Asante serikali kwa bajeti yenye kulenga zaidi walala hoi!!!

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
Serikali ya CCM imeandaa bajeti ambayo ina mlenga zaidi mlala hoi kwa maana ya kumpunguzia mzigo wa kodi huku ikiwabana wenye vipato vya kati na vya juu!!

Katika bajeti hii ya serikali ya mwaka 2013/2014, imeondoa kabisa kodi ama kupunguza kodi kwa kiwango cha kuridhisha kwenye maeneo fulani fulani ambayo yana athiri sana watu wenye vipato vya chini.

Maeneo ambayo serikali imeondoa kabisa kodi ama kuipunguza kwa kiasi cha kuridhisha ni kama ya yafuatayo;

1. Boda boda na Bajaj hakuna kodi, hivi ni vyombo vya usafiri ambavyo injini zao ni chini ya 501cc, vyombo hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa vijana wengi kwani vimeweza kuwapatia vijana vipato na kuwaletea maendeleo.

2. Mafuta ya taa hayata kuwa na ongezeko la kodi, kwa kutambua kuwa nishati hii inatumiwa sana na watu wa kipato cha chini, serikali itaendelea kutoza ushuru wa Tshs. 400/= kwa lita.

3. Ununuzi wa magari mapya marufuku, kwa kutambua kuwa gharama kubwa utumika kwa manunuzi ya magari mapya, serikali imepiga marufuku manunuzi ya magari mapya ili kupunguza matumizi ya kawaida.

4. Kodi ya mshahara itakuwa 13%-14%. Kilio cha muda mrefu cha wafanyakazi sasa kimesikika na serikali kuwapa unafuu kwa kupunguza kodi kwenye mishahara.

Ila kama ilivyo ada, hakuna zuri lisilo ambatana na lawama, dhihaka na kejeli, wapinzani na watu wasio na mapenzi mema na taifa wamelaumu eti hii bajeti itaongeza ukali wa maisha hasa kwa watu wa vipato vya chini. Haya maneno hayana ukweli wowote kwani dhumuni la hii bajeti ni kupunguza mzigo kwa walipa kodi ili kupunguza ukali wa maisha.

Aidha, watu wengi wanao lalama ni wenye vipato vya juu, kwani wengi wao wanajua kuwa kodi kubwa imeelekezwa kwao, hasa wale watumiaji wa mvinyo, kwa ule mvinyo wa dhabibu za nchini utatozwa sh 160 kwa lita badala ya sh 145, mvinyo wa dhabibu za nje ushuru umepanda kutoka sh 1641 mpaka sh 1775 kwa lita, huku vinywaji vikali vikitoka sh 2392 mpaka sh 2631.
 
Sometime kama hamjui kuchambua bajeti muwe mnasubiri wataalamu wa fedha na uchumi wachambue ili mpate mawazo ya kuandika.
 
NAONA UNAINGIZA SIKU WALA HUJUI UNACHOANDIKA HAPA. NIKUPE MFANO MDOGO TU KUKUONYESHA KUWA HIYO PAYE NI CHANGA LA MACHO;

MFANO MTU ANAYEPATA MSHAHARA WA SH 2,000,000 ANALIPA PAYE 491,600 AMBAYO NI SAWA NA PAYE YA 25% NA SIYO 13% UNAYODANGANYA NA HUYO MGIMWA WAKO.

"KUMBUKA PAYE SIYO FIXED FIGURE"

INGIA HAPA UPATE MAJIBU ZAIDI

Tanzania Revenue Authority - Calculators & tools
 
Nina hakika unatania unaposema bajeti hii imemfikiria mtu wa chini? Hivi umefanya uchambuzi punguzo la kodi kwa bajaji na gharama za kuiendesha - kwa bei ya mafuta tu? Au bajaji hizo zitatumia maji kujiendesha? Hivi sababu za mwaka jana mafuta ya taa na dizeli kukaribiana bei zimetoweka? I hope hatutaona wafanyabiashara wakianza kuchakachua tena mafuta kwa tofauti hii ya bei! Sina hakika kama kweli serkali imesema haitanunua magari mapya, kwa sababu hii haiwezekani! Una maana serkali itanunua mitumba? Kama ni hivyo basi gharama za kuendesha serkali zitakuwa juu zaidi.
 
4. Kodi ya mshahara itakuwa 13%-14%. Kilio cha muda mrefu cha wafanyakazi sasa kimesikika na serikali kuwapa unafuu wa kupunguza kodi kwenye mishahara.

