Ardhi yetu hatujaweza kuitumia vizuri...

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,587
215,184
1104438


Umiliki wa ardhi Afrika uliingiliwa na utawala wa kikoloni. Baada ya kupata uhuru nchi nyingi zilishindwa kurudisha ardhi kwa wananchi. Kutokana na misimamo imara ya Baba wa Taifa Tanzania hatuna hali hiyo. RIP.

Tatizo kwetu kiko kwenye matumizi ya ardhi hii. Hii nguvu kazi ya vijana 50% ingetumia ardhi kuzalisha mazao tungeweza za kusambaza matunda, nafaka na mboga Afrika nzima.

Tatizo la kwanza ni masoko, wakishalima watauza wapi? Barabara zetu kwa sasa zinapitika wakati wa jua na mvua kwa 70%. Ni mipango tu ya kuweza kuweza kuzungusha mazao mtu wa Kigoma aweze kununua pears na apple kutoka Lushoto sokoni, wa Mwanza anunue samaki changu dukani, wa Mtwatra ale kabichi na nyanya kutoka Iringa.

Lingine ni elimu ya kilimo. Mafunzo ya kilimo kwa vijana hasa wale ambao haw kusomea kilimo waweze kupata mwongozo.
 
Nini ushauri wako Sasa kwa serikali hii isiyo sikivu kwa mujibu wa uzi wako huu mkuu....
Ushauri :
1. Kutafuta soko la ndani na nje. Jinsi tutakavyoweza kusafirisha local products national wide.

2. Jinsi ya kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa wanaotaka kuanzisha kilimo cha biashara

3. Kuleta simple farming tools, kusema ukweli kilimo cha jembe la mkono kimepitwa na wakati.
 
Mzizi wa tatizo ni uduni wa elimu. Hilo ndilo linafanya kila kitu watu wasubiri serikali. Serikali inasubiriwa kutafuta masoko! Serikali imefanywa baba, mama na mjomba!

Kenya na Ethiopia wanauza sana maua na mazao ya bustanini Ulaya. Ni serikali inawatafutia masoko? Hapana. Mtu aliyeelimika vizuri anatumia nyenzo za mitandao kujifanyia utafiti na hata kuwasiliana na wahitaji wa mazao anayopanga kulima.

Kijana mwenye elimu pana ya kawaida akiamua kulima mbogamboga hatasubiri serikali imfundishe afanyeje. Atatumia Wikipedia na websites nyingine kujifundisha.

Kuanzia uhuru mpaka miaka ya tisini, kiasi cha bajeti ya Tanzania kwenye elimu kilishuka toka asilimia 20 hadi asilimia 4.9. Kenya kilibaki asilimia 20 na kuongezeka hadi 25.

Tuanze upya. Tuache mzaha kwenye elimu. Bila elimu hatutaweza kutatua matatizo mengine.
 
Mzizi wa tatizo ni uduni wa elimu. Hilo ndilo linafanya kila kitu watu wasubiri serikali. Serikali inasubiriwa kutafuta masoko! Serikali imefanywa baba, mama na mjomba!

Kenya na Ethiopia wanauza sana maua na mazao ya bustanini Ulaya. Ni serikali inawatafutia masoko? Hapana. Mtu aliyeelimika vizuri anatumia nyenzo za mitandao kujifanyia utafiti na hata kuwasiliana na wahitaji wa mazao anayopanga kulima.

Kijana mwenye elimu pana ya kawaida akiamua kulima mbogamboga hatasubiri serikali imfundishe afanyeje. Atatumia Wikipedia na websites nyingine kujifundisha.

Kuanzia uhuru mpaka miaka ya tisini, kiasi cha bajeti ya Tanzania kwenye elimu kilishuka toka asilimia 20 hadi asilimia 4.9. Kenya kilibaki asilimia 20 na kuongezeka hadi 25.

Tuanze upya. Tuache mzaha kwenye elimu. Bila elimu hatutaweza kutatua matatizo mengine.
Mkuu vijana wana kosa soko la nyanya zinaozea shambani au kuuza kwa bahati sh 200 kwa ndoo ya litre 5.

Tuko hapa kubadilishana mawazo ikiwamo jinsi ya kusafirisha perishable products
 
Suluhisho la kilimo chetu ni processing. Kama tutaendelea kuuza mazao ghafi, kilimo hakilipi. Niliwahi kulima tikiti. Matunda yalikubali vizuri. Nikapakia fuso nikaingia nayo sokoni buguruni. Kilichotokea hskifai kuandika hapa. Mwaka jana nilivuna vitunguu magunia 700@ kg 100. Nikikuambia mapato yake utanitukana.
 
