Wildlifer
JF-Expert Member
- May 12, 2021
- 1,883
- 5,186
Salaam WanaJF!
Baba wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kazi kubwa aliyoifanya katika utawala wake ni kujenga Taifa. Bara la Afrika mataifa yako machache sana, wengi wao ni nchi tu yaani kusanyiko la watu walio ndani ya mpaka mmoja, lakini ndani ya mipaka hiyo kila watu wana lugha zao, desturi zao, mambo yao, maono yao, changamoto zao, matarajio yao, fursa zao. Sisi kwetu ni watu tulio ndani ya mipaka ambapo tuna lugha moja, maono ya aina moja, matarajio ya aina moja na fursa za pamoja. Bila kujali dini zetu, rangi zetu, nasaba zetu, koo zetu, au mikoa yetu. Kinachotokea Mtwara leo, kinafanana na kinachowagusa watu wa bukoba kwenye sera za serikali. Tuko na taifa moja, lenye fursa sawa bila kujali unatoka wapi au jinsi yako ni ipi.
Nimekutana na picha hii mtandaoni ya Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na Viongozi wa Jumuiya ya Kikristo. Rais Samia ni Muislam, ni Mzanzibar na ni mwanamke. Jumuiya hiyo ni ya Kikristo. Ni jambo la nadra sana. Haitokei hata nchi zilizoendelea ambao kila siku wanajifanga kutuhubiria Demokrasia na usawa wa binadamu. Kule Marekani imewachukua miaka zaidi ya 200 kuwa na VP mwanamke. Kule Uingereza ni ngumu sana kuwa mkatoliki na ukawa kwenye UPM. Mimi binafsi kama feminist, kuona Tanzania tumefikia hatua hii kwenye picha hii, ni faraja kubwa. Picha hizi zinaeleza na kusema mengi.
Baba wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kazi kubwa aliyoifanya katika utawala wake ni kujenga Taifa. Bara la Afrika mataifa yako machache sana, wengi wao ni nchi tu yaani kusanyiko la watu walio ndani ya mpaka mmoja, lakini ndani ya mipaka hiyo kila watu wana lugha zao, desturi zao, mambo yao, maono yao, changamoto zao, matarajio yao, fursa zao. Sisi kwetu ni watu tulio ndani ya mipaka ambapo tuna lugha moja, maono ya aina moja, matarajio ya aina moja na fursa za pamoja. Bila kujali dini zetu, rangi zetu, nasaba zetu, koo zetu, au mikoa yetu. Kinachotokea Mtwara leo, kinafanana na kinachowagusa watu wa bukoba kwenye sera za serikali. Tuko na taifa moja, lenye fursa sawa bila kujali unatoka wapi au jinsi yako ni ipi.
Nimekutana na picha hii mtandaoni ya Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na Viongozi wa Jumuiya ya Kikristo. Rais Samia ni Muislam, ni Mzanzibar na ni mwanamke. Jumuiya hiyo ni ya Kikristo. Ni jambo la nadra sana. Haitokei hata nchi zilizoendelea ambao kila siku wanajifanga kutuhubiria Demokrasia na usawa wa binadamu. Kule Marekani imewachukua miaka zaidi ya 200 kuwa na VP mwanamke. Kule Uingereza ni ngumu sana kuwa mkatoliki na ukawa kwenye UPM. Mimi binafsi kama feminist, kuona Tanzania tumefikia hatua hii kwenye picha hii, ni faraja kubwa. Picha hizi zinaeleza na kusema mengi.