Asasi ya Mjumbe wa Kamati ya Madini yapewa Mill 120 na Serikali!

Mafuchila

JF-Expert Member
Apr 29, 2006
751
65
Kikwete ampa John Cheyo milioni 120/-

Hivi kuna ndoa gani kati ya John Cheyo na serikali ya CCM?
Na Gladness Mboma

SERIKALI imetoa sh. milioni 126 kama mchango wake kwa ajili ya kuimarisha shughuli za Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).

Mwenyekiti wa UDP, Bw. John Cheyo alisema hayo jana Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge, alipozungumzia mgogoro wa Kenya.

Bw. Cheyo alisema fedha hizo walikabidhiwa jana Ikulu, Dar es Salaam na Rais Jakaya Kikwete, ambazo zitasaidia kuimarisha kituo hicho kinachopigania demokrasia nchini.

Alisema kwa muda mrefu sasa wamekuwa wakiiambia Serikali kuwekeza katika amani kwa kukutana na vyama vya Upinzani kuzungumzia amani na kuwekeza TCD.

Akizungumzia mgogoro wa Kenya, Bw. Cheyo alisema Watanzania wanapenda kuona watu hao wakikaa pamoja katika meza moja, ili kutatua migogoro yao.

"Nimewapongeza Wakenya kwa kuwaona wamekaa meza moja juzi na kuchagua Spika kwa utulivu na amani bila kuleta fujo na ninaamini mwendelezo huo utasaidia amani iliyokuwapo mwanzo kurejea upya," alisema Bw. Cheyo.

Aliwataka Wakenya wajaribu kutumia Bunge kutatua migogoro waliyonayo ili waweze kukaa pamoja kama ilivyokuwa mwanzo.
Source: Majira 17-01-2007
 
Kula na kulipa! kwani mmesahau mzee Cheyo alivyoimba sifa za Kikwete kule Bariadi? na jinsi ambavyo amekuwa upande wa CCM. Nadhani ni sehemu ya siasa, unawakuna huku na wao wanakukuna kule.. baada ya nyumba yake kukoswa koswa kupigwa mnada ilibidi asalimu amri!

Ndiyo tatizo la siasa za njaa!
 
Kula na kulipa! kwani mmesahau mzee Cheyo alivyoimba sifa za Kikwete kule Bariadi? na jinsi ambavyo amekuwa upande wa CCM. Nadhani ni sehemu ya siasa, unawakuna huku na wao wanakukuna kule.. baada ya nyumba yake kukoswa koswa kupigwa mnada ilibidi asalimu amri!

Ndiyo tatizo la siasa za njaa!

TCD ni Taasisi ya vyama vyenye wabunge. Cheyo ni Mwenyekiti tu. Kwenye mkutano mkuu wa CCM alijipendekeza tu hii taasisi ipewe fedha za serikali, ingawa inastahili kabisa kupewa ruzuku na serikali. Cheyo ufisadi wake ni tofauti kidogo, alihongwa na Barick enzi hizo. Na pia alihongwa kwenye IPTL. Ila kwa hili msimsingizie mwanawane. Yeye ni tarishi tu wa kupokea hizo fedha. Matumizi yake yapo chini ya Kikwete, Lipumba, Mbowe, Cheyo na Mrema. Hata nchi zingine duniani zina"TCD" zao. Mmenielewa eti jamani?

Asha
 
Kama alivyosema Asha, hii sio hongo wajama. TCD wamelalamika siku nyingi sana kwa kitendo cha kutegemea hela za wafadhili wa nje na waliitaka serikali watoe mchango wao. Hapa hakuna uhusiano wowote kati ya ujumbe wa Cheyo kwenye kamati ya madini na hizi hela.
 
ila mapenzi yangu na Mhe. Cheyo hayawezi kuiSha,Jamaa ni mpanga hoja mzuri na anapenda sana kusoma kwa makini jambo lolote linaloletwa Bungeni.Waulize wanaofanya naye Kazi watakueleza,nilishawahi kuzungumza naye kipindi Flani,Nafahamu dhamira yake ni nini,suala la kuuzwa Nyumba yake lilikuwa limekaa kisiasa na ndio maana Mzee Mkapa alikataa,
 
Back
Top Bottom