Arusha Jiji kuongeza shuke za A, krvel

kwedikwazu

Member
Dec 17, 2016
18
15
8713a66da13311f2ab9aa186de799a5b.jpg
Kwa Hivi sasa Jiji la Arusha lina shule mbili tu zinazopokea wanafunzi wa Kidato cha Tano ambazo ni Arusha Sec n Arusha Girls.

Kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaofaulu kidato na Nne na namna ambavyo shule zilizopo zinavyopokea idadi kubwa ya wanafunzi wa kidato cha Tano Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Daqarro amemuagiza Mkurugezi Ndg. Athumani Kihamia kuhakikisha anaongeza shule za Kidato cha Tano kufikis mwaka 2018.

Daqaro ameyasema hayo wakati akipokea taarifa ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Tano kuanzia July mwaka huu na kueleza kuwa wanafunzi waliochaguliwa ni 578 kati ya hayo wasichana ni 322 huku wavulana wakiwa 256.

Aidha amempongezs Mkurugenzi Kihamia pamoja na Menejinent kwa kusimamia Upatikanaji wa Elimu bora kwa wanafunzi mpaka kupelekea kiwango cha ufaulu kuongezeka.

Naye Mkurugenzi wa Jiji Ndg. Athumani Kihamia amesema amepokea agizo hilo na atatekeleza haraka iwezekanavyo kutokana na kuwekwa kwenye bajeti itakayoanza July 2017 na shule hizo ni Korona(bweni) na Suye(Kutwa).

Ameongeza kuwa ataendelea kusimamia maslah ya Walimu ikiwa ni pamoja na kulipa Stahiki zao kwa wakati na kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ili waweze kuwa na moyo zaidi ya kufundisha kwa weledi wanafunzi wanaosoma katika Jiji hili.
 
Ungeweka wazi kama ni government schools au private schools
 
Daah KALOLENI NA ARUSHA DAY BADO ZINAKIMBIZANA TU KWENYE KUFAULISHA...WAKO VIZURI
 
Arusha girls ipo kwenye eneo zuri sana na tulivu, ile shule ikiwa na uongozi madhubuti, walimu wazuri na maabara nzuri itakuja kutoa wanafunzi bora sana..
 
Back
Top Bottom