Suluhisho la kilimo chetu ni processing. Kama tutaendelea kuuza mazao ghafi, kilimo hakilipi. Niliwahi kulima tikiti. Matunda yalikubali vizuri. Nikapakia fuso nikaingia nayo sokoni buguruni. Kilichotokea hskifai kuandika hapa. Mwaka jana nilivuna vitunguu magunia 700@ kg 100. Nikikuambia mapato yake utanitukana.
Tatizo hapa ni soko, wakati unahangaika hivyo kuna mikoa tikiti maji linahitajika mno. Hapa unahitaji good information na transportation facilities.
 
Tatizo hapa ni soko, wakati unahangaika hivyo kuna mikoa tikiti maji linahitajika mno. Hapa unahitaji good information na transportation facilities.

Sky, hilo ni jibu rahisi. Kwa maendeleo tuliyo nayo sasa kwenye mawasiliano, siamini kuwa wafanyabiashara kutoka mkoa fulani wanashindwa kujua kuhusu uwepo wa bidhaa kwenye eneo jingine.
 
Mkuu vijana wana kosa soko la nyanya zinaozea shambani au kuuza kwa bahati sh 200 kwa ndogo ya litre 5.

Tuko hapa kubadilishana mawazo ikiwamo jinsi ya kusafirisha perishable products

Na mimi nakubaliana na wewe. Labda nianze kutoa angalizo: Hawa wanaobeza ujenzi wa reli ya kisasa wamesoma thread yako?

Back to the topic: Kuna mchangiaji mmoja kasema kuna nchi wakulima wanatafuta masoko wenyewe, hivyo si jukumu la serikali kuwatafutia! Mimi nitatofautiana naye kidogo, japo sipingi kuwa yuko sahihi. Serikali nzuri ni ile inayojua weaknesses za raia wake na kuzifanyia kazi.

Hili la wakulima kutokuwa na knowledge ya masoko bado serikali inaweza kusaidia. Kwa mfano mabalozi wa Tanzania walioko ughaibuni kufanya uchunguzi wa demand ya mazao mbalimbali na kuja info zitazosaidia wakulima wetu. Vinginevyo thread yako ni nzuri sana na Tanzania kama kweli tunataka maendeleo ni basi tuwekeze kwenye kilimo. Tuna ardhi na hali ya hewa nzuri sana.

Na zaidi uwekezaji wa kilimo hauhitaji mtaji mkubwa na complex technology kama uwekezaji mwingine. Hata hii inayoitwa Bandari ya Bagamoyo na mazagazaga yake yote (huku tukiwa tumeweka reheni ardhi yetu) haina faida na si rahisi kama kilimo. Kuna mradi kama wa Lower Moshi irrigation (ukulima wa mpunga) uliojengwa kwa msaada wa Japan.

Mwanzoni ulibadilisha familia nyingi zilizopata bahati ya kuwa kwenye ule mradi na ufukura ukawa umepunguzwa kwa kiwango kikubwa. Lakini baada ya Japan kuondoka, sisi wabongo tumeshindwa kuundeleza na umekufa kabisa.
 
Sky, hilo ni jibu rahisi. Kwa maendeleo tuliyo nayo sasa kwenye mawasiliano, siamini kuwa wafanyabiashara kutoka mkoa fulani wanashindwa kujua kuhusu uwepo wa bidhaa kwenye eneo jingine.
Tatizo ni transportation. Ninajiuliza kama Ulaya wanaweza kula machungwa kwa miezi 12 ya mwaka, wanafahamu machungwa ya Florida ni msimu gani, ya Spain na ya South Africa.
Ingawa sikuhizi wengi wanapinga kuwa usafirishaji wa mazao ya biashara kwa ndege kunachangia global warming kwa kuongeza carbon dioxide.

Pears Kigoma yanahitajika lakini gharama za kusafirisha gunia la pears mpaka Kigoma hata ukuiza moja 5,000 bado hujalipia gharama.
 
