Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imeahirisha kesi ya Unyang'anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai , Mkoani Kilimanjaro,Lengai Ole Sabaya na wasaidizi wake wawili.
Kesi hiyo ya jinai namba 66/2021 ilikuja mahakamani hapo leo kwa ajili ya kusikilizwa,lakini ilishindwa kuendelea kutokana na shahidi wa upande wa mashtaka kushindwa kufika mahakamani.
Mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo ,Salome Mshasha wakili wa Serikali, Tarcilla Gervas aliiomba mahakama hiyo kuahirisha shauri hilo kutokana na shahidi wao kutofika mahakamani,ambapo hakimu Mshasha aliahirisha shauri hilo hadi Julai 16 mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kusikilizwa huku akisisitiza upande wa mashtaka kuhakikisha wanakamilisha mashahidi wao.
Awali wakili wa utetezi,Mosses Mahuna na Dancan Oolah wakiwakilisha washtakiwa wote watatu wamelalamikia upande wa mashtaka kupoteza muda wakati walishaiambia mahakama hiyo kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika na kuomba Jambo hilo lisijirudie.
Washtakiwa wengine katika shauri hilo ni wasaidizi wa Sabaya,Silvester Nyegu (26) na Daniel Mbura(38) ambapo kwa pamoja wanaokabiliwa na kosa la Unyang'anyi wa kutumia silaha katika duka la mfanyabiashara Saad Mohamed baada ya kumpiga na kumtishia kwa silaha diwani wa kata ya Sombetini Bakari Msangi na Kumpora kiasi Cha shilingi 390,000.
Wakati huo huo kesi namba 27/2021ya uhujumu Uchumi, Utakatishaji fedha haramu,na Rushwa,inayomkabili Sabaya na wenzake saba imeahirishwa kutokana na upelelezi kutokamilika.
Wakili wa Serikali Tarcilla Gervas Mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Salome Mshasha alidai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kesi hiyo kuahirisha Hadi Julai 16 mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kutajwa
Akiongea nje ya mahakama wakili wa Serikali Tarcilla Gervas,alisema kuwa shauri hilo awali lilikuwa na washtakiwa Sita ila June 21mwaka huu,upande wa mashtaka umeongeza washtakiwa wengine wawili na kufikia nane.
Aliwataja washtakiwa hao ni Jackson Macha (24) na Nathan Msuya (31) wote wakati wa Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Wengine ni Enock Togolani Mnkeni {41} Watson Stanley Mwahomange {27} John Odemba Aweyo na Syliverster Nyengu{26} .
Kesi hiyo ya jinai namba 66/2021 ilikuja mahakamani hapo leo kwa ajili ya kusikilizwa,lakini ilishindwa kuendelea kutokana na shahidi wa upande wa mashtaka kushindwa kufika mahakamani.
Mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo ,Salome Mshasha wakili wa Serikali, Tarcilla Gervas aliiomba mahakama hiyo kuahirisha shauri hilo kutokana na shahidi wao kutofika mahakamani,ambapo hakimu Mshasha aliahirisha shauri hilo hadi Julai 16 mwaka huu itakapokuja kwaajili ya kusikilizwa huku akisisitiza upande wa mashtaka kuhakikisha wanakamilisha mashahidi wao.
Awali wakili wa utetezi,Mosses Mahuna na Dancan Oolah wakiwakilisha washtakiwa wote watatu wamelalamikia upande wa mashtaka kupoteza muda wakati walishaiambia mahakama hiyo kwamba upelelezi wa shauri hilo umekamilika na kuomba Jambo hilo lisijirudie.
Washtakiwa wengine katika shauri hilo ni wasaidizi wa Sabaya,Silvester Nyegu (26) na Daniel Mbura(38) ambapo kwa pamoja wanaokabiliwa na kosa la Unyang'anyi wa kutumia silaha katika duka la mfanyabiashara Saad Mohamed baada ya kumpiga na kumtishia kwa silaha diwani wa kata ya Sombetini Bakari Msangi na Kumpora kiasi Cha shilingi 390,000.
Wakati huo huo kesi namba 27/2021ya uhujumu Uchumi, Utakatishaji fedha haramu,na Rushwa,inayomkabili Sabaya na wenzake saba imeahirishwa kutokana na upelelezi kutokamilika.
Wakili wa Serikali Tarcilla Gervas Mbele ya Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Salome Mshasha alidai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kesi hiyo kuahirisha Hadi Julai 16 mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya kutajwa
Akiongea nje ya mahakama wakili wa Serikali Tarcilla Gervas,alisema kuwa shauri hilo awali lilikuwa na washtakiwa Sita ila June 21mwaka huu,upande wa mashtaka umeongeza washtakiwa wengine wawili na kufikia nane.
Aliwataja washtakiwa hao ni Jackson Macha (24) na Nathan Msuya (31) wote wakati wa Moshi Mkoani Kilimanjaro.
Wengine ni Enock Togolani Mnkeni {41} Watson Stanley Mwahomange {27} John Odemba Aweyo na Syliverster Nyengu{26} .