Ila kama ilivyo ada, hakuna zuri lisilo ambatana na lawama, dhihaka na kejeli, wapinzani na watu wasio na mapenzi mema na taifa wamelaumu eti hii bajeti itaongeza ukali wa maisha hasa kwa watu wa vipato vya chini. Haya maneno hayana ukweli wowote kwani dhumuni la hii bajeti ni kupunguza mzigo kwa walipa kodi ili kupunguza ukali wa maisha.
Mkuu P, . HAMY-D, kadi siku zinavyozidi kusonga mbele unazidi kujidhalilisha hapa jamvini, jalibu kutulia, usi-panic fanya uchmbuzi taratibu, kisha tetea posho yako vizuri kwa hoja. angalia page45, bajeti kwa kiingereza.

ona hou usanii unaoutetea?
The current rates and the proposed rates are as follows as extracted from the budget attached;



Current Rates TOTAL INCOME
TAX RATES
Where total income does not exceed 2,040,000
NIL
Where total income exceeds Tshs. 2,040,000 but does not exceed Tshs. 4,320,000/=
14% of the amount in excess of Tshs. 2,040,000
Where total income exceeds Tshs. 4,320,000/=but does not exceed Tshs. 6,480,000/=
Tshs 319,000/= plus 20% of the amount in excess of Tshs. 4,320,000/=
Where total income exceeds Tshs. 6,480,000/=but does not exceed Tshs. 8,640,000/=
Tshs. 751,200/= plus 25% of the amount in excess of Tshs. 6,480,000/=
Where total income exceeds Tshs. 8,640,000/=
Tshs. 1,291,200/= plus 30% of the amount in excess of Tshs. 8,640,000/=



Proposed Rates TOTAL INCOME

TAX RATES
Where total income does not exceed 2,040,000
NIL
Where total income exceeds Tshs. 2,040,000 but does not exceed Tshs. 4,320,000/=
13% of the amount in excess of Tshs. 2,040,000
Where total income exceeds Tshs. 4,320,000/=but does not exceed Tshs. 6,480,000/=
Tshs 296,400/= plus 20% of the amount in excess of Tshs. 4,320,000/=
Where total income exceeds Tshs. 6,480,000/=but does not exceed Tshs. 8,640,000/=
Tshs. 728,400/= plus 25% of the amount in excess of Tshs. 6,480,000/=
Where total income exceeds Tshs. 8,640,000/=
Tshs. 1,268,400/= plus 30% of the amount in excess of Tshs. 8,640,000/=
 
Last edited by a moderator:
hao wa bodaboda na bajaj zitaanza kutumia maji nini? au hujui kwa bajeti hi petrol hainunuliki sasa,

mbaya zaidi uchakachuaji wa mafuta unarudi tena kwa kasi ile ile, si amepandisha petrol na disel akaacha mafuta ya taa!
 
Hii bajeti inaenda kumbana mlalahoi na atakuwa hoi zaidi. In fact kimahesabu iliyopungua ni kama 1,700 ambayo ni hela ya kununulia maji ya kunywa lita moja ya Kilimanjayo.
Moja, walalahoi hawana hata account benki. Wanategemea sana kutuma na kutumiwa pesa kwa njia ya simu, serekali imeamua kukata kodi hapo.
Pili, hata hivyo hivyo vibajaji vilikuwa havina ecise taxi, kwa hiyo hakuna kilichoondolewa. Kama huamini, bado nauli ya bajaji haitashuka bali itapanda kwa sababu kodi ya mafuta imepanda. Kwa hiyo hakuna kilichoongezeka, ni kiinimacho tu.
Nchi zinazojali wananchi wake huwa matajiri wanalimwa kodi kubwa kuliko masikini. Ukiangalia hii bajeti utakuta kuwa masikini anaenda kukamuliwa mpaka tone la mwisho. Vyanzo kama kodi za madini na utalii, kwa sababu mlalahoi haendi kufanya utalii, vingeongezwa kufidia hata angalau kutuma pesa kwa njia ya tigo-pesa na M-Pesa.
Misamaha ya kodi bado ni mingi kwa sababu wakubwa wana hisa kwenye hiyo misamaha. Nashangaa investors wanapewa misamaha ya kodi ili mlalahoi aendelee kukamuiwa. Nikupe mfano mmoja tu kuwa Dubai mtu wa nje akitaka kufungua duka, hakuna msamaha wa kodi, lakini mbaya zaidi lazima mwenyeji awe na share kwenye hilo duka. Kwa hiyo mgeni inabidi achukue mlalahoi mmoja ili ampe share tena inayotambulika sio ya kiudanganyifu.
Kwa bajeti za aina hii, usitegemee nchi kusonga mbele. Mgimwa bado hajafikiria jinsi ya kupunguza deni la taifa lakini bado kuendelea kukopa. Deni la trilioni 23 halijamtosha, ikiwa na maana kuwa vizazi vijavyo vitalilipa. Wanasema kuwa deni limeongezeka kwa sababu ya uwekezaji kwenye miundombinu, wakati CAG amesema deni limeongezeka kwa sababu ya matumizi ya kawaida ikiwa ni pamoja na kulipa mishahara.
Bajeti haionyeshi jinsi ya kupunguza matumizi yasiyo ya kawaida kama sitting allowances na chai maofisini.
 
