Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Nimepata taarifa kuwa ommy255 hapatikani toka Ijumaa usiku.
Mtoa taarifa anasema haonekani nyumbani, kwa marafiki wa karibu, kwa majirani, simu haipo hewani.
Kwamba kwa mara ya mwisho alipost mitandaoni taarifa ya kukabidhi rambirambi kwa Mhe Josephine S. Lemoyan tukio lililotendeka Njiro Kontena (Shule ya Msingi) nyumbani kwa marehemu Hussein Rasta.
Hebu tusaidiane kusambaza taarifa hii kwa jinsi tuwezavyo maana Mtu anapokosekana kuonekana maeneo ya mazoea tunajawa na wasiwasi.
Kati ya timu ya watu takribani 13 walofika kutoa rambirambi ommy255 aliondoka wa kwanza aliaga kwenda kufunga ofisi yake.
Kwa taarifa nilizopata Ommy baada ya kutoka kwenye msiba alirudi dukani na alifunga Duka vizuri tu ila wakati anarejea nyumbani alivamiwa na watu akapigwa sana na kunyanganywa kila kitu ila alifanikiwa kurudi kwake akawaeleza ndugu zake kilichomkuta Asbh kulivyokucha aliwaambia ndugu zake anasikia maumivu makali ivo anaenda HSP,basi ndio hajarudi tena mpka sasa na wamezunguka HSP zote Ommy hayupo