Augustine Moshi
JF-Expert Member
- Apr 22, 2006
- 2,554
- 1,382
Haikumwagiga damu kumg'oa mkoloni mweupe, lakini CCM ni mkoloni mweusi king'ang'anizi, anapiga na hata kuua ili abaki madarakani. Green Guards ni militia ya CCM ya kufanya vita dhidi ya Watanzania kama itabidi, na kama ambavyo imeshabidi.
Ni muhimu CDM iunde kitengo cha kukusanya ushahidi. Ningeshukuru kama kingeongozwa na Kamanda Lisu. Tukisharudisha tena utawala wa kisheria basi wote wale waliopiga na kuua with impunity wafikishwe mahakamani. Lazima mwishowe haki itendeke.
Lazima mwishowe hawa Green Guards wafungwe. Lazima mwishowe RPC Kamuhanda, RPC Andengenye, Kamishina Mwema na wote wale ambao sasa wamejitwalia sheria mkononi wafungwe. Wengi wao wanadhani sasa watang'atuka na kupumzika uzeeni, lakini ukweli ni kwamba watafia jela.
CDM inawajibika kuhakikisha haki itatendeka, hakuna damu itamwagwa kama ya kuku. Lazima wahusika waajibishwe.
Ni muhimu CDM iunde kitengo cha kukusanya ushahidi. Ningeshukuru kama kingeongozwa na Kamanda Lisu. Tukisharudisha tena utawala wa kisheria basi wote wale waliopiga na kuua with impunity wafikishwe mahakamani. Lazima mwishowe haki itendeke.
Lazima mwishowe hawa Green Guards wafungwe. Lazima mwishowe RPC Kamuhanda, RPC Andengenye, Kamishina Mwema na wote wale ambao sasa wamejitwalia sheria mkononi wafungwe. Wengi wao wanadhani sasa watang'atuka na kupumzika uzeeni, lakini ukweli ni kwamba watafia jela.
CDM inawajibika kuhakikisha haki itatendeka, hakuna damu itamwagwa kama ya kuku. Lazima wahusika waajibishwe.