Gwiji wa Siasa Tanzania na Katibu Mkuu CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amefurahishwa na ukarimu wa watu wa Kigoma tangia aanze ziara ya kichama mkoani humo.
Akizungumza katika Baraza la Uongozi la Mkoa wa Kigoma kiongozi huyo wa kisiasa nchini alisema watu wa Kigoma wameonyesha mshikamano mkubwa na kupambana na wahuni wote waliokuwa wameagizwa kuvuruga ziara yake.
Kauli hiyo ya Dr Slaa inafuatia wahuni na wavuta bangi kujaribu kuvuruga mikutano yake lakini nguvu ya UMMA ilidhibiti hujuma hizo.
Wiki iliyopita watu walionyweshwa gongo na wengine walevi wa bangi waliandamana Kigoma mjini kulaani ujio wa Dr Slaa na kujiapiza endapo kama kiongozi huyo angekanyaga Kigoma mjini wangemdhuru.
Hata hivyo Dr Slaa aliingia Kigoma mjini kwa Kishindo kikubwa na kulakiwa na msururu wa magari na Pikipiki huku umati ukijipanga kandokando ya barabara na kupeperusha majani ya miti.
Kutokana na ujasiri wa Dr Slaa kupuuza vitisho vya wahuni hao baadhi ya watu wa Kigoma wamempachika jina la SIMBA WA TANZANIA.
Akizungumza katika Baraza la Uongozi la Mkoa wa Kigoma kiongozi huyo wa kisiasa nchini alisema watu wa Kigoma wameonyesha mshikamano mkubwa na kupambana na wahuni wote waliokuwa wameagizwa kuvuruga ziara yake.
Kauli hiyo ya Dr Slaa inafuatia wahuni na wavuta bangi kujaribu kuvuruga mikutano yake lakini nguvu ya UMMA ilidhibiti hujuma hizo.
Wiki iliyopita watu walionyweshwa gongo na wengine walevi wa bangi waliandamana Kigoma mjini kulaani ujio wa Dr Slaa na kujiapiza endapo kama kiongozi huyo angekanyaga Kigoma mjini wangemdhuru.
Hata hivyo Dr Slaa aliingia Kigoma mjini kwa Kishindo kikubwa na kulakiwa na msururu wa magari na Pikipiki huku umati ukijipanga kandokando ya barabara na kupeperusha majani ya miti.
Kutokana na ujasiri wa Dr Slaa kupuuza vitisho vya wahuni hao baadhi ya watu wa Kigoma wamempachika jina la SIMBA WA TANZANIA.