Arusha: Mahakama yaahirisha uamuzi wa rufaa ya dhamana ya Mbunge Lema hadi tarehe 20 Dec

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo Ijumaa tarehe 16.12.2016 majira saa 4 asubuhi itatoa uamuzi dhidi ya Pingamizi la awali lililowekwa na Mawakili wa upande wa serikali kwenye rufaa mpya ya dhamana yaliyowasilishwa mawakili upande wa Mbunge Godbless Lema.

Pia kutasikilizwa kwa maombi upande wa mawakili wa mbunge Lema. Wananchi wote mnakaribishwa kujitokeza kwa wingi mahakamani ili kumtia moyo Mbunge wenu Godbless Jonathan Lema.

[HASHTAG]#Justice[/HASHTAG] For Lema

[HASHTAG]#Bring[/HASHTAG] Back Ben Saanane

[HASHTAG]#Justice For [/HASHTAG]Maxence Melo
============
Wakili anayemtetea Mbunge Godbless Jonathan Lema Sheck Mfinanga ameshawasili

Jeshi la Polisi wamezuia wananchi kuingia mahakamani kusikiliza kesi ya mbunge Godbless Lema.

Tulipewa taarifa kesi itaanza kusikilizwa kuanzia saa 10.00 mpaka sasa bado hajaanza.

Kesi ya kwanza inaendelea mahakamani muda huu tumezuia kuingia ndani.

Waandishi wa habari tumezuia kuingia mahakamani kusikiliza kesi ya mbunge Godbless Jonathan Lema kwa kisingizio kuwa ndani nafasi ni ndogo sana.

Geti la kwanza tumekaguliwa tukaruhusiwa kuingia ndani tena kukawa na ukaguzi mwingine wakutoa kitambulisho tofauti na geti la kwanza,licha ya kuonyesha vitambulisho kisingizio kikaja hamna nafasi ndani.

Pingamizi la upande wa mawakili wa serikali la kwanza limetupiliwa nje.

Mapingamizi mawili juu ya rufaa ya dhamana ya kesi inayomkabili Lema zilizowekwa na Serikali yametupiliwa mbali na mahakama mchana huu.

Shauri upande wa mawakili wa mbunge Godbless Lema limeshaanza kusikilizwa
Kesi ya rufaa ya dhamana inaendelea mahakamani muda huu.
Majibizano ya kisheria yanaendelea muda huu mahakamani.

Kesi bado inaendelea mahakamani maamuzi yakitolewa tutawaletea taarifa muwe na subira kuna mabishano makubwa sana ya kisheria kati pande zote mbili

Uamuzi umetolewa kesi ya Mbunge Godbless Jonathan Lema imearishwa mpaka tarehe 20.12.2016

Tarehe 20.12.2016 ndo maamuzi kuhusu dhamana ya Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema yatatolewa.

========

Pingamizi la serikali latupwa kesi ya Lema

Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imetupilia mbali pingamizi la mawakili wa serikali ilizoweka dhidi ya taarifa ya dharura ya kusudio la kukataa rufaa ya mawakili wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godblees Lema.

Lema%20kurudi%20gerezani.jpg

Mbunge Godbless Lema akirudishwa gerezani

Jaji Modesta Opiyo wa mahakama kuu kanda ya Arusha alisema katika maamuzi yake kuwa pingamizi zilizowekwa hazina msingi kwani waleta maombi walifuata taratibu zote za katika kiapo na hati ya dharua ya kuitwa mahakamani.

Baada ya uamuzi huo Jaji Opiyo aliwataka mawakili wa Lema ,Shedrack Mfinanga na Faraji Mangula kuwasilisha hoja zao katika kiapo na hati ya dharura.

Akizungumza baada ya kukubaliwa na Jaji ,wakili Mfinanga alimtaka Jaji huyo kusikiliza rufaa hiyo kwani kuchelewa siyo sababu ya msingi sana kwa mujibu wa sheria na kunukuu kesi mbalimbali zilizochelewa kukatiwa rufaa kwa siku nyingi na kudai kuwa mahakama ya rufaa ilizikubali na kuzitolea maamuzi.

Mfinanga amesema na kumwomba Jaji kusikiliza rufaa yao kwa sababu ni ya msingi na kamwe haiwezi kuvunja sheria ya makosa ya jinai iliyowekwa kwa mujibu wa sheria.

Mawakili wa serikali wakiongozwa na Wakili Mfawidhi Materius Marandu, Hashim Ngole na Elizabert Swai walipinga vikali kukubaliwa kwa rufaa hiyo kwa madai kuwa Jaji Msengi alitupilia mbali na kurudia kuikubali ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za makosa ya Jinai.

Baada ya malumbano hayo yaliyochukuwa zaidi ya masaa 5 Jaji Opiyo alisema kuwa uamuzi wa kuikubali ama kuikataa rufaa hiyo atautoa Desemba 20 mwaka huu majira ya saa 6 mchana katika mahakama hiyo.

