ARUSHA; MAHAKAMA yamwachia huru Mshitakiwa wa uhujumu uchumi Lucas Mdeme

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
Mahakama ya wilaya ya Mkoa wa Arusha imemwachia huru mfanyabiashara Maarufu wa madini ya Tanzanite jiiini Arusha Lucas Mdeme(46) na mwenzake Nelson Lyimo(58) waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka sita likiwemo la uhujumu uchumi baada ya upande wa mashtaka kudai haina Nia ya kuendelea nao katika shauri hilo.

Mdeme na Lyimo walikuwa ni miongoni mwa washtakiwa nane wakiwemo Askari Polisi watatu katika kesi ya uhujumu uchumi ,utakatishaji fedha haramu na kupanga njama za kujipatia rushwa ya fedha ya awali shilingi milioni 10 kati ya milioni 30 walizohitaji kutoka kwa Mfanyabiashara maarufu Jijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wauzaji Madini Wakubwa ndani ya nchi na nje {TAMIDA} Sammy Mollel.

Waendesha mashtaka wa serikali Adelaide Kassalay na Agnes Hyera walimweleza Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Arusha,Rose Ngoka kwamba upande wa jamhuri haina nia ya kuendelea nao katika shauri hilo na hivyo wanaiomba mahakama iweze kuwaachia huru bila masharti yoyote.

‘’Mheshimiwa Hakimu upande wa jamhuri hatuna Nia ya kuendelea na mshtakiwa namba sita na Saba katika shauri hilo hivyo tunaiomba mahakama iwaachie huru bila masharti yoyote’’alisema Kassalay.

Kufuatia maelezo hayo Hakimu Ngoka aliamuru kuachiwa kwa mshtakiwa namba Saba ,Lucas Mdeme na mshtakiwa namba sita Nelson Lyimo na alihairisha kesi hiyo hadi mai 4 mwaka huu kwa washtakiwa wengine waliobakia wakiwemo Askari Polisi.

Askari waliopandishwa kizimbani baada ya kufukuzwa kazi ni pamoja na askari mwenye namba G. 5134 DC Heavenlight Mushi aliyekuwa Askari kitengo Cha Intelijensia Mkoa wa Kipolisi Kinondoni jijini Dar es Salaam,H.125 PC Gasper Paul kitengo Cha Intelijensia Makao Makuu Dodoma na H.1021 PC Bryton Murumbe aliyekuwa Askari wa kawaida Mkoani Dodoma.

Wengine wanaoshikiliwa mahabusu katika kesi hiyo ni pamoja na Joseph Chacha{43} maarufu kwa jina la ‘’baba Ngodo’’ mkazi wa Ilboru, Leonila Joseph{46} mkazi wa Ilboru, na Omary Alphonce{43} maarufu kwa jina la Matelephone mkazi wa Olasiva Jijini Arusha.

Ends...
 
Mahakama ya wilaya ya Mkoa wa Arusha imemwachia huru mfanyabiashara Maarufu wa madini ya Tanzanite jiiini Arusha Lucas Mdeme(46) na mwenzake Nelson Lyimo(58) waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka sita likiwemo la uhujumu uchumi baada ya upande wa mashtaka kudai haina Nia ya kuendelea nao katika shauri hilo.


Mdeme na Lyimo walikuwa ni miongoni mwa washtakiwa nane wakiwemo Askari Polisi watatu katika kesi ya uhujumu uchumi ,utakatishaji fedha haramu na kupanga njama za kujipatia rushwa ya fedha ya awali shilingi milioni 10 kati ya milioni 30 walizohitaji kutoka kwa Mfanyabiashara maarufu Jijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wauzaji Madini Wakubwa ndani ya nchi na nje {TAMIDA} Sammy Mollel.





Waendesha mashtaka wa serikali Adelaide Kassalay na Agnes Hyera walimweleza Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Arusha,Rose Ngoka kwamba upande wa jamhuri haina nia ya kuendelea nao katika shauri hilo na hivyo wanaiomba mahakama iweze kuwaachia huru bila masharti yoyote.





‘’Mheshimiwa Hakimu upande wa jamhuri hatuna Nia ya kuendelea na mshtakiwa namba sita na Saba katika shauri hilo hivyo tunaiomba mahakama iwaachie huru bila masharti yoyote’’alisema Kassalay



Kufuatia maelezo hayo Hakimu Ngoka aliamuru kuachiwa kwa mshtakiwa namba Saba ,Lucas Mdeme na mshtakiwa namba sita Nelson Lyimo na alihairisha kesi hiyo hadi mai 4 mwaka huu kwa washtakiwa wengine waliobakia wakiwemo Askari Polisi.






Askari waliopandishwa kizimbani baada ya kufukuzwa kazi ni pamoja na askari mwenye namba G. 5134 DC Heavenlight Mushi aliyekuwa Askari kitengo Cha Intelijensia Mkoa wa Kipolisi Kinondoni jijini Dar es Salaam,H.125 PC Gasper Paul kitengo Cha Intelijensia Makao Makuu Dodoma na H.1021 PC Bryton Murumbe aliyekuwa Askari wa kawaida Mkoani Dodoma.







