figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,483
- 54,846
Madiwani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha watangaza kujiuzulu na kuhamia Chama Chama cha Mapinduzi (CCM). Madiwani hao ni Zacharia Mollel wa kata ya Oloirieni, diwani wa kata ya Themi Melance Kinabo na diwani wa Kata ya Unga Limited James Lyatuu.
====
Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jiji la Arusha wamejiuzulu na kuhamia katika Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa maelezo kuwa wanaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli.
Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jiji la Arusha wamejiuzulu na kuhamia katika Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa maelezo kuwa wanaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli.
Madiwani hao ni pamoja na Welance Kinabo (Themi), Zakaria Mollel (Oloirien), na James Lyatuu (Unga Limited). Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Dk. Maulid Madeni amethibitisha kupokea barua za madiwani hao kujiuzulu.
“Nimepokea barua zao nitatoa taarifa baaadaye,” amesema Madeni.
Hivi karibuni aliyekuwa Meya wa jiji hilo, Kalist Lazaro alijiuzulu na kujiunga na CCM. Katika uchaguzi mkuu wa 2015, Chadema kilikuwa na madiwani 25 na CCM mmoja, lakini kutokana na baadhi ya madiwani kuhamia chama hicho tawala kimekuwa na madiwani nane hadi sasa na Chadema kubakia 15.
====
Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jiji la Arusha wamejiuzulu na kuhamia katika Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa maelezo kuwa wanaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli.
Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika jiji la Arusha wamejiuzulu na kuhamia katika Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa maelezo kuwa wanaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli.
Madiwani hao ni pamoja na Welance Kinabo (Themi), Zakaria Mollel (Oloirien), na James Lyatuu (Unga Limited). Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Dk. Maulid Madeni amethibitisha kupokea barua za madiwani hao kujiuzulu.
“Nimepokea barua zao nitatoa taarifa baaadaye,” amesema Madeni.
Hivi karibuni aliyekuwa Meya wa jiji hilo, Kalist Lazaro alijiuzulu na kujiunga na CCM. Katika uchaguzi mkuu wa 2015, Chadema kilikuwa na madiwani 25 na CCM mmoja, lakini kutokana na baadhi ya madiwani kuhamia chama hicho tawala kimekuwa na madiwani nane hadi sasa na Chadema kubakia 15.