GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,876
Kwanza nianze kwa kutoa Pongezi zangu Kwenu Radio One ( hasa hasa ) Watangazaji wangu Bora kwa Afrika na Kipindi changu pendwa cha Mazungumzo ya Familia cha kila Jumapili kuanzia Saa 1 na Nusu hadi Saa 4 Kamli za Asubuhi kwa Kukubali Ubalozi wangu wa Kujiteua na Kulazimisha wa hicho Kipindi.
Pili niseme Asante kwenu Watangazaji wangu bora na Wapendwa wa Radio One na ITV na wana Simba SC wa 'Kutukuka' Wenzangu Farhia Middle na Abubakary Sadick kwa 'Kuniheshimisha' leo GENTAMYCINE mwisho wa Kipindi kwa Kunitaja na kunipa 'Dedication' ya Wimbo mzuri ambao ama hakika Umesindikiza vyema kabisa Siku yangu ya Kuzaliwa ( Birthday yangu ) ambayo ni leo tarehe 27 Machi.
Tatu niseme Asante mno kwenu Radio One na Watangazaji wangu Wapendwa na Bora Afrika Farhia Middle na Abubakary Sadick kwa Kuuheshimisha huu Mtandao wa JamiiForums hewani pale kila mlipokuwa mkinitaja GENTAMYCINE mkionyesha kuwa kumbe hata nyie huwa tunatiririka na kuserereka Wote hapa 24/7 tu.
Kama Balozi wa Kujiteua na Kulazimisha wa Kipindi kizuri cha Mazungumzo ya Familia kinachorushwa na Radio One kila Jumapili Saa 1 na dakika 30 Asubuhi hadi Saa 4 Kamili Asubuhi kikiwa chini ya Watangazaji wangu Bora Afrika Farhia Middle na Abubakary Sadick nawashauri wana JamiiForums Wote muwe mnatenga muda Wenu huo Kukisikiliza kwani Kipindi hicho ni Darasa tosha kwa walio ndani ya Ndoa, Mahusiano ya Malengo na hata Sisi wengine ambao tupo tupo Kuoa / Kuolewa hatutaki na tunabaki Kupuyanga puyanga tu.
Ukiona mpaka GENTAMYCINE nakipenda na nakisikiliza Kipindi fulani cha Redio basi jua ya kwamba kwa 100% kipo vizuri kina Elimisha, kina burudisha na kina Fundisha pia kwa kutoa Elimu mbalimbali juu ya Masuala mazima ya Mahusiano.
Mwisho Kwako Dada yangu Mpendwa Farhia Middle mwishoni umesema kuwa japo Unanikubali ila kuna muda huwa 'nawachenjia' na Kuwasema hivyo basi nami nakuambia hapa hapa JamiiForums kuwa hakuna Mtangazaji ninayempenda na sitaki aharibikiwe kama Wewe.
Nakupenda kuliko hata ujuavyo hivyo ukiona nakusema furahi kwani huwa nataka Unyooke na usiwe wa hovyo hovyo kama walivyo Watangazaji Wenzako wengi wa Kike katika Media zetu hapa Tanzania.
Kipindi chenu Nakipenda hamna mfano.
Pili niseme Asante kwenu Watangazaji wangu bora na Wapendwa wa Radio One na ITV na wana Simba SC wa 'Kutukuka' Wenzangu Farhia Middle na Abubakary Sadick kwa 'Kuniheshimisha' leo GENTAMYCINE mwisho wa Kipindi kwa Kunitaja na kunipa 'Dedication' ya Wimbo mzuri ambao ama hakika Umesindikiza vyema kabisa Siku yangu ya Kuzaliwa ( Birthday yangu ) ambayo ni leo tarehe 27 Machi.
Tatu niseme Asante mno kwenu Radio One na Watangazaji wangu Wapendwa na Bora Afrika Farhia Middle na Abubakary Sadick kwa Kuuheshimisha huu Mtandao wa JamiiForums hewani pale kila mlipokuwa mkinitaja GENTAMYCINE mkionyesha kuwa kumbe hata nyie huwa tunatiririka na kuserereka Wote hapa 24/7 tu.
Kama Balozi wa Kujiteua na Kulazimisha wa Kipindi kizuri cha Mazungumzo ya Familia kinachorushwa na Radio One kila Jumapili Saa 1 na dakika 30 Asubuhi hadi Saa 4 Kamili Asubuhi kikiwa chini ya Watangazaji wangu Bora Afrika Farhia Middle na Abubakary Sadick nawashauri wana JamiiForums Wote muwe mnatenga muda Wenu huo Kukisikiliza kwani Kipindi hicho ni Darasa tosha kwa walio ndani ya Ndoa, Mahusiano ya Malengo na hata Sisi wengine ambao tupo tupo Kuoa / Kuolewa hatutaki na tunabaki Kupuyanga puyanga tu.
Ukiona mpaka GENTAMYCINE nakipenda na nakisikiliza Kipindi fulani cha Redio basi jua ya kwamba kwa 100% kipo vizuri kina Elimisha, kina burudisha na kina Fundisha pia kwa kutoa Elimu mbalimbali juu ya Masuala mazima ya Mahusiano.
Mwisho Kwako Dada yangu Mpendwa Farhia Middle mwishoni umesema kuwa japo Unanikubali ila kuna muda huwa 'nawachenjia' na Kuwasema hivyo basi nami nakuambia hapa hapa JamiiForums kuwa hakuna Mtangazaji ninayempenda na sitaki aharibikiwe kama Wewe.
Nakupenda kuliko hata ujuavyo hivyo ukiona nakusema furahi kwani huwa nataka Unyooke na usiwe wa hovyo hovyo kama walivyo Watangazaji Wenzako wengi wa Kike katika Media zetu hapa Tanzania.
Kipindi chenu Nakipenda hamna mfano.