Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Askari polisi katika kituo kidogo Cha polisi Mbughuni wilayani Arumeru, Mkoani hapa, ameuawa kwa kukatwa na panga kichwani wakati akijaribu kumkamata mtuhumiwa.wa wizi.
Tukio hilo limetokea Jana majira ya saa tano usiku katika Kijiji Cha Makiba wakati Askari huyo( jina linahifadhiwa) alipoenda nyumbani kwa mhalifu kwa lengo la kumkamata.
Kwa mujibu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP-Justine Masejo askari huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuvunja damu nyingi.
"Askari wetu katika kituo kidogo cha polisi Mbughuni alikatwa panga kichwani na kufariki dunia baada ya kwenda nyumbani kwa mhalifu majira ya saa tano usiku lengo la kumkamata, hivi Sasa polisi wanaoendesha operesheni ya kumsaka ili afikishwe kwenye vyombo vya dola"alisema Masejo
Kamanda alifafanua kwamba askari huyo alienda Nyumbani kwa mtuhumiwa kwa nia ya kumkamata kuhusiana na matukio ya wizi wa mazao na kwamba wakati akijaribu kumkamata ndipo alipotokea mhalifu mwingine Nyumba ya jirani ambaye alimkata panga moja kichwani askari huyo nakupoteza Maisha.
Aidha Masejo aliongeza kuwa kabla ya tukio hilo mwananchi mmoja alifika katika kituo cha polisi Mbughuni kulalamika.juu ya mtuhumiwa wa wizi wa mazao yake ambapo polisi walianza msako wa kumvizia mtuhumiwa huyo.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa uchunguzi, aliweza kufanikiwa kutoroka baada ya tukio hilo na polisi wameanzisha msako Mkali dhidi ya Watuhumiwa hao .
Ends
Tukio hilo limetokea Jana majira ya saa tano usiku katika Kijiji Cha Makiba wakati Askari huyo( jina linahifadhiwa) alipoenda nyumbani kwa mhalifu kwa lengo la kumkamata.
Kwa mujibu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamishina msaidizi wa Polisi ACP-Justine Masejo askari huyo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuvunja damu nyingi.
"Askari wetu katika kituo kidogo cha polisi Mbughuni alikatwa panga kichwani na kufariki dunia baada ya kwenda nyumbani kwa mhalifu majira ya saa tano usiku lengo la kumkamata, hivi Sasa polisi wanaoendesha operesheni ya kumsaka ili afikishwe kwenye vyombo vya dola"alisema Masejo
Kamanda alifafanua kwamba askari huyo alienda Nyumbani kwa mtuhumiwa kwa nia ya kumkamata kuhusiana na matukio ya wizi wa mazao na kwamba wakati akijaribu kumkamata ndipo alipotokea mhalifu mwingine Nyumba ya jirani ambaye alimkata panga moja kichwani askari huyo nakupoteza Maisha.
Aidha Masejo aliongeza kuwa kabla ya tukio hilo mwananchi mmoja alifika katika kituo cha polisi Mbughuni kulalamika.juu ya mtuhumiwa wa wizi wa mazao yake ambapo polisi walianza msako wa kumvizia mtuhumiwa huyo.
Alisema kuwa mtuhumiwa huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa uchunguzi, aliweza kufanikiwa kutoroka baada ya tukio hilo na polisi wameanzisha msako Mkali dhidi ya Watuhumiwa hao .
Ends