Asante Rais Mwinyi kuifutilia mbali sera ya kimasikini ya Ujamaa na kujitegemea ya Nyerere

Mm ile kusaidia nch za wenzetu kupata Uhuru kwa kutumia rasilmal zetu na kuingia vita ya kagera ndio apo babu nyerere ali fail....but r.i.p....kambarage
 
Kaka tusiongee kwa kuikosoa sera ya ujamaa kwa kuegemea kwenye mkabala wa kimagharibi tu hv mkuu ww sera ya ujamaa hujaona mazuri yk ona sera hii imeondoa ukabila na kuishi km ndugu unaoa utakapo na unaishi utakapo na omba nkuulize swali kwa mfano ubebari ungekufa kwny vita barid na USSR chini ya sera ya ujamaa ndo ikawepo unategemea leo tungekua hv tulivyo tungekua mbl kwa maan dunia nzm wangekua wanatumia sera ya ujamaa na cc tungekua mbl ila sera hii iliyumba na ukaiona haifai baada ya vita barid kuisha na USA chini ya mwamvuli wa ubebari kushnda ndo maan leo unaichukia ujamaa
 
Mwalimu alidhani Watanzania wote wanataka kuishi kama yeye anavyowaza!
Hakuwatendea haki wananchi kuziexperiment fikra zake kwenye maisha yao! Kwao ujamaa kilikuwa ni kitu kigeni zaidi kuliko ubepari
Kuna wakati mwalimu alitembelea mlimani kutoa mhadhara kuhusu ujamaa, Museveni wakati huo akiwa mwanafunzi akamuuliza kuwa, kama unasema ujamaa ni Lifestyle ya mwafrika na unatolea mfano kabila lako la zanaki kuwa kiasili ni wajamaa, basi mbona kabila hilo ni masikini, je kwa nini tujifunze kwa masikini ili kuwa na maendeleo?

Mwalimu akakwepa swali!
 
Mjo


Mjomba nani alikwambia mwinyi aliufuta ujamaa? Na kwa akili yako ndogo Unaona Ujamaa ni siasa hovyo kabisa lakini kumbuka kama si Ujamaa baba yako asingekuwa Kafka mjini na c ajabu ungekuwa maporini unawinda na kula matunda.

Kwa akili yako Unaona wote wanaomuenzi NYERERE hawana akili na hawajitambui? Hata hao mnaowasifu na kuwaona wametupita kimaendeleo wanamthamini kuwa alikuwa kiongozi thabiti pamoja na Elimu zao na hayo unayoona maendeleo waliyonayo.

Kwani mwinyi hawamuoni na hawamfahamu? Mbona hawa mtaji wala kumualika kwenye shuguli zao za ki taifa kama kweli ni Jabari la uongozi?

Acha ujinga dogo soma uelimike ufaham Dunia na mfumo yake ya maisha na unapoambiwa fulani anaenziwa jaribu kujitafakari na kujifunza ni kwa nini iwe hivyo. usiibuke na mipasho na viduku ukafikirl sote wajinga.
Katika Wajinga, nafikiri na wewe umo. Jina Nyerere ni wapi nilitaja. Changia mada iliyopo mezani. Kwamba eti kwa sababu tuliendea ujamaa ndiyo maana mimi siko porini na kwamba tungefuata sera za Kiwastani kama za Sweden au Norway basi mimi au familia yangu ingekua maskini ni hoja mufilisi. Haina mashiko. Kipekee lazima niseme Mzee Mwinyi atakumbukwa kwa Legacy ya kuruhusu bidhaa kuingia kutoka nje. Kama wewe hukubali siwez kukulazimisha. Lakini pia siwezi kukulazimisha kuwa ujamaa ulifika kipindi ukashindwa, siyo Tanzania tu hata huko China, ilibidi Mtu mmoja abadili kidogo maono ya Mao, na akachanganya Ujamaa wa Uwekezaji. Hadi leo, baada ya Mao, huyo ni mtu ni wa pili kwa kuwa na heshima nchini China. Kumbuka huyo alipingana kifalsafa na Mao ingawa wote ni Wajamaa.
Sasa nakushangaa kunilisha maneno amabayo sijayasema. Suala la kumuenzi baba waTaifa siyo uzi huu. Yeye anakumbukwa kwa mambo mengi tu mazuri. Kinachojadiliwa ni sera ya Ujamaa maeneo ambayo ilikosewa na nini mchango wa Mzee Mwinyi.
Kimsingi hoja yako ni BASELESS.
 
Back
Top Bottom