Nyangomboli
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 3,501
- 1,955
Nduguzanguni, nilikuwa na kiziara uchwala huko HANDENI, SIMANJIRO, SAME , MWANGA pia KARATU. Kwa kweli nimeshangaa sana kuona huko mgao haupo na kama kuna tatizo la umeme basi ni la kawaida tu na si kama hapa kwetu ARUSHA. Swali langu ni kwa wenzangu wenye uelewa mpana kidogo juu ya mambo haya ni kwamba, umeme tunaotumia hapa ARUSHA ni chanzo tofauti na sehemu nilizozitaja? Hapa kwangu naona tangu kumi na mbili upo ila ni mdogo sana na hata sioni vizuri. Tatizo laweza kuwa nini jamani? MSAADA NAHITAJI NDUGU YENU ILI NIELEWE.