Wengine wanaoshikiliwa mahabusu katika kesi hiyo ni pamoja na Joseph Chacha{43} maarufu kwa jina la ‘’baba Ngodo’’ mkazi wa Ilboru,Leonila Joseph{46} mkazi wa Ilboru, na Omary Alphonce{43} maarufu kwa jina la Matelephone mkazi wa Olasiva Jijini Arusha.



Ends...
Hii nchi yaani hiyo sheria ya uhujumu uchumi ilianzishwa kwa malengo gani haswaa?
 
Hii nchi yaani hiyo sheria ya uhujumu uchumi ilianzishwa kwa malengo gani haswaa?
Ilikuwa maalum kwa kubambikia watu kesi na kuwakomoa.
Hawa wapinzani wa jiwe. Ukishawekwa ndani no dhamana. Sheria kandamizi kabisa hii
 
Kila anayewachiwa huru siyo awe amehonga.

Kuna kesi zingine hakimu anaona kabisa kuwa huu ni usaniii tu.
Jamaa kapiga sana hizo issue kawauza sana wafanyabiashara wa tanzanite n kuchomolewa pesa,kuna naowajua 4 wote walipigwa n huyo luca
 
Hii nchi inahitaji sana Katiba Mpya ituweke huru, badala ya kuendelea kutegemea hisani ya mtawala, bado tupo utumwani.
Sio kila changamoto kwenye jamii inahitaji suluhisho la kikatiba.
 
Mahakama ya wilaya ya Mkoa wa Arusha imemwachia huru mfanyabiashara Maarufu wa madini ya Tanzanite jiiini Arusha Lucas Mdeme(46) na mwenzake Nelson Lyimo(58) waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka sita likiwemo la uhujumu uchumi baada ya upande wa mashtaka kudai haina Nia ya kuendelea nao katika shauri hilo.


Mdeme na Lyimo walikuwa ni miongoni mwa washtakiwa nane wakiwemo Askari Polisi watatu katika kesi ya uhujumu uchumi ,utakatishaji fedha haramu na kupanga njama za kujipatia rushwa ya fedha ya awali shilingi milioni 10 kati ya milioni 30 walizohitaji kutoka kwa Mfanyabiashara maarufu Jijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wauzaji Madini Wakubwa ndani ya nchi na nje {TAMIDA} Sammy Mollel.





Waendesha mashtaka wa serikali Adelaide Kassalay na Agnes Hyera walimweleza Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Arusha,Rose Ngoka kwamba upande wa jamhuri haina nia ya kuendelea nao katika shauri hilo na hivyo wanaiomba mahakama iweze kuwaachia huru bila masharti yoyote.





‘’Mheshimiwa Hakimu upande wa jamhuri hatuna Nia ya kuendelea na mshtakiwa namba sita na Saba katika shauri hilo hivyo tunaiomba mahakama iwaachie huru bila masharti yoyote’’alisema Kassalay



Kufuatia maelezo hayo Hakimu Ngoka aliamuru kuachiwa kwa mshtakiwa namba Saba ,Lucas Mdeme na mshtakiwa namba sita Nelson Lyimo na alihairisha kesi hiyo hadi mai 4 mwaka huu kwa washtakiwa wengine waliobakia wakiwemo Askari Polisi.






Askari waliopandishwa kizimbani baada ya kufukuzwa kazi ni pamoja na askari mwenye namba G. 5134 DC Heavenlight Mushi aliyekuwa Askari kitengo Cha Intelijensia Mkoa wa Kipolisi Kinondoni jijini Dar es Salaam,H.125 PC Gasper Paul kitengo Cha Intelijensia Makao Makuu Dodoma na H.1021 PC Bryton Murumbe aliyekuwa Askari wa kawaida Mkoani Dodoma.







Wengine wanaoshikiliwa mahabusu katika kesi hiyo ni pamoja na Joseph Chacha{43} maarufu kwa jina la ‘’baba Ngodo’’ mkazi wa Ilboru,Leonila Joseph{46} mkazi wa Ilboru, na Omary Alphonce{43} maarufu kwa jina la Matelephone mkazi wa Olasiva Jijini Arusha.



Ends...

Kusimamishwa kwa maelekezo kutoka juu na Mungu mwenyewe muweza yote, tutaendelea kudhihirika kwa vitendo katika mahakama zote ambazo kwa hakika ule mhimili uliojichimbia zaidi ulikuwa umezisonga mno.

Masheikh wa uamusho, Rugemalila, mwana wa Chadema Mbeya na wote mliokuwa mkisumbuliwa na yule msukuma - yamekwisha!

Ni suala la muda tu sasa.

Hiiiiii bagosha!
 
Hii sheria ya uhujumu uchumi ni ya kiuonevu sana Magufuli ameitumia sana kukomelea watu.

Vyesi vyote vinafaa viwe na dhamana kwani unapokamatwa inakuwa ni tuhuma tu sasa wanaposema uhujumu uchumi mbona tayari wameshakuhukumu hata kabla ya kesi??

Hii katiba ya akina Nyerere ni ya kiimla sana na inanyanyasa mno watu kwani inampa fursa rais aliyeko madarakani kukomoa wale anawaona kama maadui zake. Bure kabisa hii katiba.
 
Hii sheria kwa awamu iliyoisha ilikuwa maalum hasa kwa kaskazini; Lugumi aliwekwa mahabusu ipi
 
Back
Top Bottom