Gefu
JF-Expert Member
- Nov 30, 2010
- 6,930
- 2,554
Ndungu,
Naomba kwa heshima zoote kabisa nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa kazi nzuri sana inayo fanywa na chadema. Binafsi nimekuwa nikifuatilia sana kazi za chadema kama chama cha siasa na mwisho nimejiridhisha pa si na shaka kuwa mchango wenu katika maisha yetu watanzania ni mkubwa na wa kutukuka.
Maadui zenu wasiopenda ustawi wa chadema wamekuwa wakiwataja kila mara na kila hotuba. Unaweza kuona mkutano mkuu wa ccm ajenda kuu ilikuwa ni chadema na lowassa. Hakika chadema kazi yenu ni ya kutukuka. Nimejitahidi kufuatilia wale wote wanao pinga siasa kwamba hazileti maendeleo kinyume chake wao ndo wanaongoza kuwataja chadema, hongera sana cahdema.
Wapo waliojitahidi kudhibiti vyombo vya habari visiongee saisa, kisa chadema. Hii hofu kubwa namna hii dhidi ya chadema inatoka wapi wapendwa. Hakika kazi yenu ni kubwa sana.
Kila chama cha siasa kikiunganisha nguvu na chadema wakuu watafanya kila la ziada kukivuruga. vipo viapo vingi sana vya kuiua chadema lakini haifi. Asante chadema kwa kuwanyima usigizi ili tupate dawa mahospitalini. Mlipopiga kelele juu ya mabadiliko nao waliimba wimbo huo huo, asanteni sana chadema.
Ni meengi mmefanya na sasa mnaendesha kwa remote kama mtakavyo. Mkisema twende kulia watafuata tu na mkiamua kwenda kushoto nao watakuja.
Juhudi zenu zimefanikisha usafi wa taifa. kana kwamba haitoshi tamko lenu limefanikisha upandaji wa miti.
Ombi kwenu chadema mzidi kukaza uzi ili malaika nao waisome namba.
Naomba kwa heshima zoote kabisa nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa kazi nzuri sana inayo fanywa na chadema. Binafsi nimekuwa nikifuatilia sana kazi za chadema kama chama cha siasa na mwisho nimejiridhisha pa si na shaka kuwa mchango wenu katika maisha yetu watanzania ni mkubwa na wa kutukuka.
Maadui zenu wasiopenda ustawi wa chadema wamekuwa wakiwataja kila mara na kila hotuba. Unaweza kuona mkutano mkuu wa ccm ajenda kuu ilikuwa ni chadema na lowassa. Hakika chadema kazi yenu ni ya kutukuka. Nimejitahidi kufuatilia wale wote wanao pinga siasa kwamba hazileti maendeleo kinyume chake wao ndo wanaongoza kuwataja chadema, hongera sana cahdema.
Wapo waliojitahidi kudhibiti vyombo vya habari visiongee saisa, kisa chadema. Hii hofu kubwa namna hii dhidi ya chadema inatoka wapi wapendwa. Hakika kazi yenu ni kubwa sana.
Kila chama cha siasa kikiunganisha nguvu na chadema wakuu watafanya kila la ziada kukivuruga. vipo viapo vingi sana vya kuiua chadema lakini haifi. Asante chadema kwa kuwanyima usigizi ili tupate dawa mahospitalini. Mlipopiga kelele juu ya mabadiliko nao waliimba wimbo huo huo, asanteni sana chadema.
Ni meengi mmefanya na sasa mnaendesha kwa remote kama mtakavyo. Mkisema twende kulia watafuata tu na mkiamua kwenda kushoto nao watakuja.
Juhudi zenu zimefanikisha usafi wa taifa. kana kwamba haitoshi tamko lenu limefanikisha upandaji wa miti.
Ombi kwenu chadema mzidi kukaza uzi ili malaika nao waisome namba.