Nyuzi nzuri sana minafikriavtukianza kutafuta soko la mazao ya mbogamboga nje ya ncbi itasaidia hasa watu wa chini unaweza usilime ila ukawa mnunuzi wa hizo mboga mboga ukaziexport..utakachofanya ni ww kua nawataalamu wakilimo chamboga mboga ambao watakao toa elimu kwa wakulima kukidhi ubora wa soko
 
Tatizo ni transportation. Ninajiuliza kama Ulaya wanaweza kila machungwa kwa miezi 12 ya mwaka, wanafahamu machungwa ya Florida ni msimu gani, ya Spain na ya South Africa.
Ingawa sikuhizi wengi wanapinga kuwa usafirishaji wa mazao ya biashara kwa ndege kunachangia global warming kwa kuongeza carbon dioxide.

Pears Kigoma yanahitajika lakini gharama za kusafirisha gunia la pears mpaka Kigoma hata ukuiza moja 5,000 bado hujalipia gharama.
Wazo lako ni zuri sana na laiti viongozi wetu wangekuwa na wazo kama hili na kulifanyia kazi kwa nguvu zote basi tungefika mbali. Tatizo tumekuwa tukipiga kelele bila action yoyote.

Kilimo kwanza ilianza kwa mbwembwe nyingi lakini sasa hivi imekufa. Tungewekeza kwenye kilimo na usafiri wa rahisi na uhakika (reli) nchi yetu maisha yangekuwa nafuu sana na tusingeona malalamiko ya ''vyuma kukaza'' kama tunavyoona sasa.

Kwa mfano ukiwa na mabehewa specilized kusafirisha nyanya au maparachichi, una uwezo wa kuleta bidhaa kutoka eg Mbeya mpaka Dar bila uncertainty ya kuhofia kuharibika, plus gharama nafuu vs load!

Tanzania dira yetu ingekuwa kuweka nguvu kwenye KILIMO+USAFIRASHAJI+MASOKO tungenyanyuka. Tukisha piga hatua kwenye hayo matatu ndiyo tungeongeze na VIWANDA (vya ku-process hayo mazao)
 
Kila kiongozi anakuja na sera yake ,yuko wa kilimo kwanza ,yuko wa Viwanda. Nchi ishike lipi sasa!!

Note ili nchi iendelee vyema katika nyanja zote inatakiwa iwe na sekta imara ya kilimo ,hili halipingiki hata kidogo . Refer uingereza ilianza mapunduzi kwenye kilimo kwanza

Kuna eneo Mbeya ukiwa unaelekea tukuyu kabichi nne kubwa ni 1000 na ziko trari kwenye mfuko ,hapo jiulize mkulima anapata nini?

Kilimo kikiboreshwa kitachukua vijana wengi ambao hawana ajira huku mtaani .

Vijana wanajitahid sana kulima ,changamoto hawana ujuzi wa ku-marketing mazao yao hapo ndipo wafanya biashara wanapo waliza wakulima

Serekali ina jukumu la kuhakikisha kuna pembejeo bora kwa wakulima kwa bei nafuu ,hata ikiwezekana kwa mkopo

Serekali pia inatakiwa wakti mwingine ipange bei kwenye baadhi ya mazao kuhakikisha mkulima ananufaika vyema.

Itoe ruzuku pia kwa wakulima .

Itafute masoko ya njee na ndani ya nchi

Iwe na sera nzuri zitakazo wavutia vijana kujiingiza kwenye kilimo

Ku- technologizes vijiji vijana wakitoka shamban wakutane Twitter na JF.
 
Pamoja na kutegemea reli, bara bara zetu ni nzuri kwa sasa ni bora. Kukiwa na ma Lori makubwa ya kutoa nyanya Iringa Jumamosi na zile sokoni J2 au makebichi ya Tukuyu yafike Mwanza kesho yake hii chain itazalisha ajira.

Tatizo Lipo kwenye uwajibikaji.

Anaweza kutokea kiongoz akataka magu is yake 10 yasafiri bure bila kuelewa kuwa kwa kufanya vile anaua biashara ya lori.
Dereva atapakia mizigo ya ziada apate cha juu.

Tunahitaji kuwa na self discipline na dereva aelewe akibainima ana pore za ajira na mafao yake.
 
Mzizi wa tatizo ni uduni wa elimu. Hilo ndilo linafanya kila kitu watu wasubiri serikali. Serikali inasubiriwa kutafuta masoko! Serikali imefanywa baba, mama na mjomba!

Kenya na Ethiopia wanauza sana maua na mazao ya bustanini Ulaya. Ni serikali inawatafutia masoko? Hapana. Mtu aliyeelimika vizuri anatumia nyenzo za mitandao kujifanyia utafiti na hata kuwasiliana na wahitaji wa mazao anayopanga kulima.