Lema-Arusha.jpg


Godbless Lema

Lema anakabiliwa na kesi hiyo ya uchochezi aliyosomewa katika mahakama ya wilaya ya Arusha mbele ya hakimu mkazi Deusdedit Kamugisha Novemba 8 mwaka huu na aliwekewa pingamizi na mawakili wa serikali ya kutopata dhamana baada ya hakimu kusema kuwa dhamana iko wazi.

Mbunge huyo wa Arusha Mjini alikamatwa Novemba 2 mwaka huu Mkoani Dodoama kwa kosa hilo baada ya kuhutubia katika mikutano ya hadhara katika kata mbalimbali za Jiji la Arusha kuwa ameoteshwa kuwa Rais Magufuli atakufa kabla ya mwaka 2020 hali inayodaiwa kuleta uchochezi kwa wananchi waliomchagua kuwa Rais wa nchi.

Chanzo: IPP Media
 
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo Ijumaa tarehe 16.12.2016 majira saa 4 asubuhi itatoa uamuzi dhidi ya Pingamizi la awali lililowekwa na Mawakili wa upande wa serikali kwenye rufaa mpya ya dhamana yaliyowasilishwa mawakili upande wa Mbunge Godbless Lema. Pia kutasikilizwa kwa maombi upande wa mawakili wa mbunge Lema.
Wananchi wote mnakaribishwa kujitokeza kwa wingi mahakamani ili kumtia moyo Mbunge wenu Godbless Jonathan Lema.

[HASHTAG]#Justice[/HASHTAG] For Lema

[HASHTAG]# Bring[/HASHTAG] Back Ben Saanane

[HASHTAG]#Free[/HASHTAG] Maxence Melo
Hatoki ng'o..labda kama mungu wake aliyempa maono hatari kwa usalama wa rais wa jamhuri amekamatwa. Huyu mungu wa lema akikamatwa atasimamishwa kizimbani na lema kujibu mashtaka sawa na ya lema. Muda wa cdm kucheza na sharubu
umeisha. sasa ni kichapo kwa sheria mbele kwa mbele.
 
New
Tahariri hii imetoka gazeti la Zama Mpya

BEN-SAANANE-e1481561687834.jpg


Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya ahadi za TANU ilikuwa ni ile iliyosema “Binadamu wote ni sawa” na pia “kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake”. Ahadi hizi baadaye ziliingizwa pia kwenye Katiba yetu kama sehemu ya Haki za Msingi (Bill of Rights).

Kimsingi, kanuni hizi zinatuambia kuwa tunaweza kuwa na tofauti nyingi sana baina yetu, kuanzia zile za kidini, kisiasa, rangi, lugha, asili ya kitaifa n.k. Lakini mwisho wa yote sisi sote kama binadamu ni “sawa”. Usawa huu hauko katika masuala ya kisheria, hali, hadhi, ujiko, ukwasi n.k bali ni usawa unaotokana na ubinadamu wetu. Kwamba sisi sote kama binadamu tumeumbwa sawa na utu wetu wote ni sawa. Hakuna mwenye utu zaidi ya mwingine!

Taarifa za kupatikana miili ya watu saba ambao inadaiwa walikuwa wamefungwa kwenye viroba wakiwa na dalili za kuwa wameteswa au kuumizwa ni taarifa ambazo zinapasa kumshtua kila mtu anayejiona yeye ni binadamu. Katika usawa wetu wa kibinadamu tunajikuta tunaitwa siyo tu kuhoji lakini pia kupaza sauti kwa niaba ya binadamu wenzetu hao ili kutaka haki juu yao itendeke.

Bahati mbaya taarifa hizi pia zimehusishwa na kutoweka kwa miongoni mwa vijana wanaharakati Bw. Ben Saanane ambaye hajaonekana kwa muda sasa. Ninasema ni bahati mbaya kwa sababu Ben Saanane amekuwa akijihusisha na masuala ya kisiasa na hata ukosoaji wa viongozi walioko madarakani. Kutoonekana kwake katika kipindi kile kile ambacho miili hii imepatikana na kuzikwa kwa kile ambacho watu wanaona kama ni ‘haraka haraka’ kunawafanya watu wahisi labda kijana huyu ni miongoni mwa watu hao.

Binafsi naamini kwanza kabisa hata kama Ben Saanane angekuwa hajakosekana kama hivi na kama angekuwa anaendelea na shughuli zake bado kupatikana kwa miili hiyo kungetusukuma kutaka kujua ni nini kinaendelea, kwanini na na ni nani anahusika.

Kuna mambo kadhaa ambayo ni kweli. Kwamba, hao watu hawakujifunga wenyewe kwenye viroba lakini pia ni vigumu kuamini kama walijitumbukiza wenyewe wakiwa kwenye viroba kwenye mto Ruvu. Hili kimantiki haliwezekani. Ni wazi kuna binadamu wengine walihusika katika kufanya hili – la kuwafunga kwenye viroba na kuwatumbukiza mtoni. Na kama ni kweli watu hao walikuwa wameuawa kabla ya kufungwa au kutupwa mtoni basi ni wazi pia kuwa kuna watu walihusika na mauaji hayo.

