Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Mhe. Rais, nakushukuru na kukupongeza kwa kutekeleza ahadi uliyotoa ukiwa ziarani mkoani Mwanza juu ya kuteua vijana tu kwenye nafasi ya U-Dc.
Mhe. Rais kwa hakika umedhamiria kwa dhati ya moyo wako kuleta mabadiliko makubwa kupitia vijana. Naamini vijana ni jeshi muhimu La mabadiliko kwenye nchi yoyote hivyo uwezo na ujuzi wao unatakiwa kutumika ipasavyo kama ambavyo umefanya.
Lakini Mhe. Rais, nafasi za wazee na watu wazima bado ni muhimu sana, bado tunahitaji ushauri wao na uzoefu wao katika ujenzi wa taiga letu. Naamini kuna baadhi ya wazee wameachwa ili vijana wawepo, wazee hao bado hawakutimiza umri wa kustaafu. Bado wanahitajika kwenye uongozi na utawala wako, nakuomba Mhe. Rais uwakumbuke waweze kulisaidia taifa hili.
Mhe. Rais kwa hakika umedhamiria kwa dhati ya moyo wako kuleta mabadiliko makubwa kupitia vijana. Naamini vijana ni jeshi muhimu La mabadiliko kwenye nchi yoyote hivyo uwezo na ujuzi wao unatakiwa kutumika ipasavyo kama ambavyo umefanya.
Lakini Mhe. Rais, nafasi za wazee na watu wazima bado ni muhimu sana, bado tunahitaji ushauri wao na uzoefu wao katika ujenzi wa taiga letu. Naamini kuna baadhi ya wazee wameachwa ili vijana wawepo, wazee hao bado hawakutimiza umri wa kustaafu. Bado wanahitajika kwenye uongozi na utawala wako, nakuomba Mhe. Rais uwakumbuke waweze kulisaidia taifa hili.