Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imempokonya mfanyabiashara maarufu jijini Arusha Philemon Mollel(Monaban) ,eneo lenye ukubwa wa ekari Saba alilowekeza kituo Cha mafuta lililopo Ngulelo ,jijini Arusha, Mara baada ya mahakama hiyo kujiridhisha kwamba alikuwa anamiliki kinyume Cha Sheria.
Kesi hiyo ya madai namba 1 /2017 ilikuwa ikisikilizwa na Jaji Mosses Mzuna wa mahakama hiyo ambaye aliridhika pasipo shaka kwamba eneo hilo ni Mali halali ya William Taitus Mollel Mkazi wa Ngulelo jijini Arusha.
Katika uamuzi wa jaji Mzuna alioutoa Mei 11 mwaka huu alizingatia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili ikiwemo vielelezo vya umiliki,ndipo alipobaini kwamba mollel hakuwa Mmiliki halali bali alivamia pasipo kufuata Sheria za umiliki.
Jaji Mzuna alipomtaja Mollel kama mvamizi wa eneo hilo ambaye hakuwahi kutambulika kama Mmiliki halali wa eneo hilo ambalo aliliendeleza kwa kuwekeza kituo Cha Mafuta pamoja na biashara zingine.
Kesi hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka mitano ilichukua sura mpya hapo jana mara baada ya walinzi kutoka kampuni binafsi ya ulinzi kuvamia eneo la kituo cha Mafuta na kuzua taharuki kwa kuwatimua wafanyakazi hao na kisha kulizungumzia utepe eneo hilo.
Hata hivyo upande wa Mollel ulijaribu kujibu mapigo kwa kuleta walinzi wake ili kuokoa kituo hicho cha Mafuta lakini polisi wenye silaha za Moto waliingilia Kati na kufika eneo la tukio baada ya kuarifiwa kuwepo kwa dariri za uvunjifu wa Amani na kufanikisha kuwasambaratisha watu waliojaribu kuleta vurugu.
Akizungumzia hatua hiyo Taitas amesema kwamba anaishukuru mahakama hiyo kwani imetenda haki na kuwashauri watu wengine waliodhulumiwa maeneo yao na watu wenye fedha kudai haki yao mahakamani.
Kwa upande wake Philemon Mollel alidai kutoridhika na maamuzi ya mahakama hiyo na tayari amekata rufaa kupinga uamuzi huo .
Mollel alisema kuwa kilichofanyika ni uhuni kwa sababu mahakama hiyo haikuelekeza apokonywe eneo hilo kibabe na kumfungia biashara zake.
Alisema kuwa eneo hilo lenye viwanja vinne aliinunua kisheria mwaka 2009 kutoka kwa Jimmy Taitas Mollel kwa makubaliano ya shilingi milioni 95 kwa kila kiwanja kimoja na kufanya uwekezaji wa Kituo Cha Mafuta na sehemu ya kuoshea magari .
Alisema mwaka 2017 familia ya Taitas walifanya mabadiliko ya msimamizi wa mirathi kwa kumteua Mdogo wao William Taitas Mollel ambaye mwaka 2017 alifungua shauri mahakamani alidai eneo hilo.
Alisema baada ya kutoka hukumu na wao kushindwa waliamua kukata rufaa kupinga hukumu hiyo na ameshangaa kuona Taitas akivamia kutuo cha Mafuta na kusitisha shughuli zote za biashara yake.
Mollel amelalamika kutopata msaada wowote kutoka Jeshi la polisi kutokana na kitendo Cha uvamizi kilichofanywa na William Taitas Mollel kwa kufungia biashara zake.
Ends...
Kesi hiyo ya madai namba 1 /2017 ilikuwa ikisikilizwa na Jaji Mosses Mzuna wa mahakama hiyo ambaye aliridhika pasipo shaka kwamba eneo hilo ni Mali halali ya William Taitus Mollel Mkazi wa Ngulelo jijini Arusha.
Katika uamuzi wa jaji Mzuna alioutoa Mei 11 mwaka huu alizingatia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili ikiwemo vielelezo vya umiliki,ndipo alipobaini kwamba mollel hakuwa Mmiliki halali bali alivamia pasipo kufuata Sheria za umiliki.
Jaji Mzuna alipomtaja Mollel kama mvamizi wa eneo hilo ambaye hakuwahi kutambulika kama Mmiliki halali wa eneo hilo ambalo aliliendeleza kwa kuwekeza kituo Cha Mafuta pamoja na biashara zingine.
Kesi hiyo iliyodumu kwa zaidi ya miaka mitano ilichukua sura mpya hapo jana mara baada ya walinzi kutoka kampuni binafsi ya ulinzi kuvamia eneo la kituo cha Mafuta na kuzua taharuki kwa kuwatimua wafanyakazi hao na kisha kulizungumzia utepe eneo hilo.
Hata hivyo upande wa Mollel ulijaribu kujibu mapigo kwa kuleta walinzi wake ili kuokoa kituo hicho cha Mafuta lakini polisi wenye silaha za Moto waliingilia Kati na kufika eneo la tukio baada ya kuarifiwa kuwepo kwa dariri za uvunjifu wa Amani na kufanikisha kuwasambaratisha watu waliojaribu kuleta vurugu.
Akizungumzia hatua hiyo Taitas amesema kwamba anaishukuru mahakama hiyo kwani imetenda haki na kuwashauri watu wengine waliodhulumiwa maeneo yao na watu wenye fedha kudai haki yao mahakamani.
Kwa upande wake Philemon Mollel alidai kutoridhika na maamuzi ya mahakama hiyo na tayari amekata rufaa kupinga uamuzi huo .
Mollel alisema kuwa kilichofanyika ni uhuni kwa sababu mahakama hiyo haikuelekeza apokonywe eneo hilo kibabe na kumfungia biashara zake.
Alisema kuwa eneo hilo lenye viwanja vinne aliinunua kisheria mwaka 2009 kutoka kwa Jimmy Taitas Mollel kwa makubaliano ya shilingi milioni 95 kwa kila kiwanja kimoja na kufanya uwekezaji wa Kituo Cha Mafuta na sehemu ya kuoshea magari .
Alisema mwaka 2017 familia ya Taitas walifanya mabadiliko ya msimamizi wa mirathi kwa kumteua Mdogo wao William Taitas Mollel ambaye mwaka 2017 alifungua shauri mahakamani alidai eneo hilo.
Alisema baada ya kutoka hukumu na wao kushindwa waliamua kukata rufaa kupinga hukumu hiyo na ameshangaa kuona Taitas akivamia kutuo cha Mafuta na kusitisha shughuli zote za biashara yake.
Mollel amelalamika kutopata msaada wowote kutoka Jeshi la polisi kutokana na kitendo Cha uvamizi kilichofanywa na William Taitas Mollel kwa kufungia biashara zake.
Ends...