Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,257
Wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari Lemara pamoja na shule ya msingi Lemara zote za serikali wamenusurika kusombwa na Maji ya mto Themi wakati wakienda shule.
Mwaka jana wanafunzi watatu wa shule ya msingi Lemara waliokolewa baada ya kuzidiwa na maji wakati wakivuka mto huo kwenda shule.
Mto huo unaotenganisha kata ya Sinoni, Themi pamoja na Kata ya Lemara hauna kivuko tangu kivuko cha awali kusombwa na Maji zaidi ya miaka mitano iliyopita.
Msimu wa mvua baadhi ya vijana hujenga kivuko cha muda na kutoza wananchi pamoja na wanafunzi kiasi cha shilingi 200 kuvuka kwenda upande wa pili wa mto.
Kwa maelezo ya wananchi wa maeneo hayo ni kuwa suala hilo la kivuko ni Miaka mingi wanapiga kelele kwa viongozi lakini hakuna mabadiliko yoyote.
Mwaka jana wanafunzi watatu wa shule ya msingi Lemara waliokolewa baada ya kuzidiwa na maji wakati wakivuka mto huo kwenda shule.
Mto huo unaotenganisha kata ya Sinoni, Themi pamoja na Kata ya Lemara hauna kivuko tangu kivuko cha awali kusombwa na Maji zaidi ya miaka mitano iliyopita.
Msimu wa mvua baadhi ya vijana hujenga kivuko cha muda na kutoza wananchi pamoja na wanafunzi kiasi cha shilingi 200 kuvuka kwenda upande wa pili wa mto.
Kwa maelezo ya wananchi wa maeneo hayo ni kuwa suala hilo la kivuko ni Miaka mingi wanapiga kelele kwa viongozi lakini hakuna mabadiliko yoyote.