Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,587
- 215,184
Umiliki wa ardhi Afrika uliingiliwa na utawala wa kikoloni. Baada ya kupata uhuru nchi nyingi zilishindwa kurudisha ardhi kwa wananchi. Kutokana na misimamo imara ya Baba wa Taifa Tanzania hatuna hali hiyo. RIP.
Tatizo kwetu kiko kwenye matumizi ya ardhi hii. Hii nguvu kazi ya vijana 50% ingetumia ardhi kuzalisha mazao tungeweza za kusambaza matunda, nafaka na mboga Afrika nzima.
Tatizo la kwanza ni masoko, wakishalima watauza wapi? Barabara zetu kwa sasa zinapitika wakati wa jua na mvua kwa 70%. Ni mipango tu ya kuweza kuweza kuzungusha mazao mtu wa Kigoma aweze kununua pears na apple kutoka Lushoto sokoni, wa Mwanza anunue samaki changu dukani, wa Mtwatra ale kabichi na nyanya kutoka Iringa.
Lingine ni elimu ya kilimo. Mafunzo ya kilimo kwa vijana hasa wale ambao haw kusomea kilimo waweze kupata mwongozo.