Ni kwa sababu hiyo naweza kusema kuwa ni ukosefu mkubwa wa hekima na weledi kwa chombo chochote cha umma kutokufuata taratibu za msingi za kiutu za kushughulikia watu hao. Baada ya miili kukutwa ikielea jambo kubwa na la msingi kufanyika – kwa taratibu za kisheria na kawaida kabisa – ni kutaka kujua kwanza hao ni kina nani, walikufa vipi, na kwanini wapatikane eneo moja, na ni nani anahusika.

Maelezo ambayo yametolewa yenye kuashiria kuwa hawa ni “wahamiaji haramu” yanazua maswali mengi zaidi kuliko yanayojibu. Kama Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Mwigulu Nchemba anajua kuwa hawa ni wahamaiji haramu basi ni muhimu kwenda mbele zaidi na kujibu maswali zaidi badala ya kuyaacha yaning’inie hewani kama mzoga uliooza. Yeye kama Waziri wa Mambo ya Ndani bila ya shaka atakuwa na majibu ya maswali yote haya. Hawa ni wahamiaji kutoka nchi gani na walijuaje? Je, ni kwanini waliuawa? Je, majina yao ni kina nani? Je, ni nani walihusika na ama mauaji yao au kuwatumbukiza mtoni?

Kama nilivyosema awali hawa ni binadamu; utu wao haujadiliki kwani binadamu wote ni ‘sawa’ na wote wana utu sawa. Hata adui bado ni binadamu. Hata mtu unayemchukia bado ni binadamu. Kanuni hii ya msingi iliyoliunda taifa letu haipaswi kupotezwa au kudharauliwa na yeyote.

Lakini swali la msingi na muhimu ni je Serikali iko tayari kuacha vyombo huru kufanya uchunguzi wa miili hiyo ili kujiridhisha kuwa hawa siyo Watanzania na raia wa Tanzania ambao wanalindwa na sheria mbalimbali za nchi yetu?

Binafsi naamini ili kuondoa hisia kuwa serikali ama inahusika – moja kwa moja au kwa namna moja – na tukio hili ni vizuri kwanza kabisa miili yote ifukuliwe, ifanyiwe uchunguzi wenye kushirikisha watu huru, na hatimaye taarifa itolewe (post mortem) ili kutoa wasiwasi wowote ambao unaweza kuonekana umeingia kwa wananchi.

Lakini pia, ni jukumu la vyombo vyote vya serikali ikiwemo TISS, Polisi na vyombo vingine vya usalama kuhakikisha kijana Ben Saanane anapatikana kwani kutokupatikana kwake kunaleta ubaridi katika harakati za kisiasa nchini. Hii ni kwa sababu kama miili ya watu hao ni kazi ya kundi la kihalifu nchini na kutokujulikana au kupatikana kwa kundi hilo kunaweza kutumiwa kisiasa kuonesha kuwa serikali inaanza au taasisi zake zinaanza kufanya kile ambacho kimeshuhudiwa huko Burundi na Rwanda na kwenye baadhi ya nchi ambazo siasa zake hazijali sana haki za raia au zile haki za kibinadamu. Ni kwa maslahi ya serikali kumpata Ben Saanane.

Ni matumaini yangu, kuwa serikali yetu itafanya yote yanayopaswa ili kuondoa wingu la hofu ambalo linaweza kufanya watu wahofie serikali yao. Kupatikana kwa Ben Saanane na kufanyiwa uchunguzi kwa miili iliyopatikana Ruvu ndio njia pekee ya kuzidi kuonesha kuwa serikali ya Awamu ya Tano inajali wanyonge na wale wasio na watetezi hata kama watu hao ni wahamiaji au wanasiasa wa upinzani au wale ambao wanawakera au wanaoweza kuwaona kuwa ni maadui wao.

Nje ya hapo maswali yanayoulizwa sasa hayatakoma na yatapaswa kuulizwa na kutakiwa kujibiwa siku moja. Hata kama siku hiyo itachelewa. Na majibu yake yatakapopatikana wahusika wote bila kujali vyeo vyao vya sasa, hadhi zao za sasa, au kile wanachoweza kuamini kuwa ni kinga za sasa siku moja wataitwa kujibu mbele ya Watanzania, na mbele ya Mungu.

Acha tuone Kamanda kama Atatoka leo!
Ni vigumu pale kuna mahakim wanaopokea mahagizo toka ofisi za ccm pale makao makuu
 
Vyovyote itakavyo kua Lema amejifunza sasa, akitoka nje nidhamu itarudi, Lema aliweka uzi humu kuwaonya vijana kua Rais haziakiwi.. Na shangaa na yeye kafanya ujinga huo huo.. Lema akitoka sasa hivi.. Hawezi rudia, maana atajua akirudi tena anaweza kukaa Mwaka
 
Back
Top Bottom