mmmh cjaona unafuu kama petrori na dizel zinaathiri maisha ya watu wa chini tena sana tu na kodi imezidi kupandiishwa
 
Nasikitika sana kwa uelewa finyu wa mleta uzi. Unapopandisha bei ya petroli na diesel unampiga nyundo ya kichwa mlalahoi.

Kinachoniuma zaidi ni kodi ktk kuhamisha pesa kutumia mitandao ya simu. Wale ndugu zetu wa Kagunga na Mwamgongo na kule Kalema wataumia sana.

Ni heri wangeongeza kodi kwenye airtime, lkn kuweka kodi kwenye kuhamisha pesa ni kuumiza moja kwa moja mlala hoi
 
huyu angekuwa karbu ningemdotipile
Mimi ningemserukamba, huyu HAMY-D anawaza kiliberali.

Kwa mfano mdogo, kwa kuongeza bei ya petrol tayari wananchi wa hali ya chini ndio wameshaambiwa wasisafiri, wameshaambiwa wasisafirishe mazao yao, wasisage nafaka zao, wasiende sokoni maana kila kitu kitapanda bei kutokana na kupanda kwa gharama za usafiri.
 
Serikali ya CCM imeandaa bajeti ambayo ina mlenga zaidi mlala hoi kwa maana ya kumpunguzia mzigo wa kodi huku ikiwabana wenye vipato vya kati na vya juu!!

Katika bajeti hii ya serikali ya mwaka 2013/2014, imeondoa kabisa kodi ama kupunguza kodi kwa kiwango cha kuridhisha kwenye maeneo fulani fulani ambayo yana athiri sana watu wenye vipato vya chini.

Maeneo ambayo serikali imeondoa kabisa kodi ama kuipunguza kwa kiasi cha kuridhisha ni kama ya yafuatayo;

1. Boda boda na Bajaj hakuna kodi, hivi ni vyombo vya usafiri ambavyo injini zao ni chini ya 501cc, vyombo hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa vijana wengi kwani vimeweza kuwapatia vijana vipato na kuwaletea maendeleo.

2. Mafuta ya taa hayata kuwa na ongezeko la kodi, kwa kutambua kuwa nishati hii inatumiwa sana na watu wa kipato cha chini, serikali itaendelea kutoza ushuru wa Tshs. 400/= kwa lita.

3. Ununuzi wa magari mapya marufuku, kwa kutambua kuwa gharama kubwa utumika kwa manunuzi ya magari mapya, serikali imepiga marufuku manunuzi ya magari mapya ili kupunguza matumizi ya kawaida.

4. Kodi ya mshahara itakuwa 13%-14%. Kilio cha muda mrefu cha wafanyakazi sasa kimesikika na serikali kuwapa unafuu wa kupunguza kodi kwenye mishahara.

Ila kama ilivyo ada, hakuna zuri lisilo ambatana na lawama, dhihaka na kejeli, wapinzani na watu wasio na mapenzi mema na taifa wamelaumu eti hii bajeti itaongeza ukali wa maisha hasa kwa watu wa vipato vya chini. Haya maneno hayana ukweli wowote kwani dhumuni la hii bajeti ni kupunguza mzigo kwa walipa kodi ili kupunguza ukali wa maisha.