Kijana mwenye elimu pana ya kawaida akiamua kulima mbogamboga hatasubiri serikali imfundishe afanyeje. Atatumia Wikipedia na websites nyingine kujifundisha.

Kuanzia uhuru mpaka miaka ya tisini, kiasi cha bajeti ya Tanzania kwenye elimu kilishuka toka asilimia 20 hadi asilimia 4.9. Kenya kilibaki asilimia 20 na kuongezeka hadi 25.

Tuanze upya. Tuache mzaha kwenye elimu. Bila elimu hatutaweza kutatua matatizo mengine.
Hivi unaanzaje kuuza mazao nje bila support ya serikali. Kwa point yako hapo juu ningehoji kazi ya serikali kwa wakulima wa ndani, mara ngapi serikali inapiga marufuku uuzwaji wa mazao nje!?.
 
Kila kiongozi anakuja na sera yake ,yuko wa kilimo kwanza ,yuko wa Viwanda. Nchi ishike lipi sasa!!


Note ili nchi iendelee vyema katika nyanja zote inatakiwa iwe na sekta imara ya kilimo ,hili halipingiki hata kidogo . Refer uingereza ilianza mapunduzi kwenye kilimo kwanza


Kuna eneo Mbeya ukiwa unaelekea tukuyu kabichi nne kubwa ni 1000 na ziko trari kwenye mfuko ,hapo jiulize mkulima anapata nini?


Kilimo kikiboreshwa kitachukua vijana wengi ambao hawana ajira huku mtaani .

Vijana wanajitahid sana kulima ,changamoto hawana ujuzi wa ku-marketing mazao yao hapo ndipo wafanya biashara wanapo waliza wakulima

Serekali ina jukumu la kuhakikisha kuna pembejeo bora kwa wakulima kwa bei nafuu ,hata ikiwezekana kwa mkopo


Serekali pia inatakiwa wakti mwingine ipange bei kwenye baadhi ya mazao kuhakikisha mkulima ananufaika vyema.


Itoe ruzuku pia kwa wakulima .


Itafute masoko ya njee na ndani ya nchi

Iwe na sera nzuri zitakazo wavutia vijana kujiingiza kwenye kilimo

Ku- technologizes vijiji vijana wakitoka shamban wakutane Twitter na JF.

Sirikali imetoa milioni hamsini (50million/=) kila kijiji mmezifanyia nini?
Tuanzie hapo kwanza.
 
Ushauri :
1. Kutafuta soko la ndani na nje. Jinsi tutakavyoweza kusafirisha local products national wide.

2. Jinsi ya kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa wanaotaka kuanzisha kilimo cha biashara

3. Kuleta simple farming tools, kusema ukweli kilimo cha jembe la mkono kimepitwa na wakati.
Ushauri :
1. Kutafuta soko la ndani na nje. Jinsi tutakavyoweza kusafirisha local products national wide.

2. Jinsi ya kutoa mafunzo ya kilimo bora kwa wanaotaka kuanzisha kilimo cha biashara

3. Kuleta simple farming tools, kusema ukweli kilimo cha jembe la mkono kimepitwa na wakati.

4. Tatizo lingine walimu wanaofundisha masomo ya mifugo na kilimo wanatumia akili za miaka ya 1980 kufundisha miaka hii ya 2019.

5. Lingine walimu wanaofundisha masomo ya mifugo na kilimo wao wenyewe unakuta hawalimi wala kufuga hata njiwa.

6. Tatizo lingine ni kuwa na mbadiliko wa mawazo{Mindset}¶

7. Lingine watunga sera, wengi hawana uelewa ktk Maswala ya aridhi, mifugo na kilimo. Mfano mnauona Kati ya wafugaji na wakulima kugombania aridhi na wakati aridhi ni kubwa ila haijapangiwa matumizi vizuri..

8. Kingine vijana hawaaminiwi na serikali pamoja na wazazi ktk kujihusisha na Maswala ya kiuchumi. Wahindi na waarabu kijana akifika miaka 18 upewa majukumu ya kukikwamua kiuchumi tofauti na waafrika.
 
Mkuu vijana wana kosa soko la nyanya zinaozea shambani au kuuza kwa bahati sh 200 kwa ndoo ya litre 5.

Tuko hapa kubadilishana mawazo ikiwamo jinsi ya kusafirisha perishable products
Ser mbovu sana, zinafanya mzunguko ktk kilimo na mifugo kuwa ngumu. Kama Serikali inapiga danadana ktk kuwasaidia wafugaji na wakulima
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom