ARUMERU: Wabunge wa CCM wakosa hoja, wajikita kwenye uchaguzi na ukabila

MWITONGO MAARIFA

JF-Expert Member
Aug 11, 2018
276
1,428
Mhe. Rais yupo ARUMERU kuzindua mradi wa maji ambapo Mbunge wa Arumeru hayupo katika uzinduzi huo. Wabunge wa ccm waliopo wanadai Mbunge huyo amelikimbia Jimbo na hivyo wananchi hawana wa wakuwasemea lakini kila wanapozungumza wanaonyesha kabisa hata jeographia ya wilaya hiyo hawaijui na hawakuwa tayari kujifunza kabla ya Rais kufika.

Mhe. Milya wa simanjiro badala ya kutoa hoja amekariri mstari mmoja wa biblia ndo anauzungumzia lakini pia anampongeza Rais ka kumteua DC wa Hai Bw.Sabaya akidai kuwa ni uthibitisho kuwa Rais siyo mbaguzi. Kwa tafsiri nyepesi huyu mbunge ubaguzi kwake ni kuteuliwa kuwa DC lakini anashindwa kujua huyo ni mwanaccm na anayohaki yakuteuliwa hata angekuwa mbondei

Hakuna anayezungumzia ugumu wa maisha, hakuna anayezungumzia madhara ya kushuka kwa utalii, hakuna anayewazungumzia wafanyabishara wanaonyanyaswa kwa Kodi lukuki, hakuna anayeomba kibali Cha kuuza mazao ndani na nje ya nchi kulingana na soko badala yake wamebaki kusifia bila kujiuliza chanzo cha fedha za hiyo miradi ni Nini?

CCM jaribuni kutafuta wajenga hoja achaneni na Mambo ya kusifia kila Jambo hata Kama Ni baya maana mnawafanya viongozi waamini Hali ni shwari kumbe si swari
 
CHA KUSHANGAZA NI KUWA PAMOJA NA KUWA WANASEMA WAPINZANI WANAKIMBIA MAJIMBO YAO NA WANANCHI HAWANA WA KUWASEMEA, BADO MWENYEKITI WAO ANAOGOPA HADI KIVULI CHAKE? AKISIKIA JINA MEMBE, ZITTO, MBOWE ANACHANGANYIKIWA
 
Hicho kinachoendelea hapo ni siasa chafu katika uzinduzi wa mradi wa maji. Kwasasa ni nadra kutofautisha kampeni za ccm na uzinduzi wa miradi. Ninachokiona, cdm ni chama kilichoweka hofu kubwa kuanzia kwa mwenyekiti wa ccm mpaka wafuasi wake, kiasi ni nadra sana mkutano/hafla yoyote usisikie cdm ikitajwa tena kwa mtindo wa siasa chafu. Simply huo uzinduzi ni eneo la kusikilizia siasa chafu za ccm.
 
Wananchi wanaoshangilia haya maigizo ni wachache.. Angalia TBC utajionea
 
Mleta mada ni mzushi arifu. Mie niko hapa. Watu wanafuraha kweli juu ya kazi za MAGUFULI na CCM. Maasai na wa wameru wameshaapa wakiwa na malaigwanan wao kwamba 2020 CDM wasijisumbue. Watu wanaangalia live TBC na AZAM. Wabunge wamesema juu ya kero za barabara na umeme na maji. Mleta mada unazingua eti wameleta ukabila. Muone aibu kwenye mambo mengine wakuu
Nikupe konyagi nyingine
 
CHA KUSHANGAZA NI KUWA PAMOJA NA KUWA WANASEMA WAPINZANI WANAKIMBIA MAJIMBO YAO NA WANANCHI HAWANA WA KUWASEMEA, BADO MWENYEKITI WAO ANAOGOPA HADI KIVULI CHAKE? AKISIKIA JINA MEMBE, ZITTO, MBOWE ANACHANGANYIKIWA
Lazima! Mtu alimchimba biti IGP kisa washabiki wa Yanga waliosha gari ya Manji na wanakwaya kuimba nje ya mahakama. Baada ya pale, ndo nikajuwa tumekwisha.
 
Mleta mada ni mzushi arifu. Mie niko hapa. Watu wanafuraha kweli juu ya kazi za MAGUFULI na CCM. Maasai na wa wameru wameshaapa wakiwa na malaigwanan wao kwamba 2020 CDM wasijisumbue. Watu wanaangalia live TBC na AZAM. Wabunge wamesema juu ya kero za barabara na umeme na maji. Mleta mada unazingua eti wameleta ukabila. Muone aibu kwenye mambo mengine wakuu
So true
Watanzania watawapiga mawe machandrama mcharuko 2020 Maana tumegundua nia yao ni kumrudisha nyuma Mama Tanzania na juhudi za maendeleo
 
Mhe. Rais yupo ARUMERU kuzindua mradi wa maji ambapo Mbunge wa Arumeru hayupo katika uzinduzi huo. Wabunge wa ccm waliopo wanadai Mbunge huyo amelikimbia Jimbo na hivyo wananchi hawana wa wakuwasemea lakini kila wanapozungumza wanaonyesha kabisa hata jeographia ya wilaya hiyo hawaijui na hawakuwa tayari kujifunza kabla ya Rais kufika.

Mhe. Milya wa simanjiro badala ya kutoa hoja amekariri mstari mmoja wa biblia ndo anauzungumzia lakini pia anampongeza Rais ka kumteua DC wa Hai Bw.Sabaya akidai kuwa ni uthibitisho kuwa Rais siyo mbaguzi. Kwa tafsiri nyepesi huyu mbunge ubaguzi kwake ni kuteuliwa kuwa DC lakini anashindwa kujua huyo ni mwanaccm na anayohaki yakuteuliwa hata angekuwa mbondei

Hakuna anayezungumzia ugumu wa maisha, hakuna anayezungumzia madhara ya kushuka kwa utalii, hakuna anayewazungumzia wafanyabishara wanaonyanyaswa kwa Kodi lukuki, hakuna anayeomba kibali Cha kuuza mazao ndani na nje ya nchi kulingana na soko badala yake wamebaki kusifia bila kujiuliza chanzo cha fedha za hiyo miradi ni Nini?

CCM jaribuni kutafuta wajenga hoja achaneni na Mambo ya kusifia kila Jambo hata Kama Ni baya maana mnawafanya viongozi waamini Hali ni shwari kumbe si swari


Ndiyo elimu yao ilipofikia
 
Back
Top Bottom