Aidha, watu wengi wanao lalama ni wenye vipato vya juu, kwani wengi wao wanajua kuwa kodi kubwa imeelekezwa kwao, hasa wale watumiaji wa mvinyo, kwa ule mvinyo wa zabuni za chini utatozwa sh 160 kwa lita badala ya sh 145, mvinyo wa dhabibu za nje ushuru umepanda kutoka sh 1641 mpaka sh 1775 kwa lita, huku vinywaji vikali vikitoka sh 2392 mpaka sh 2631.

mdau haya umeandika au umeandikiwa????acha utani wewe acha kabisa,,,
 
Tatizo letu wabongo huwa hatujadili issues kwa utashi wa uhalisia, kila kitu tunapiga siasa na ndo maana tunafeli.
Huyu sijui alikuwa kalala kaibuka na kumwaga -----.
 
Mkuu HAMY-D, kwa haya unayoyatetea hapa, nashawishika kuamini pasipo shaka kwamba wewe ni mmoja wao wa hao wanaofaidika na mfumo wa utawala uliopo. Ni bahati tu kwamba JF wanaturuhusu kuingia na ID hizi tunazotumia. Si vyema kuonyesha dharau za namna hii kwa watanzania walio wengi.
 
Last edited by a moderator:
Huyo Mlalahoi unayesema amefikiwa na hii bajeti ndiye atakayelipa nauli zaidi kwenye dalala na mabasi kwa vile serikali yako sikivu imeongeza kodi kwenye mafuta. Imeondoa kodi kwenye usajiri wa pikipiki lakini imeongeza shs 61 kwenye ushuru wa petroli ili huyu mlalahoi akamuliwe zaidi wakati anapanda bodaboda.

Lakini huku kwenye bodaboda si ndio ajira milioni moja za Kikwete zilipo na hao waajiriwa wamejaa kibao wodini wanauguza majeraha. CCM oyeeeee
 
Liuzi la ovyo kabisa sijui hata nimefungua la nini ngoja nisepe huyu jamaa nilimuambia tangu jana aache umbeya sio fani ya wanaume hasikii.
 
wewe ndugu mbona unanitafutia BAN bure. sitaki kubigwa ban ila kwahizi kauli zako nitakubali ban.
Serikali ya CCM imeandaa bajeti ambayo ina mlenga zaidi mlala hoi kwa maana ya kumpunguzia mzigo wa kodi huku ikiwabana wenye vipato vya kati na vya juu!!

Katika bajeti hii ya serikali ya mwaka 2013/2014, imeondoa kabisa kodi ama kupunguza kodi kwa kiwango cha kuridhisha kwenye maeneo fulani fulani ambayo yana athiri sana watu wenye vipato vya chini.

Maeneo ambayo serikali imeondoa kabisa kodi ama kuipunguza kwa kiasi cha kuridhisha ni kama ya yafuatayo;

1. Boda boda na Bajaj hakuna kodi, hivi ni vyombo vya usafiri ambavyo injini zao ni chini ya 501cc, vyombo hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa vijana wengi kwani vimeweza kuwapatia vijana vipato na kuwaletea maendeleo.

2. Mafuta ya taa hayata kuwa na ongezeko la kodi, kwa kutambua kuwa nishati hii inatumiwa sana na watu wa kipato cha chini, serikali itaendelea kutoza ushuru wa Tshs. 400/= kwa lita.

3. Ununuzi wa magari mapya marufuku, kwa kutambua kuwa gharama kubwa utumika kwa manunuzi ya magari mapya, serikali imepiga marufuku manunuzi ya magari mapya ili kupunguza matumizi ya kawaida.

4. Kodi ya mshahara itakuwa 13%-14%. Kilio cha muda mrefu cha wafanyakazi sasa kimesikika na serikali kuwapa unafuu kwa kupunguza kodi kwenye mishahara.

Ila kama ilivyo ada, hakuna zuri lisilo ambatana na lawama, dhihaka na kejeli, wapinzani na watu wasio na mapenzi mema na taifa wamelaumu eti hii bajeti itaongeza ukali wa maisha hasa kwa watu wa vipato vya chini. Haya maneno hayana ukweli wowote kwani dhumuni la hii bajeti ni kupunguza mzigo kwa walipa kodi ili kupunguza ukali wa maisha.

Aidha, watu wengi wanao lalama ni wenye vipato vya juu, kwani wengi wao wanajua kuwa kodi kubwa imeelekezwa kwao, hasa wale watumiaji wa mvinyo, kwa ule mvinyo wa dhabibu za nchini utatozwa sh 160 kwa lita badala ya sh 145, mvinyo wa dhabibu za nje ushuru umepanda kutoka sh 1641 mpaka sh 1775 kwa lita, huku vinywaji vikali vikitoka sh 2392 mpaka sh 2631.
 
Back
Top Bottom