Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Juzi tumeendelea kushuhudia uhaini wa demokrasia ukifanyika ndani ya nchi yetu wakati wa uchaguzi wa meya wa manispaa ya Arusha. Nauita uhaini kwa sababu kitendo kilichofanywa na madiwani wa CCM kumchagua meya toka uchochoroni ni kudhihirisha oroho wa madaraka wa chama hicho.
Kutokana na kanuni za mabaraza ya halmashauri, yaani uchaguzi utafanyika tu endapo kolamu imetimia 2/3 ya wajumbe kitu ambacho hakikuwepo ni dhahiri kuwa kanuni zimekiukwa, na kwa kitendo hicho CCM imebaka demokrasia ni sawa na mapinduzi ya kijeshi.
Nakishauri chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, pamoja na kukusudia kwenda mahakamani waitishe mapema uchaguzi wao wa meya chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi kuchagua meya atakayefanya kazi sambamba na meya wa CCM.
Najua mwanzo CCM watakibeza kitendo hiki kama walivyobeza walkout ya wabunge kususia hotuba ya rais lakini baadaye watakuja kutambua umuhimu wa wake baada ya jamii kuona msuguano utakaokuwepo. Serikali ya Ivory Coast ilibeza vile vile rais kujiapisha lakini leo wanazungumuza lugha nyingine.
Kwa kitendo hicho Chadema watakuwa wanaua ndege wawili kwa jiwe moja.
Hivi Chadema watajifanya wastaarabu hadi lini wakati CCM haionyeshi ustaarabu?
Kutokana na kanuni za mabaraza ya halmashauri, yaani uchaguzi utafanyika tu endapo kolamu imetimia 2/3 ya wajumbe kitu ambacho hakikuwepo ni dhahiri kuwa kanuni zimekiukwa, na kwa kitendo hicho CCM imebaka demokrasia ni sawa na mapinduzi ya kijeshi.
Nakishauri chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, pamoja na kukusudia kwenda mahakamani waitishe mapema uchaguzi wao wa meya chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi kuchagua meya atakayefanya kazi sambamba na meya wa CCM.
Najua mwanzo CCM watakibeza kitendo hiki kama walivyobeza walkout ya wabunge kususia hotuba ya rais lakini baadaye watakuja kutambua umuhimu wa wake baada ya jamii kuona msuguano utakaokuwepo. Serikali ya Ivory Coast ilibeza vile vile rais kujiapisha lakini leo wanazungumuza lugha nyingine.
Kwa kitendo hicho Chadema watakuwa wanaua ndege wawili kwa jiwe moja.
Hivi Chadema watajifanya wastaarabu hadi lini wakati CCM haionyeshi ustaarabu?