Arumeru: Jerry Muro awaambia wananchi kama hawataki kufuata sheria na kanuni za nchi basi wahame nchi

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Utawala wa Mwendo kasi unaendana na Ukiukaji wa Katiba

Nimeona clip inayosambaa mtandaoni ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akielekeza polisi kumkamata mwananchi huku akidai “Kama mmeshindwa kuishi kwenye hii nchi katafuteni nchi nyingine.”

Huu siyo uongozi bali ni udikteta uliopitiliza. Ukiona viongozi wananchi kutamka nchi yangu, serikali yangu, mtanyooka, katafuteni nchi nyingine ya kuishi nk tambua hana maono wala malengo anayopanga kufikia.

Suala analozungumzia la upimaji wa ardhi si suala la kulazimisha ni suala la kisheria na linapaswa kuendeshwa kwa majadiliano na ukilazimisha utawanya watu wanyamaze kwa sababu ya nafisi yako na matumizi ya vyombo vya dola ila ukiondoka au dola ikiondkka mgogoro utakaozaliwa hautasuluishika kirais.

Nakumbuka Mhe. Lukuvi alipita huko Arusha akazungumza na wananchi maeneo mbalimbali na hakukuwepo na ukinzani anaopata Muro, hivyo inaleta tafsiri kuwa yeye anatafuta sifa kwenye kamera bila kuwa na maono.

Usipobadilika utajikuta unawagawa wananchi Kama kiongozi badala ya kuwaunganisha...
 

Attachments

  • VID-20180903-WA0050.mp4
    11.1 MB · Views: 66
ongea yake tu inatosha kujua kuwa kijana kichwa cha panzi
 
Tusi hapo lipo wapi?
Mkuu kuna lugha ya dhihaka, inaweza kukufunga pia. Yale yale ya mwandishi wa habari hajavaa beji kifuani halafu anapandishiana na mapolisi, wanakubutua tu, mpaka video clip ikifika facebook na kutazamwa na kila mtu wewe unakuwa hospitali ukiuguza makovu.
 
Hahahah katafuteni sehemu nyingine yakuishi, ????!!!!!
 
Nimeona clip inayosambaa mtandaoni ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru akielekeza polisi kumkamata mwananchi huku akidai “Kama mmeshindwa kuishi kwenye hii nchi katafuteni nchi nyingine.”

Huu siyo uongozi bali ni udikteta uliopitiliza. Ukiona viongozi wananchi kutamka nchi yangu, serikali yangu, mtanyooka, katafuteni nchi nyingine ya kuishi nk tambua hana maono wala malengo anayopanga kufikia.

Suala analozungumzia la upimaji wa ardhi si suala la kulazimisha ni suala la kisheria na linapaswa kuendeshwa kwa majadiliano na ukilazimisha utawanya watu wanyamaze kwa sababu ya nafisi yako na matumizi ya vyombo vya dola ila ukiondoka au dola ikiondkka mgogoro utakaozaliwa hautasuluishika kirais.

Nakumbuka Mhe. Lukuvi alipita huko Arusha akazungumza na wananchi maeneo mbalimbali na hakukuwepo na ukinzani anaopata Muro, hivyo inaleta tafsiri kuwa yeye anatafuta sifa kwenye kamera bila kuwa na maono.

Usipobadilika utajikuta unawagawa wananchi Kama kiongozi badala ya kuwaunganisha...
 
Back
Top Bottom