Ndugu zangu wana JF,
Hivi karibuni nimesikia kuwa dawa za ARV (sijui kirefu chake nini) lakini ni zile zinazotumiwa na watu wanaoishi na VVU kuwa sasa hivi wafugaji wa kitimoto wanazitumia kunenepeshea au kulisha mifugo yao. Wafugaji wa Kyela nasikia ndio wanaotumia sana.
Nimeleta hoja hii hapa ili nijue kama ni kweli, maana watu kama "MFUKUNYUZI" wanaweza kuwa taarifa nzuri zaidi au wanaweza kutusaidia kufukunyua zaidi. Lakini cha muhimu ni kujua kama kunaweza kuwa na madhara yoyote kwa watumiaji wa chakula hicho mbali na hasara itakayopatikana kwa dawa kutowafikia wahusika.
nawasilisha
Hivi karibuni nimesikia kuwa dawa za ARV (sijui kirefu chake nini) lakini ni zile zinazotumiwa na watu wanaoishi na VVU kuwa sasa hivi wafugaji wa kitimoto wanazitumia kunenepeshea au kulisha mifugo yao. Wafugaji wa Kyela nasikia ndio wanaotumia sana.
Nimeleta hoja hii hapa ili nijue kama ni kweli, maana watu kama "MFUKUNYUZI" wanaweza kuwa taarifa nzuri zaidi au wanaweza kutusaidia kufukunyua zaidi. Lakini cha muhimu ni kujua kama kunaweza kuwa na madhara yoyote kwa watumiaji wa chakula hicho mbali na hasara itakayopatikana kwa dawa kutowafikia wahusika.
nawasilisha