As we run out of time and ideas, namna chache sana zinabakia za kuidhibiti COVID19 Tanzania

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,828
Moja kwa moja kwenye mada.

Ni kwa maslahi ya taifa hili na kwetu sote kuona kuwa covid-19 inadhibitiwa au hata kuuondoshwa kabisa nchini.

Huu ugonjwa ni hatari na kwa bahati mbaya zaidi, hauwezi kuondoka wenyewe pasipo na jitihada za kutosha kutoka kwetu na hasa serikali.

Duniani kote hata magaidi wasiokuwa na huruma wamelazimika kusitisha harakati zao zote katika kipindi hiki. Pia hata ambako vita vilikuwa vikirindima, silaha kwa sasa zimewekwa chini kuipa nafasi vita dhidi ya Corona kupiganwa kwanza vilivyo.

Ni kwa kutambua umuhimu huo, zimekuwapo jitihada mbali mbali za dhati tokea kwa wadau mbalimbali tangia awali mno, zenye mikakati iliyokuwa wazi ili kuona:

1. Corona haingii nchini, wakati ilipokuwa bado haijaingia nchini:

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine? - JamiiForums

(Uzi wa March 14 kabla ya Corona kuingia nchini)

2. Corona haisambai pale ilipokuwa imeingia tokea siku alipopatikana mgonjwa wa kwanza hapa nchini:

Corona ni uzembe wetu isingetufikia, na itatumaliza tusipoamka sasa - ukweli mchungu - JamiiForums

(Uzi wa March 20 baada ya Corona kuingia nchini March 16).

Jitihada zote (kama hizo) zimekuwa kila wakati na mikakati ambayo kwa #1 ufanisi wake ungepimwa kwa kuona ugonjwa hauingii nchini.

Wakati jitihada za #2 hapo juu ilipaswa kupimwa kwa kuona ugonjwa hausambai.

Mikakati iliyokuwa hapo, kwa #1 na #2 haikupewa umuhimu wowote na serikali. Serikali iliamua kufanya yake kwa namna yake.

Matokeo yake ugonjwa ukaingia na bado unaendelea kusambaa kwa kasi:

Kwenu: Ummy, Taskforces, mabibi na mabwana katika mapambano ya dhati dhidi ya Corona - JamiiForums

Kwa maana kamili kuwa mikakati waliyoamua wao kama serikali kuichukua, ilishindwa kutusaidia kuzuia ugonjwa kuingia na hata imeshindwa kutusaidia kuzuia ugonjwa huu kusambaa:

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO! - JamiiForums

Hata hapa tulipo imekuwa ikipendekezwa kuwapo kwa mwelekeo tofauti bila mafanikio huku maambukizi yakizidi kusambaa zaidi.

Umuhimu wa kuwa na mikakati mingine japo tukiwa tayari tumechelewa mno unazidi kukua zaidi na zaidi. Ni muhimu sana kwa kigugumizi kilichopo serikalini kuweza kuangaziwa vilivyo.

Hii ya maombezi, dawa za kienyeji na sasa dawa zisizothibitishwa tokea kokote kule, si uchaguzi unaotushawishi sote kama suluhu ya tatizo hili la kisayansi dhidi ya mausia yote tokea WHO na hata marafiki zetu.

Kwa mujibu wa Raila Odinga:

"Viongozi wa kanda wamekuwa wakitaka kushauriana na rais John Pombe Magufuli, bila mafanikio."

Kwa mujibu wa Cyril Ramaphosa:

"Jitihada zote za kumtaka mwenyekiti wa nchi za SADC kuitisha mkutano wa video baina ya wakuu wa nchi hizi kujadili masuala ya Corona zimegonga mwamba".

Kwa mujibu wa Kaguta Museveni:

"Alikuwa na mazungumzo marefu kuhusiana na suala la Corona na marais Kagame, Magufuli na Kenyatta. Katika wote, walikuwa na makubaliano mazuri isipokuwa kwa Dr. Magufuli."

Si sahihi kuendelea hivi wakati watu wanakufa na mkakati wa kuudhibiti huu ugonjwa vilivyo haupo:

Rais Magufuli kuhusiana na Corona bora ukachukua hatua bila kuchelewa zaidi unauweka uongozi wako njia panda - JamiiForums

Ni katika kutafuta uwezekano zaidi wa usalama wetu sote, mchango wa marais wetu wastaafu katika kushauriana, hauwezi kudunishwa (labda na misukule tu):

Waraka wa wazi kwa Marais wetu Wastaafu kuhusiana na hali ya Corona nchini - JamiiForums

Ni wazi kuwa tunaendelea kuishiwa mawazo kwani jitihada zote zilizokwishafanywa zimeaangukia kwenye masikio viziwi.

Ninawasilisha, Itifaki yote ikiwa imezingatiwa na hasa kwa kuutambua uwepo wote wa misukule.

Ukweli usiopingika, kwa mwendo huu tunakoelekea tunazidi kuishiwa mawazo.
 
Uzi wa March 14 kabla ya ugonjwa kuingia March 16 ulikuwa wazi kabisa:

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine? - JamiiForums

Lipi kati ya haya tuliweza kujifunza toka kwa wenzetu?

"1. Kuwekwa quarantine kwa wageni wote tokea nchi zenye kufahamika kuwa na wagonjwa kwa takribani siku 14 kabla ya kuruhusiwa kuingia katika nchi nyingine wanakotaka kwenda.

2. Ndege za moja kwa moja tokea nchi zenye wagonjwa zimesitishwa kuelekea nchi zingine.

3. Mikusanyiko ya watu: kwenye mashindano ya mpira, matamasha, makanisani, misikitini nk imesimamishwa.

4. Taratibu za mambo ya kodi kwa wananchi zimecheleweshwa kuwapa wananchi ahueni kwenye kujikimu kuhusiana na mdororo wa uchumi kwani takribani shughuli zote za uzalishaji mali zimesita.

5. Sehemu za wazi kwa ajili kunawa kujiweka salama zimewekwa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu.


6. Namba za simu za kupiga mtu anapojishuku kuwa na dalili za ugonjwa zimewekwa wazi."

Tumekuja kufunga anga baada ya mashirika yote ya ndege kusitisha safari zao. Hata tusinge funga hakukuwa kumebakia ndege zinazoruka.

Kwa maana nyingine anga liliendelea kuwa wazi hadi wote waliotaka kutuletea Corona kwa raha zao wakamaliza.

Na sasa mipaka nayo inaendelea kuwa wazi hadi pia wanaotaka kutuletea Corona kwa raha zao wamalize.
 
All starts here ,how comes a politician ana ongoza wizara ya afyia?
 

Attachments

  • Screenshot_20200509-190210.png
    Screenshot_20200509-190210.png
    268.9 KB · Views: 1
  • 20200509_191157.png
    20200509_191157.png
    41.8 KB · Views: 1
  • 20200509_191221.png
    20200509_191221.png
    45.2 KB · Views: 1
All starts here ,how comes a politician ana ongoza wizara ya afyia?

Mkuu unasomeka lakini suala hili lilikuwa common sense zaidi.

Ama kweli "common sense can also be not so common."
 
Uzi wa March 20 siku 4 baada ya ugonjwa kuingia nchini. Ushauri upi ikizingatiwa?

Corona ni uzembe wetu isingetufikia, na itatumaliza tusipoamka sasa - ukweli mchungu - JamiiForums

"Bila kuamuru watu wote kusalia majumbani, ugonjwa huu utakuwa bado upo upo sana nasi na utatutesa kweli kweli.

Serikali tutendeeni haki kwa kuwataka watu wote wasalie majumbani japo kwa siku 14 kwa kuanzia sote tuupime upepo unaenda wapi.


Huu ndiyo ukweli mchungu, tusipousema wazi wazi kama hivi tunakuwa hatujitendei haki sisi wenyewe."

Ilikuwa kuongezeka kwa lockdown ya siku 14 tu na leo hii tusingekuwa na wagonjwa wasiojulikana na mashule yangekuwa kazini.

Leo tuko hapa tukihesabu wafu:


Kwetu tunapohesabu wafu, wenzetu sasa wako kwenye kurejea maisha yao ya kawaida - JamiiForums

Kwa kweli inauma sana.
 
Mwisho wake ni mbaya, hapa ni kila mtu kujiongeza mwenyewe na kulinda familia yake kwa kadri atakavyoweza.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu unasomeka vyema kabisa. Pamoja na yote hayo, vita hivi hatutavishinda kwa vita vya mtu mmoja mmoja.

WHO anaona angalau watu 190,000 watapoteza maisha Afrika pekee yake.

God forbid kwa mwelekeo wetu huu, we are for the lion's share.

Inasikitisha sana.
 
Kilichobakia ni hiki wataalamu wanaita herd immunity acha ugonjwa usambae kila sehemu wa kufa wafe wa kupona wapone watengeneze hiyo kinga ya jumuiya ubaya wa huu mchakato una maumimu sana na utachukua muda mrefu pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilichobakia ni hiki wataalamu wanaita herd immunity acha ugonjwa usambae kila sehemu wa kufa wafe wa kupona wapone watengeneze hiyo kinga ya jumuiya ubaya wa huu mchakato una maumimu sana na utachukua muda mrefu pia

Sent using Jamii Forums mobile app


Huu utaratibu haukubaliki. Haukubaliki kwa namna yoyote. Ni muhimu kuwafahamisha hilo kwa kila hali.
 
Moja kwa moja kwenye mada.

Ni kwa maslahi ya taifa hili na kwetu sote kuona kuwa covid-19 inadhibitiwa au hata kuuondoshwa kabisa nchini.

Huu ugonjwa ni hatari na kwa bahati mbaya zaidi, hauwezi kuondoka wenyewe pasipo na jitihada za kutosha kutoka kwetu na hasa serikali.

Duniani kote hata magaidi wasiokuwa na huruma wamelazimika kusitisha harakati zao zote katika kipindi hiki. Pia hata ambako vita vilikuwa vikirindima, silaha kwa sasa zimewekwa chini kuipa nafasi vita dhidi ya Corona kupiganwa kwanza vilivyo.

Ni kwa kutambua umuhimu huo, zimekuwapo jitihada mbali mbali za dhati tokea kwa wadau mbalimbali tangia awali mno, zenye mikakati iliyokuwa wazi ili kuona:

1. Corona haingii nchini, wakati ilipokuwa bado haijaingia nchini:

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine? - JamiiForums

(Uzi wa March 14 kabla ya Corona kuingia nchini)

2. Corona haisambai pale ilipokuwa imeingia tokea siku alipopatikana mgonjwa wa kwanza hapa nchini:

Corona ni uzembe wetu isingetufikia, na itatumaliza tusipoamka sasa - ukweli mchungu - JamiiForums

(Uzi wa March 20 baada ya Corona kuingia nchini March 16).

Jitihada zote (kama hizo) zimekuwa kila wakati na mikakati ambayo kwa #1 ufanisi wake ungepimwa kwa kuona ugonjwa hauingii nchini.

Wakati jitihada za #2 hapo juu ilipaswa kupimwa kwa kuona ugonjwa hausambai.

Mikakati iliyokuwa hapo, kwa #1 na #2 haikupewa umuhimu wowote na serikali. Serikali iliamua kufanya yake kwa namna yake.

