Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu wanaArumeru,
Kwanza, nianze kwa kuwapongeza wananchi wa Arumeru kwa kazi nzito ya kupiga kura na kufuatilia kwa ukaribu wa uhesabuji na kuzuia kabisa mbinu chafu za kubadili matokeo na hatimaye kumwezesha kijana wenu na chaguo lenu kupata ushindi. Ushindi uliopatikana siyo wa chedema bali ni wenu wenyewe. Ninachotaka kuwahakikishia wanaArumeru ni kwamba mmechagua ushindi. Ushindi dhidi ya ccm ni ushindi dhiti ya ufisadi na ni ushindi dhidi ya umaskini. Kila mtanzania mpenda amani, mshikamano na maendeleo kwa sasa anatambua wazi kwamba kuichagua ccm maana yake ni kuchagua kushindwa jambo ambalo ningewashangaa sana mngefanya hivyo. Sasa, shirikianeni na kijana wenu katika kujiletea maendeleo yenu.
Pili, nimpongeze Meneja wa Kampeni, viongozi wote wa chadema, wanachama na wapenzi wote kwa ujumla wao ndani na nje ya nchi kwa jitihada zao zilizowezesha kupatikana kwa ushindi. Najua kazi imefanyika kubwa lakini kubwa zaidi ni mshikamano wenu wakati wa kampeni. Ushindi huu iwe ni chachu ya ushindi mkubwa wa uchaguzi wa 2015 na watanzania wengi ndiyo tunaousubiri kwa hamu kubwa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa.
Kwanza, nianze kwa kuwapongeza wananchi wa Arumeru kwa kazi nzito ya kupiga kura na kufuatilia kwa ukaribu wa uhesabuji na kuzuia kabisa mbinu chafu za kubadili matokeo na hatimaye kumwezesha kijana wenu na chaguo lenu kupata ushindi. Ushindi uliopatikana siyo wa chedema bali ni wenu wenyewe. Ninachotaka kuwahakikishia wanaArumeru ni kwamba mmechagua ushindi. Ushindi dhidi ya ccm ni ushindi dhiti ya ufisadi na ni ushindi dhidi ya umaskini. Kila mtanzania mpenda amani, mshikamano na maendeleo kwa sasa anatambua wazi kwamba kuichagua ccm maana yake ni kuchagua kushindwa jambo ambalo ningewashangaa sana mngefanya hivyo. Sasa, shirikianeni na kijana wenu katika kujiletea maendeleo yenu.
Pili, nimpongeze Meneja wa Kampeni, viongozi wote wa chadema, wanachama na wapenzi wote kwa ujumla wao ndani na nje ya nchi kwa jitihada zao zilizowezesha kupatikana kwa ushindi. Najua kazi imefanyika kubwa lakini kubwa zaidi ni mshikamano wenu wakati wa kampeni. Ushindi huu iwe ni chachu ya ushindi mkubwa wa uchaguzi wa 2015 na watanzania wengi ndiyo tunaousubiri kwa hamu kubwa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa.