Arusha na Musoma nao wazomea Mawaziri,mwendomdundo.

BroJay4

JF-Expert Member
Aug 27, 2007
236
16
Ziara za mawaziri mikoani balaa

2007-10-08 09:27:14
Na Waandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Henry Daffa Shekifu, amelazimika kuingilia kati na kuwasihi wananchi wa wilaya ya Hanang wasimzomee Waziri wa Mipango Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa, anaripoti Zillipa Joseph wa PST kutoka Hanang.

Bw. Shekifu aliwataka wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya soko mjini Katesh kutoa nafasi kwa viongozi kujieleza badala ya kuzomea.

Hali hiyo ilijitokeza baada ya Dk. Ngasongwa kujibu maswali ya baadhi ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.

`Tufautishe mikutano. Mkutano huu sio wa kampeni ni wa serikali, tutoe nafasi kwa viongozi, tusitunishiane misuli tukapoteza amani, na amani ikivunjika kuirudisha ni kazi. Kama kuna mwananchi anataka kubadilisha mkutano huu uwe wa kampeni nitamdhibiti kwa nguvu za serikali,` alionya Bw. Shekifu.

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi hao ni kutaka kufahamu ni kwa sababu� gani serikali inawasambaza mawaziri na manaibu wao mikoani kuelezea bajeti, na kudai kuwa huo ni ubadhirifu wa fedha za walipa kodi, wakati wananchi wanataabika na bei za bidhaa kupanda.

Swali lingine lilihoji uhalali wa kumsimamisha mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe, kuhudhuria vikao vya Bunge huku wananchi hao wakidai kuwa ziara hiyo ni sehemu ya kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Akijibu maswali hayo, Dk. Ngasongwa alisema Bw. Zitto, anajitafutia umaarufu na kuongeza kuwa alitoa lugha ya matusi bungeni ndio sababu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao.

`Wabunge wenyewe ndio waliomhukumu kwa sababu alikiuka utaratibu,` alisema.

Kuhusu mfumuko wa bei,� alisema hali hiyo inasababishwa na majanga ambayo Tanzania iliyopata kama ukame na mafuriko.

Alisema hali hiyo iliilazimu serikali kutenga fedha za dharura kutumika na kuifanya nchi katika hali ngumu.

Kuhusu mawaziri kufanya ziara kuelezea bajeti, alisema inawalazimu kufanya hivyo ili kujibu shutuma zinazotolewa na vyama vya upinzani kuhusu bajeti hiyo.

Aliongeza kuwa serikali haitumii fedha vibaya bali wapinzani ndio wanatumia kodi za wananchi kwa kukodi helikopta na kufafanua kuwa vyama vya upinzani vyenye wabunge vinapata ruzuku kutoka serikalini.

`Kati ya mimi niliyefika hapa kwa gari na hao wanaokuja kwa helikopta nani mfujaji?` aliuliza Dk. Ngasongwa.

Mara baada ya kusema hivyo, wananchi hao walilipuka na kukataa majibu hayo huku wengine wakianza kuzomea hali iliyomfanya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, kushika kipaza sauti na kuanza kuongea na wananchi na kusema anasikitishwa na tabia hiyo ya aibu ya kutomheshimu kiongozi mkubwa kama huyo.

Awali akihutubia wananchi hao, Dk. Ngasongwa alisema serikali imetenga shilingi trilioni sita na kutaja vipaumbele vya utekelezaji wa bajeti hiyo kuwa ni kuboresha sekta za elimu, miundombinu, afya, kilimo na maji ili kumwezesha mwananchi kujiinua kiuchumi.

Alisema katika sekta ya elimu wametenga Sh. trilioni moja, miundombinu bilioni 777, afya bilioni 590, kilimo bilioni 379 na maji 309.

Aidha waziri huyo aliwataka wananchi kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao shuleni kwa kushirikiana na walimu ili kupata wanafunzi wa vyuo vikuu miaka ijayo.

Katika ziara hiyo Dk. Ngasongwa anatembelea wilaya za Mbulu, Hanang, Babati Mjini na Babati Vijijini.

Wakati huo huo, Bigambo Jeje wa PST anaripoti kutoka Musoma kuwa Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Deodatus Kamala, mwishoni mwa wiki alipata wakati mgumu baada ya kuzomewa na wananchi katika mkutano wa hadhara na kulazimika kulikimbia jukwaa.

Alikumbana na mkasa huo katika mkutano uliofanyika katika kata ya Nyasho Manispaa ya Musoma mkoani Mara na baada ya kuona anazidi kuzomewa aliteremka haraka jukwaani na kuondoka.

Dk. Kamala alianza kuzomewa na wananchi hao baada ya kutetea tuhuma zilizoelekezwa kwa Waziri wa Miundombinu Bw. Andrew Chenge na viongozi wengine waliotajwa kuhusika katika kashfa ya ufisadi iliyotolewa siku za hivi karibuni na kambi ya vyama vya upinzani.

Wananchi hao waliamua kumzomea Naibu waziri huyo mara tu alipoanza kumtetea waziri mwenzake huku akibeza kauli za kambi ya upinzani kuhusiana na kashfa ya rushwa.

Dk. Kamala alisema tuhuma dhidi ya vigogo hao akiwemo Waziri Chenge hazina msingi kwa kuwa wapinzani hawana ushahidi wowote.

Alisema serikali ya CCM itaendelea kutawala tu hata kama wapinzani watazidi kuwashambulia viongozi wa serikali.

Alisema wamechaguliwa na wananchi kwa zaidi ya asilimia 80 huku akiwabeza wapinzani kwamba kama na wao wanataka kutawala basi waombe ridhaa kutoka kwa wananchi.

`Tutaendelea tu kutawala hata kama wapinzani watazidi kutushambulia na kutupaka matope, ukiona wapinzani wanatusifu mjue kuwa CCM na serikali yake inaelekea kubaya lakini mkiona wanatupaka matope ni dalili ya kwamba kazi yetu kwa wananchi ni nzuri,` alisema licha ya mayowe ya kuzomea ya muda wote kutoka kwa wananchi.

Hali ya kuzomeazomea ilizimwa na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya (CCM) Taifa, Bw. Vedastus Mathayo, ambaye pia ni Mbunge wa Musoma mjini.

Aliposimama alijibu baadhi ya maswali yaliyokuwa yameulizwa na wananchi katika mkutano huo, majibu ambayo yalionekana dhahiri kuwaridhisha na hivyo kushusha jazba waliyokuwa nayo hapo awali.

Kwa upande wake, Waziri wa Miundo mbinu, Bw. Andrew Chenge alisema hawezi kujibu tuhuma hizo kwa kuwa hata kama atajieleza vipi wananchi hawawezi kuridhika na majibu yake.

Alisema angependa kuongelea mambo mengine ya maendeleo kuliko kuchukua muda mwingi kujibu tuhuma kama hizo.

Wakati huo huo, Wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Geita, mkoani Mwanza wameeleza chanzo cha mbunge wa jimbo la Geita, Bw. Ernest Mabina kuzomezwa mbele ya Waziri Mkuu hivi karibuni kuwa ni mbunge huyo kutowajibika kwa wapiga kura wake.

Baadhi ya wazee hao walidai kuwa walitaka kumkabidhi mbunge huyo kwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa, aondoke naye siku hiyo kwa madai kuwa yeye ni mbunge wa Dar es Salaam na siyo Geita anaandika Renatus Masuguliko wa PST, Geita�.

Walisema mbunge huyo haonekani jimboni mpaka wakati wa ziara za viongozi.

Walisema wapiga kura wake wamekuwa kama yatima kwa sababu tangu achaguliwe hajakutana nao.

Tuhuma hizo zilitolewa na baadhi ya wazee wa CCM katika kikao chao kilichofanyika kwenye jengo la CCM wilayani siku ya Jumatano wiki hii.

Kikao hicho kiliwashirikisha wazee zaidi 70 wakiwemo viongozi wa mashina.

Kikao hicho�kiliitishwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita, Bw. John Chenge Luhemeja kwa lengo la kutafuta kiini cha kuzomewa kwa mbunge wa Geita mbele ya Waziri Lowassa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapa mwezi uliopita.

Habari zaidi kutoka ndani ya kikao hicho, zimedai kuwa baadhi ya wazee walidai mbunge huyo anawabagua wanachama wakiwemo wazee na vijana katika makundi na wengine kuonekana bora na kwamba bila wao hakuna CCM.

`Tunashangaa baadhi ya wazee wamekuwa wakibaguliwa na wengine wachache kupewa kipaumbele�kwa maslahi binafsi,�bila kujali matokeo yake na wengi wetu tumekuwa tunabaguliwa kutokana na kuwa na msimamo wa kusema ukweli,` alidai mzee Michael Makongoro.

Mwezi uliopita mamia ya wananchi walimzomea mbunge huyo, Mabina, mbele ya Waziri Lowassa pale alipotambulishwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,� Bi. Margaret Sitta, kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Bw. Lowassa.

Jitihada za kumpata Bw. Mabina kuzungumzia suala hilo hazikuzaa matunda kwa kuwa simu yake ya kiganjani ilikuwa imezimwa.

* SOURCE: Nipashe
 
`Tufautishe mikutano. Mkutano huu sio wa kampeni ni wa serikali, tutoe nafasi kwa viongozi, tusitunishiane misuli tukapoteza amani, na amani ikivunjika kuirudisha ni kazi. Kama kuna mwananchi anataka kubadilisha mkutano huu uwe wa kampeni nitamdhibiti kwa nguvu za serikali,` alionya Bw. Shekifu.

Wao ndo wanao jichanganya kama mkutano wa serkali iweje wavalie jezi za kijani? Ama siku hizi serikali nayo ina jezi?

Wanapata wanacho kistahili, mahali pengine nasikia wamefanya mikutano ya ndani badala ya hadhara baada ya kuona soo litakuwa kubwa!

Huyu mkuu wa Mkoa aache kutisha watu..awaache wajieleze eti dola itawashughulikia?? asubiri naye siku zake zahesabika!

Amani gani hiyo anayo ona wataipoteza ya kulala njaa na kukosa hela ya asprin?
Namshauri akasome alama za nyakati.. enzi za chama kushika hatam zilisha zikwa.. tunakaribia kumalizia matanga kwa kukizika chama chenyewe kwani kimezidi kuwa na mawazo mgando.. kazi kulindana na kugawiana wao peke yao vilivyo vyetu wote!...... mpaka kieleweke!
 
Ufisadi: Ni mshike mshike tu

2007-10-08 17:28:09
Na Mwandishi wetu, Jijini

Lile sakata la kuibuliwa kwa tuhuma za ufisadi kwa baadhi ya vigogo nchini limeendelea kuzua mshike mshike wa aina yake baada ya wananchi wenye hasira kumtoa baru jukwaani Naibu Waziri mmoja.

Taarifa zinamtaja Naibu Waziri aliyekumbwa na balaa hilo la kushushwa jukwaani kutokana na kelele za jazba toka kwa wananchi kuwa ni Dk. Deodatus Kamala wa Wizara ya Afrika Mashariki na Kati.

Taarifa zinasema Dk. Kamala amekumbwa na kisanga hicho wakati akijaribu kutoa ufafanuzi kwa wananchi kuhusiana na swali lililoulizwa na mwananchi mmoja kuhusu tuhuma za ufisadi ambazo wapinzani wamekuwa wakizishikia bango kwa siku kadhaa sasa.

Mashuhuda wa tukio hilo wanasema lenyewe lilijiri pale katika stendi ndogo ya mabasi ya Nyasho mjini Musoma.

Inaelezwa kuwa Dk. Kamala alilazimika kutimka jukwaani kutokana na zomea zomea iliyoibuka kwa kasi baada ya kutoa majibu yaliyoonekana kutowaridhisha wananchi.

Inaelezwa kuwa balaa lilianza wakati mwananchi mmoja aliposimama na kuuliza kuhusu sababu za msafara wa mawaziri hao kuongozwa na Waziri wa Miundombinu.

Bw. Andrew Chenge, ambaye ni miongoni mwa wanatuhumiwa na wapinzani juu ya ushiriki wake katika ufisadi
Inaelezwa kuwa baada ya hapo, ndipo akainuka Dk. Kamala kutaka kujibu swali hilo.

``Tuhuma za ufisadi zilizotolewa na wapinzani dhidi ya viongozi hazina msingi kwa kuwa hao waliozitoa hawana ushahidi wowote,`` alisema Dk. Kamala.

Hata hivyo badala ya wananchi kumsikiliza, walianza kumzomea.
Inaelezwa zaidi kuwa licha ya kuzomewa, Dk. Kamala aliendelea kusema kuwa Serikali ya CCM itaendelea kutawala tu hata kama wapinzani watazidi kuwashambulia viongozi wa Serikali.

Akasema wakiona wapinzani wanawasifu wajue kuwa CCM inaelekea kubaya na wakiona wanawapaka matope ni dalili ya kwamba kazi yao kwa wananchi ni nzuri.

Kauli hiyo iliwafanya wananchi wazidi kupiga mayowe na kuzomea kwa nguvu, hali iliyomfanya Dk. Kamala ashuke jukwaani haraka haraka na kumpisha Mbunge wa Musoma Mjini Bw. Vedasus Mathayo aliyekuja kuwatuliza wananchi hao.

Aidha, mshike mshike mwingine umedaiwa kutokea mkoani Manyara baada ya Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwekezaji, Dk. Juma Ngasongwa, kujikuta kwenye wakati mgumu wakati alipotupiwa swali mwananchi mmoja kuhusu sababu za kusimamishwa kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe.

Inaelezwa kuwa wakati Dk. Ngasongwa akijaribu kutoa ufafanuzi kuhusu suala hilo, wananchi wakamchenjia na kuanza kumsomea vikali.

* Source Alasiri.
 
kwanini hawawaachii wabunge kuelezea uzuri bajeti hiyo? wabunge si waliunga mkono bajeti?
 
labda tatizo kuwa wanajaribu kuelezea "Kasungura ka Lowassa" lakini wananchi wanataka maelezo ya ng'ombe "wao"....
 
nimesoma mapesa ni mengi sana lakini sisi wa hanang zetu ni kiasi gani? naomba kuuliza mweshimiwa waziri
 
Binafsi nitawaunga mkono watanzania wanaozomea hao viongozi mchwara na wala rushwa! Na nadhani hiyo ndo dawa iliyobakia kwani wanatakiwa wafahamu kuwa wanachi tumechoka na tumeamua kusema sasa basi!!
 
Kitumbua chake kiko mashakani atakwenda wapi zaidi ya kwenda kupiga porojo ofisini kwake bila kufanya kazi yoyote. Hawa watu mafedhuli tu hawawezi kuona hata aibu lakini siku yao yaja tena haraka sana vile anbavyo hawakutegemea.
 
"Kweli siku ya Kufa Nyani miti yote huteleza, na sikio la kufa halisikii dawa" Wahenga walisema.

Mwalimu J.K Nyerere kwenye kitabu chake alichoakiandika baada ya kung'atuka cha " Uongozi na Hatima Ya Tanzania" alisema mambo makubwa sana kuhusu uongozi wa nchi hii chini ya Chama cha mapinduzi, mimi nitaongelea moja tu hapa, alisema kwamba CCM in "Cancer ya Kiongozi" hayo ni Maneno ya Baba wa taifa mwenye Kadi namba moja ya CCM. Na Mlolongo wa viongozi waandamizi wa serikali mawaziri kuzomewa na wananchi inadhirisha kwamba ile "Cancer" ambayo mwalimu aliisema imeanza kuimaliza serikali ya chama cha mapinduzi. Na mwalimu alionya kwamba kama hiyo "Cancer" haitatibiwa itaiua CCM pamoja na serikali yake na hicho ndo kinachotokea sasa. Kwakuwa viongozi wa CCM wamekuwa wakimuenzi baba wa taifa kwa maneno tu matupu, na kunukuu baadhi ya maneno ya mwalimu kwa manufaa yao binafsi huo usanii wao ndo umewafikisha hapo walipo na wasiwalaumu wapinzani, kwani wanachokifanya ni wajibu wao kwa jamii ya watanzania na tunawapongeza sana kwa kazi nzuri.

Kuzomewa kwa viongozi hawa ni ishara kwamba wananchi wa Tanzania wamezinduka na sasa wako tayari kupigania maslahi ya nchi yao, kama ilivyokuwa kwa Tanganyika ilivyozinduka dhidi ya hujuma za mkoloni vivyo hivyo watanzania wamezinduka dhidi ya hujuma za CCM na viongozi wake.

CCM wanaogopa vivuli vyao wenyewe kwanini wasiwaache waliounga mkono bajeti kwenda kuwaelezea wale wanawawakilisha uzuri wa kile walichokiunga mkono.

"Revolutionary Ideas Never Die"
 
Atathubutu kujitokeza hadharani! Habari nilizonazo ni kwamba Kala-magi sasa hivi ni houseboy huko ikulu anasaidia kazi za nyumbani za JK. Unafikiri atalipa vipi fadhila za kukingiwa kifua kiasi hicho.
 
"Kweli siku ya Kuanguka Nyani miti yote huteleza, na sikio la kufa halisikii dawa" Wahenga walisema.

Mwalimu J.K Nyerere kwenye kitabu chake alichoakiandika baada ya kung'atuka cha " Uongozi na Hatima Ya Tanzania" alisema mambo makubwa sana kuhusu uongozi wa nchi hii chini ya Chama cha mapinduzi, mimi nitaongelea moja tu hapa, alisema kwamba CCM in "Cancer ya Kiongozi" hayo ni Maneno ya Baba wa taifa mwenye Kadi namba moja ya CCM. Na Mlolongo wa viongozi waandamizi wa serikali mawaziri kuzomewa na wananchi inadhirisha kwamba ile "Cancer" ambayo mwalimu aliisema imeanza kuimaliza serikali ya chama cha mapinduzi. Na mwalimu alionya kwamba kama hiyo "Cancer" haitatibiwa itaiua CCM pamoja na serikali yake na hicho ndo kinachotokea sasa. Kwakuwa viongozi wa CCM wamekuwa wakimuenzi baba wa taifa kwa maneno tu matupu, na kunukuu baadhi ya maneno ya mwalimu kwa manufaa yao binafsi huo usanii wao ndo umewafikisha hapo walipo na wasiwalaumu wapinzani, kwani wanachokifanya ni wajibu wao kwa jamii ya watanzania na tunawapongeza sana kwa kazi nzuri.

Kuzomewa kwa viongozi hawa ni ishara kwamba wananchi wa Tanzania wamezinduka na sasa wako tayari kupigania maslahi ya nchi yao, kama ilivyokuwa kwa Tanganyika ilivyozinduka dhidi ya hujuma za mkoloni vivyo hivyo watanzania wamezinduka dhidi ya hujuma za CCM na viongozi wake.

CCM wanaogopa vivuli vyao wenyewe kwanini wasiwaache waliounga mkono bajeti kwenda kuwaelezea wale wanawawakilisha uzuri wa kile walichokiunga mkono.

"Revolutionary Ideas Never Die"
 
Najiuliza.....

Hivi ni nani alitoa wazo hili la kuwapeleka hawa waheshimiwa sana kujianika? Hivi huu ni mwendelezo wa ule mkakati TUCHAFUKE SOTE ama? Unapowatuma watu na heshima zao kutetea UFISADI na kuimba nyimbo za maendeleo kwa watanzania wenye hasira na machungu ya maisha ni kuwa unawatega wananchi ama?

Kwa kweli nashindwa kung'amua mantiki ya hili labda walio karibu wanielimishe..

