Arusha: Wananchi walia na kituo cha mabasi makubwa ya abiria ya kwenda mikoani

Kuna Shamba La Marehemu Mathias Manga hapa Terrat Barabara ya Maweni eneo maarufu la Mapambazuko linafaa Kwa Stendi Kubwa Sana, Shule na Hospital. Naonalinamegwa megwa Kwa viwanja 10x10 ni hasara Kwa kweli. Serikali Ingelinunua lingekuwa Stendi ya Daladala Gari za Moromboo, Njiro na Uswahilini.
 
Hapoa Arusha wanaweza wakafanya mpango wakahamisha hayo makaburi nyuma ya stendi Ndogo kisha eneo lote mpaka huku stendi ndogo likiwa stendi kubwa ya mabasi.Yaani kuanzia hapo stadium kote kunakuwa ni STAND.Inawezekana kabisa
Mawazo gani haya?.
 
Arusha nadhani ndiyo jiji linaongoza kwa barabara mbovu za mtaani.

Huwa nashangaa sehemu kama Njiro hakuna hata barabara moja yenye lami,, kwa Mrombo, Mianzini, moshono kote hali ni hiyo hiyo.
 
Ushauri mbovu sana huu. Kwa hiyo mtu anayetoka moshi kwrnda karatu, ashukie USA apande dala dala mbili hadi kisongo ili apande gari la kwenda karatu? Maana kubwa ya kuwa na stand kuu ni kurahisisha pia connection.
Aaah wapi? Hilo wazo la huyo jamaa ni wazo jema sana kama litafanyiwa kazi. Impact yake kiuchumi ni kubwa mno
 
Arusha ndio mnataka kuifananisha na Mwanza kweli?

Arusha inapambana na miji kama Musoma, Geita, Katoro, nk. Kahama sasa sio level za Arusha tena.

Soon senta kama Kagongwa ama Runzewe zinaipita Arusha.
Huu nao ugoro. Income per capita ya mwanza kwa mtu mmoja mmoja ikoje? Unaweza kuilinganisha na ya Chugastan?
 
Huu nao ugoro. Income per capita ya mwanza kwa mtu mmoja mmoja ikoje? Unaweza kuilinganisha na ya Chugastan?
wakati watu wanafundishwa darasani we ulikuwa miembeni ile wanagawanya pato lote linalopatikana kwa idadi ya watu sasa mwanza kuna watu wengi kuliko chuga ishu pambanisha pato la mkoa wacha ushamba wa wapi pato la mmoja mmoja nenda wilayani kuna mtu hata laki hajawai kushika unaongea ugoro hapa


mfano ukichukua billion gawana kwa million 2
na hyo billion moja gawanya kwa million 3 jibu linakuja sawa

hyo
 
Arusha nadhani ndiyo jiji linaongoza kwa barabara mbovu za mtaani.

Huwa nashangaa sehemu kama Njiro hakuna hata barabara moja yenye lami,, kwa Mrombo, Mianzini, moshono kote hali ni hiyo hiyo.
Arusha ulitoka huko mwaka gani?
 
Uliwahi kutembea nje ya arusha au hata hapo babati?
Ndugu yangu mi nina uzoefu na watu wa Arusha. Hawajui kuongea kwa hoja na wengi wao kwa sababu hawajawahi kutembea utakuta wanabishana tu kwa kulazimisha eti mji wa Arusha ni mkubwa kuliko Mwanza. Tuwavumilie tu ni Watanzania wenzetu.
 
Arusha ulitoka huko mwaka gani?
Kwani kibarabara kinachotokea mianzini kuelekea stand ndogo hadi stend kubwa huoni mashimo yake? Ufinyu wa barabara kutokea uwanja wa kisongo-kilombero-clock tower -round about ya kijenge huoni barabara ilivyo finyu na mapengo pembeni?
 
Mwaka huu. Mwezi uliopita
Hawezi kukuelewa mtu wa Arusha hajawahi kuamini kwamba mikoa mingine ni mizuri kuliko Arusha. Na hata watu ambao hawajawahi kwenda wanaamini Arusha ni kuzuri kuliko miji mingine ila wakifika tu pigo la kwanza ni bei za vyakula kabla hujakutana na nyumba za udongo Sanawari nyuma ya maduka.
 
Arusha ipo over rated sana.

Lakini pia serikali imefeli kabisa kuujenga huu mji.

Ilipaswa kabisa uweze kutoa ushindani na jiji la Nairobi.

Lakini umebakia kuwa jiji la hovyo,hata ukipita pale East Africa Hq, AICC ile barabara inatia aibu.

Ndio maana leo google,microsoft na int offices nyingi zinawekwa nairobi.
 
mji gani nje ya dar unabarabara ndugu kuizidi Arusha
Moshi wana barabara nzuri kuliko Arusha. Niambie kwa Arusha ukitoa hapo mjini ni wapi mtaani kuna lami. Zaidi ya barabara moja tu zinazoingia kwenye maeneo kama Morombo, Njiro, na Moshono ambako kote mitaani hakuna lami zaidi ya vumbi, mashimo na matope....jini lina barabara za changarawe😅😅😅
 
Arusha ndio mnataka kuifananisha na Mwanza kweli?

Arusha inapambana na miji kama Musoma, Geita, Katoro, nk. Kahama sasa sio level za Arusha tena.

Soon senta kama Kagongwa ama Runzewe zinaipita Arusha.

Acha utani mkuu, unaweza kuwa hujafika Arusha. Yani unalinganisha kahama na Arusha kweli? Daharau kubwa.
 
Arusha ipo over rated sana.

Lakini pia serikali imefeli kabisa kuujenga huu mji.

Ilipaswa kabisa uweze kutoa ushindani na jiji la Nairobi.

Lakini umebakia kuwa jiji la hovyo,hata ukipita pale East Africa Hq, AICC ile barabara inatia aibu.

Ndio maana leo google,microsoft na int offices nyingi zinawekwa nairobi.

Mbona Arusha mji mzuri, Seema serikali ndio haina mikakati mizuri.
 
Watakuambia walitengwa na utawala wa awamu ya tano! Wenzao kila kona stendi nzuri Morogoro,Dar,dodoma,singida,mwanza wanajenga mbili moja imekamilika na ya pili iko njiani kukamilika! Pia stendi ya Mabasi Mbeya ya ajabu ajabu hata siielewi! Hawa wana Mbeya wanamambo mengi vitendo zero!

Arusha na mbeya hazikuwa base ya CCM ndio maana.
 
Ili mji wa Arusha upanuke na ukue kwa haraka wahusika wazingatie yafuatayo:
1. Ondoa stendi na masoko yale pale mjini kati.
2. Stendi mabasi ya kutoka Dodoma road inatakiwa iwe Kisongo. Weka soko huko.
3. Stendi mabasi kutoka Moshi road iwe USA au Chekereni. Weka soko huko.
4. Stendi magari kutoka Nairobi iwe Ngaramtoni ya Juu. Weka soko huko.
5. Stendi magari kutoka Simanjiro/Kiteto iwe Oljoro. Weka soko huko.

NB: Lakini msije mkalalamika kuwa stendi na masoko yako mbali!
...na wasilalamike maana mjini patapoa kama makaburini
 
Arusha ndio mnataka kuifananisha na Mwanza kweli?

Arusha inapambana na miji kama Musoma, Geita, Katoro, nk. Kahama sasa sio level za Arusha tena.

Soon senta kama Kagongwa ama Runzewe zinaipita Arusha.
Hahahahahaah we jamaa kuwa serious.
 
Back
Top Bottom