Matokeo yake ugonjwa ukaingia na bado unaendelea kusambaa kwa kasi:

Kwenu: Ummy, Taskforces, mabibi na mabwana katika mapambano ya dhati dhidi ya Corona - JamiiForums

Kwa maana kamili kuwa mikakati waliyoamua wao kama serikali kuichukua, ilishindwa kutusaidia kuzuia ugonjwa kuingia na hata imeshindwa kutusaidia kuzuia ugonjwa huu kusambaa:

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO! - JamiiForums

Hata hapa tulipo imekuwa ikipendekezwa kuwapo kwa mwelekeo tofauti bila mafanikio huku maambukizi yakizidi kusambaa zaidi.

Umuhimu wa kuwa na mikakati mingine japo tukiwa tayari tumechelewa mno unazidi kukua zaidi na zaidi. Ni muhimu sana kwa kigugumizi kilichopo serikalini kuweza kuangaziwa vilivyo.

Hii ya maombezi, dawa za kienyeji na sasa dawa zisizothibitishwa tokea kokote kule, si uchaguzi unaotushawishi sote kama suluhu ya tatizo hili la kisayansi dhidi ya mausia yote tokea WHO na hata marafiki zetu.

Kwa mujibu wa Raila Odinga:

"Viongozi wa kanda wamekuwa wakitaka kushauriana na rais John Pombe Magufuli, bila mafanikio."

Kwa mujibu wa Cyril Ramaphosa:

"Jitihada zote za kumtaka mwenyekiti wa nchi za SADC kuitisha mkutano wa video baina ya wakuu wa nchi hizi kujadili masuala ya Corona zimegonga mwamba".

Kwa mujibu wa Kaguta Museveni:

"Alikuwa na mazungumzo marefu kuhusiana na suala la Corona na marais Kagame, Magufuli na Kenyatta. Katika wote, walikuwa na makubaliano mazuri isipokuwa kwa Dr. Magufuli."

Si sahihi kuendelea hivi wakati watu wanakufa na mkakati wa kuudhibiti huu ugonjwa vilivyo haupo:

Rais Magufuli kuhusiana na Corona bora ukachukua hatua bila kuchelewa zaidi unauweka uongozi wako njia panda - JamiiForums

Ni katika kutafuta uwezekano zaidi wa usalama wetu sote, mchango wa marais wetu wastaafu katika kushauriana, hauwezi kudunishwa (labda na misukule tu):

Waraka wa wazi kwa Marais wetu Wastaafu kuhusiana na hali ya Corona nchini - JamiiForums

Ni wazi kuwa tunaendelea kuishiwa mawazo kwani jitihada zote zilizokwishafanywa zimeaangukia kwenye masikio viziwi.

Ninawasilisha, Itifaki yote ikiwa imezingatiwa na hasa kwa kuutambua uwepo wote wa misukule.

Ukweli usiopingika, kwa mwendo huu tunakoelekea tunazidi kuishiwa mawazo.
Hili tatizo linahitaji a rapid change of leadership. Tunahitaji mtu mwingine haraka sana achukue hatamu katikati ya janga hili la sivyo tutaangamia.
 
Kilichobakia ni hiki wataalamu wanaita herd immunity acha ugonjwa usambae kila sehemu wa kufa wafe wa kupona wapone watengeneze hiyo kinga ya jumuiya ubaya wa huu mchakato una maumimu sana na utachukua muda mrefu pia

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni kweli mkuu. Hii ndio strategy ambayo serikali yetu imeamua kutumia. Kuacha ugonjwa usambae nchi nzima mpaka watu wote wapate. Wenye kinga imara wapone, wasio na kinga wafe then ugonjwa uishe wenyewe. Kwa strategy hii wote tujiandae tuu maana hata ujilinde vipi kuna uwezekano ipo siku tu utakutana na corona maana mpaka ije iwapitie watu wote milioni 60 sio mwaka huu.
Nadhani mwanzoni serikali ilidhani kwamba huu ni upepo tu ambao utapita kama ambavyo mambo mengine hua yanapita ndio maana hawakuchukua hatua. Tuombe dawa ipatikane mapema laa sivyo ndio kama alivyosema mukulu kwamba huu ugonjwa tutaishi nao kama ukimwi.
 
Back
Top Bottom