ROKY
Senior Member
- May 4, 2011
- 182
- 70
Ni muda kidogo umepita tangu niliposoma post ya Natalia(kama sikosei)akiomba ushauri kuhusu kupunguza uzito,watu wengi walichangia mengi,mimi pia yamenisaidia sana na nasema asante kwa mawazo yenu.nilisumbuliwa sana na uzito mkubwa na jitihada za kupunguza zikawa zinanichosha kwa kuona sipungui,kama mwezi hivi umepita nilipata kichomi ndani ya kifua upande wa kulia,nikaenda hospitali,nikapima kila kitu kipo sawa isipokuwa uzito,dokta akanishauri niache kula mlo wa usiku jambo ambalo nililizingatia na kuamua kuchukua wazo la member mmoja(bahati mbaya simkumbuki jina),yeye alisema ukitumia maji ya moto unaweka asali vijiko viwili na limao unakunywa asubuhi,saa nne,saa saba,saa kumi na saa mbili usiku,nimefanya hivyo na nimeacha kula usiku nimefanikiwa kupunguza kilo nne ndani ya mwezi mmoja,najua ni kilo chache lakini kwangu ni hatua kubwa.
Asanteni sana jf members,asante wewe ulie toa ushauri katika post ile ya natalia.
Tuendelee kuelimisha.
Asanteni sana jf members,asante wewe ulie toa ushauri katika post ile ya natalia.
Tuendelee kuelimisha.