiyo ni Mtandao wa Asasi zilizo Kusini mwa Afrika zinazojishughulisha na Masuala ya Haki za Binaadamu (SAHRINGON), Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Asasi inayojishughulisha na Haki za Wanawake (KIVULINI) na Shirika la Kitaifa la Msaada wa Sheria (Nola) na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Ananilea Nkya, mashirika hayo yanadai kuwa kanuni hizo Kanuni ya 6 (1) na (2) zenye vipengele vinavyoweka vipingamizi visivyo vya lazima vya kumzuia mwananchi kuwa na haki ya kupata taarifa zinazotolewa na viongozi wa umma kuhusiana na rasilimali, mapato au madeni yao.
Taarifa za mali za viongozi zinapaswa kupokelewa na Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kama inavyoagizwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ibara ya 132 kifungu kidogo cha 4 na cha (5) (b).
Vifungu hivyo vya Katiba pamoja na mambo mengine vinampa mwananchi haki ya kupata taarifa za mapato, rasilimali na madeni ya kiongozi, ilisema taarifa ya Nkya. Nkya alidai kuwa lakini cha kushangaza kanuni ya 7(2) (c) inazuia mtu aliyepata fursa ya kuona mali za kiongozi wa umma kuzitangaza hadharani hivyo zinapingana na Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye vipengele (a), (b), (c) na (d) ambavyo vinampa uhuru raia wa Tanzania haki kuhusu habari.
Vifungu hivyo vinavunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 132 kifungu kidogo cha 4 na cha (5) (b) na pia kwenye Sheria hiyo ya Maadili Ibara ya 9, ibara ndogo ya (1) na Ibara ya 14, ambavyo vinatoa mwanya wa kufunguliwa kesi ya jinai kwa mtu au chombo chochote kitakachotoa taarifa kuhusiana na mapato, rasilimali na madeni ya viongozi wa umma.
Hivyo alisema mashirika hayo yamefungua kesi hiyo kuomba tafsiri ya Mahakama, kutamka kuwa kanuni 6 (1) (2) na kanuni 7 (2) (c) za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 kuwa ni batili kwa kuwa inapingana na Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo ni sheria mama ya nchi.
Kadhalika mashirika hayo yanaitaka Mahakama Kuu kutamka kuwa raia ye yote wa Jamhuri ya Muungano ana haki ya kupewa na kuchapisha taarifa kuhusiana na mapato, rasilimali na madeni ya viongozi wa umma bila vipingamizi mradi atatunza maadili na usalama wa Taifa, ilisema taarifa hiyo.
Mashirika hayo pia yanaomba nguvu ya Mahakama kutoa nafuu zozote zinazowezekana kuhakikisha kuwa masilahi ya umma wa Tanzania yanazingatiwa kutokana na sheria hiyo.
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,April 25, 2008 @17:03
Habari nyingine
Tabata Dampo waendesha zoezi kutambua wamiliki
Mkakati wa udhibiti wa mafua ya ndege keshokutwa
Watano kesi ya kuua Polisi waachiwa huru
Asasi zapinga kanuni batili katika Sheria ya Maadili
Ndege iliyokodishwa na ATC siyo mbovu Waziri
Wizara yaeleza faida za ziara ya Bush
Mbunge ataka elimu ya wanawake wa miaka 40
Nafasi ya wabunge wilayani yafafanuliwa
Mbunge ataka barabara Mnazi Bay iwekwe lami
Shekifu: Uopoaji maiti Mererani utaendelea
ASASI tano zisizokuwa za kiserikali jana zilifungua kesi ya msingi kupinga kanuni batili katika sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.
Kesi hiyo imefunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupinga kanuni ya 6 (1) na (2) na kanuni ya 7 (2) (c) ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.
Mashirika yaliyofungua kesi hiyo ni Mtandao wa Asasi zilizo Kusini mwa Afrika zinazojishughulisha na Masuala ya Haki za Binaadamu (SAHRINGON), Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Asasi inayojishughulisha na Haki za Wanawake (KIVULINI) na Shirika la Kitaifa la Msaada wa Sheria (Nola) na Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA).
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Ananilea Nkya, mashirika hayo yanadai kuwa kanuni hizo Kanuni ya 6 (1) na (2) zenye vipengele vinavyoweka vipingamizi visivyo vya lazima vya kumzuia mwananchi kuwa na haki ya kupata taarifa zinazotolewa na viongozi wa umma kuhusiana na rasilimali, mapato au madeni yao.
Taarifa za mali za viongozi zinapaswa kupokelewa na Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kama inavyoagizwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ibara ya 132 kifungu kidogo cha 4 na cha (5) (b).
Vifungu hivyo vya Katiba pamoja na mambo mengine vinampa mwananchi haki ya kupata taarifa za mapato, rasilimali na madeni ya kiongozi, ilisema taarifa ya Nkya. Nkya alidai kuwa lakini cha kushangaza kanuni ya 7(2) (c) inazuia mtu aliyepata fursa ya kuona mali za kiongozi wa umma kuzitangaza hadharani hivyo zinapingana na Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye vipengele (a), (b), (c) na (d) ambavyo vinampa uhuru raia wa Tanzania haki kuhusu habari.
Vifungu hivyo vinavunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 132 kifungu kidogo cha 4 na cha (5) (b) na pia kwenye Sheria hiyo ya Maadili Ibara ya 9, ibara ndogo ya (1) na Ibara ya 14, ambavyo vinatoa mwanya wa kufunguliwa kesi ya jinai kwa mtu au chombo chochote kitakachotoa taarifa kuhusiana na mapato, rasilimali na madeni ya viongozi wa umma.
Hivyo alisema mashirika hayo yamefungua kesi hiyo kuomba tafsiri ya Mahakama, kutamka kuwa kanuni 6 (1) (2) na kanuni 7 (2) (c) za Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 kuwa ni batili kwa kuwa inapingana na Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo ni sheria mama ya nchi.
Kadhalika mashirika hayo yanaitaka Mahakama Kuu kutamka kuwa raia ye yote wa Jamhuri ya Muungano ana haki ya kupewa na kuchapisha taarifa kuhusiana na mapato, rasilimali na madeni ya viongozi wa umma bila vipingamizi mradi atatunza maadili na usalama wa Taifa, ilisema taarifa hiyo.
Mashirika hayo pia yanaomba nguvu ya Mahakama kutoa nafuu zozote zinazowezekana kuhakikisha kuwa masilahi ya umma wa Tanzania yanazingatiwa kutokana na sheria hiyo.