Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kimandolu kupitia Chadema Grayson Ngowi, Ameingia katika Malumbano Mazito na mama Mwenye nyumba Mara baada ya kushindwa kulipa kodi ya nyumba kwa mwaka moja na miezi Mitatu kiasi cha shilingi millioni Tatu na Laki sita pamoja na kumtapeli Sofa seti ya kijana wake ikiwa ni zawadi ya Arusi .
Akizungumza na vyombo vya habari kwa masikitiko makubwa Mama mwenye nyumba aliyejitambulisha kwa jina la Mama Hendry amesema diwani huyo ambaye ni mchungaji amemtesa kwa muda mrefu na kodi yake
Mama huyo ameleza kuwa Mchungaji huyo alipewa notisi ya kuhama katika nyumba yake ya miezi minne kuisha amegoma kuhama na pia kugoma kulipa fedha zake mpaka sasa
Amesema mchungaji huyo ni tapeli kwani amekuwa akimpa ahadi za mara kwa mara kulipa fedha zake lakini amekuwa akimzungusha kulipa fedha zake .
Sikuchache mchungaji huyo aliyejivua udiwani kwa tiketi ya Chadema na kutimkia Ccm mbele ya Rais Magufuli katika uwanja wa mpira shekh Amri Abed Stadium Arusha .
Mama huyo ameomba msaada kwa viongozi wa serikali akiwemo mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema na Meya wa jiji la Arusha Kalisti Lazaro kuingilia kati kwani mchungaaji huyo alikuwa kiongozi mwenzao na sasa sio tena na kama kuna kiongozi aliye karibu naye amsaidie kwani amesikia amenunuliwa anapesa hivyo amlipe kodi yake,
,