Ahsante Rais Samia, kwa hili Watumishi wa Umma tumekuelewa sana

Utangoja sana .. Haipungui miezi 6 mpaka mshahara kueffect cheo kipya. Vumilia tu
Pole sanaa TAGA.
Na pole kwa msiba wa kufiwa na baba.

Katibu mkuu utumishi (Ndumbaro) na waziri wa TAMISEMI (Ummy) walielekeza na kusisitiza kutochelewa kwa madaraja ili kutozalisha deni (arrears).

Huu ni utawala mwengine yule mnyima haki mwache ale vitasa za uzurimishi huko..!!!

#YNWA
 
Mzee mwenzangu concern yangu ni pale ulipokuja na sifa za kumtetea huyo mama as if malaika ametua madhabahuni.

Kingine, sijamaanisha kwamba unategemea mshahara tu, hata mimi sitegemei mshahara tu.

Halafu madeni ninayowadai nimeshayasamehe hizo faranga tumbueni tu huko juu, baada ya kuzungushwa kama mtoto kwenye madai yangu nimeshaapa kutopeleka nyaraka ya madai popote pale. Nimeridhika na mshahara wangu huu. Laki 2 zinanitosha mimi na familia yangu.


Sent using Jamii Forums mobile app
Relax bro...
The saviour has been born something will be alright.

Ameonyesha promise na maslahi ya watumishi hebu tumpe nafasi.

Yule mwenzake alibinya haki Tena kwasababu zake Ila huyu katoa ahadi Tena zenye deadline.

Tumpe muda ila mwanga amenionyesha.

#YNWA
 
Na nyie ndio mliokua mkitukatalia kutuandika kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

Usitake kumlaumu Mama kwa yasiyomuhusu. Tumuunge mkono mama mkuu. Kila mmoja atafikiwa tu.
Mkuu hakuna sehemu ambayo nampinga huyo mama yenu.

Pia siwezi kumpa sifa kwenye hamna.

Kuhusu kuandikwa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura kama mtumishi alikataa kukuandika kwa sababu zake binafsi na wewe ukakubali, basi wewe ndiyo una matatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukitaka kumuibia Mtanzania iba kidogo kidogo na kwa reja reja hawezi kukushtukia
Ndugu.
Pamoja na kumuelewa lakini pia tafakari na hii. PAYE imeshushwa kutoka 9% hadi 8% ni jambo jema lakini inawezekana isiwe na maana kushuka kwa sababu kama hizi.
1. Kodi ya laini za simu imeanzishwa jambo ambalo litahitaji ile hela ya punguzo kwenye PAYE.
2. Kodi ya majengo kupitia kununua LUKU ambapo utalazimika kulipa pale unapolipa bill ya umeme ukiwa kwenye nyumba ya kupanga au ya kwako.
3. Kuwepo kwa kodi mpya kwenye miamala ya simu kila unapotuma na kutoa hela.
4.Ongezeko la kodi kwenye bidhaa za mafuta ya dizeli na petrol ambapo gharama za usafiri na usafirishaji zinatarajiwa kupanda.

Kwa hizi baadhi ya kodi mpya ni vigumu kumuelewa mama kwani ni kama mtu amekukupunguzia shs. Mia kwenye hela unayopata ila atachukua elfu moja kwako.
 
Relax bro...
The saviour has been born something will be alright.

Ameonyesha promise na maslahi ya watumishi hebu tumpe nafasi.

Yule mwenzake alibinya haki Tena kwasababu zake Ila huyu katoa ahadi Tena zenye deadline.

Tumpe muda ila mwanga amenionyesha.

#YNWA
Mkuu tuombe Mungu atufikishe tena tarehe 01/05/2022.

Hadi muda huu ninapoandika tulitakiwa tuongezwe angalau 18% ya salary. Ila mama naye kama ilivyokuwa kwa mwendazake, kamute.

Na hiyo 18% ni kwa ajili ya manunuzi ya chakula na bills zingine. Sasa sijui kama hiyo mwakani ataongeza salary kwa 100%?

Juisi ni ileile kwenye chupa mpya. Mwanasiasa anaweza kukwambia mwakani na mwakani ikifika atabadili lugha akwambie ile board ya mishahara haijakamilisha kazi ya kutathimini aongeze mshahara kwa kiwango gani.

Natamani niandike mambo mengi ila naamini bado hautanielewa sababu una mahaba na wanasiasa ambao mimi nishawajua rangi zao halisi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanaouliza maswali kama haya ndio wamejaa JF , eti nae GT
Nakupuuza tu mkuu .Unajua swali langu kwa mlete uzi nilikuwa Na objective Gani?

Na ndio maana aliponijibu nilicheka kidogo kureflect nilichokitarajia.


Wengine ni Ma -HRO huku ndani usipuuze kila mtu.


Over!!
 
Pelekeni ujinga wenu wa ubinafsi huko, mnafikiri kila mtu kaajiriwa na serikali.
Nyinyi Mwendazake alikataa kuwapandisha madaraja na marupurupu kwasababu wengi ni majizi ya nchi hii,mnajitungia semina za ajabu ajabu kisha mnakula hela yetu ya kodi.

Watumishi wenyewe wavivu,wezi na wala rushwa wakubwa
 
Ila kiukweli ukisomaa sheria za utumishi, kwasasa nilistahili kuwa juu ya daraja hili nililopandishwa sasa, ila yule msukuma yule sijui anaenda kuongoza malaika gani wanaozuia haki za watu tena za kisheria.


Yule ni shetani,ibilisi na afe tena huko
 
Back
Top Bottom