Halafu hii ni ziara ya kiserekali ama kichama....

Mbona naona ukada mwingi tu ama ndio masuala ya kuwasilimisha waumini wa UCCM badala ya kutafuta waumini wapya....

Naanza kuamini maneno ya jamaa yangu mmoja kuwa uroda wa madaraka umeharibu uwezo wa kufikiri wa waladau wetu. Yaani hata wale niliokuwa nawaamini katika uwezo wao wa kufikiri wameingia katika mkondo huu wa kuzima moto kwa kutumia petroli...
 
Ziara za mawaziri mikoani balaa

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi hao ni kutaka kufahamu ni kwa sababu� gani serikali inawasambaza mawaziri na manaibu wao mikoani kuelezea bajeti, na kudai kuwa huo ni ubadhirifu wa fedha za walipa kodi, wakati wananchi wanataabika na bei za bidhaa kupanda.

Swali lingine lilihoji uhalali wa kumsimamisha mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe, kuhudhuria vikao vya Bunge huku wananchi hao wakidai kuwa ziara hiyo ni sehemu ya kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Akijibu maswali hayo, Dk. Ngasongwa alisema Bw. Zitto, anajitafutia umaarufu na kuongeza kuwa alitoa lugha ya matusi bungeni ndio sababu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao.

`Wabunge wenyewe ndio waliomhukumu kwa sababu alikiuka utaratibu,` alisema.

Kuhusu mfumuko wa bei,� alisema hali hiyo inasababishwa na majanga ambayo Tanzania iliyopata kama ukame na mafuriko.

nilikuwa naangalia bunge wakati wanamsulubisha zitto na kumwacha huru barnaba Kaa-la-maji. Ni kwamba hata sura zao wakati wanatoa hoja walikuwa wanaona haya na vilevile walilazimishia kwamba dogo Zitto ametukana na wakaanza kutusingizia sisi vijana kwamba hatuna staha na tunapaswa kujifunza.

kuhusu majanga ni kwamba sio kisingizio cha kupandisha kodi na kufumuka kwa bei. hii yote inatokana na kutojali kwa serikali na kukosa ubunifu kwa watendaji wake hasa wataalam wa bajeti na mipango.

serikali inaabishwa leo na wajue kuwa wananchi ndio wenye nchi na inapaswa kujifunza na kujirudi au la maumivu yatazidi. Hizi ndondondo za kuzomewa zitajaa na hatimaye siku moja waziri atatolewa mkuku jukwaani na sijui itakuwaje....

Am proud to be JF member
 
Atathubutu kujitokeza hadharani! Habari nilizonazo ni kwamba Kala-magi sasa hivi ni houseboy huko ikulu anasaidia kazi za nyumbani za JK. Unafikiri atalipa vipi fadhila za kukingiwa kifua kiasi hicho.

Tunapofika mahala mfumo unaruhusu mtu mmoja tena kawaziri kasichokuwa na hata mizizi ya kisiasa kuwa zaidi ya maslahi ya dola (serikali) kwa kweli ni hali mbaya mno.

JK tusaidie "waumini" wako....WATOSE HAWA MANYANG'AU SASA. Kuendelea na uozo huu hata kwa siku moja ni kutiana majaribuni na uzalendo wetu kwako na kwa taifa letu. Wewe ni kiongozi ambaye mwenye kadi ya mwisho kuinusuru Tanzania yetu huko inapoelekea. Uchaguzi ndani ya CCM hauwezi kuwa sababu ya kushindwa kutuondolea haya machungu ya kuona hawa manyang'au wanaendelea kutu-enjoy zaidi. Tafadhali kaka chonde ndugu yangu na hizi temptations unazotupa. Pleaseeeeeeeeee kaka tumesubiri vya kutosha tusipelekane kubaya...

Tanzanianjema
 
Napendekeza thread hii ibadilishwe jina na kuitwa:
MAWAZIRI WETU NA ZIARA YA KUTETEA TUHUMA ZA UFISADI
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom