Meale
Member
- Nov 24, 2009
- 91
- 0
Matokeo rasmi mpaka sasa Chadema inaongoza kata 10 kati ya kata 19. Tayari barabara kadhaa zimefungwa kutokana na watu kujaa wakishangilia. Mgombea ubunge wa Chadema Lema yupo katika kituo cha majumuisho ya kura wakati Dr. Buriani amekataa kupokea simu. Katka hali iliyowashangaza wengi diwani kata ya Kaloleni ambaye amefuga nywele (rasta) kijana wa miaka 26 Charles Philipo amemwangusha vibaya mgombea udiwani CCM ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM mkoa licha ya kampeni chafu zilizokuwa zinaendeshwa na CCM kwamba ni mvuta bangi kutokana na muonekano wake ulivyo.
Source: star tv.
Source: star tv.