safi kwa detail nzuri..
jamani hivi uelewa wa wawakilishi wetu (wabunge) achilia mbali ukereketwa wao wa kijinga, nadiriki kusema wana upeo wa chini sana wengi waooo...hawastahili hata kidogo kuwa law makers na wawakilishi wa wananchi...ni mambumbuuuuuuu...
ukifuatilia mijadala yao wakati wa kujadili mambo muhimu kama nishati, utagundua upeo wao mdogo kwa kuleta mipashoo zaidi kuliko hojaaa...
sio watu makini jamani....wengi hawajui wajibu wao kama wabunge, wengine ni wapenda kuchangia kwa sifa ya kusikika kwenye media zetu ambazo pia ni zao la yale yale upeo mdogoooo...
tumeshuhudia wabunge wachache wa upinzani (dr slaa, hamad, zitto, nk) wakichangia kwa umakini unaostahili katika bunge.
haya matatizo ya tanesco/richmond/dowans na sasa yaongezeka arthumas ni dalili za umbumbu wetu katika kukabiliana na tatizo la nishati nchinii..
haiwezekani kila siku tudai mafisadi wanaingilia miradi yetu, wansheria wanakosea mikatabaa, viongozi hawatambui wajibu wao...na bado wananchi tupo tupo tuuuu...
kuna zaidi ya tatizo....hatuna rasilimali watuuu (we desperately need HUMAN CAPITAL)
Tuna wanasheria waliobobea kwenye mikataba ya nishati??? tuna wabunge makini katika kujadili kuhusu sekta ya nishati? tanesco wakoje kwa upande wa menejimenti (bodi na wafanyakazi wa shirika)? Mgeni wetu EWURA anajenga vipi uwezo wa kuregulate sekta ya nishati? Media yetu ina watu makini(waandishi) wenye upeo na uchumi na sekta ya nishati????????????
Tunao hao wataalamu tatizo ni njaa na ufisadi