Apson: The Beginning of TISS's Failure

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Tunapozungumzia idara ya Usalama wa Taifa na jinsi imeiangusha serikali yetu na kuweka usalama wa taifa letu hatarini nafasi ya Bw. Apson Mwang'onda haiwezi kupuuzwa. Baadhi ya matukio yaliyotokea na kuruhusu ufisadi nchini yalitokea wakati wa "ulinzi" wake na hatujui ni kwa kiasi gani alisimamia idara hiyo katika Usalama wa Taifa.

Wakati umefika na huyu naye ajibu, alifanya nini kuiimarisha idara hiyo na kuhakikisha inajijenga sawasawa kukabiri matishio ya ulimwengu wa utanda wazi?

Kwa vile Rada ilinunuliwa wakati wa uongozi wake wananchi wana haki ya kujua ni kwa kiasi gani idara yake ilishiriki katika kuhalalisha mauzo ya kurushwa kwa Vithlani? Zaidi ya yote binafsi ningependa kujua mambo yafuatayo kuhusu idara ya TISS enzi za Apson:

a. Walijua nini kuhusu Saileth Vithlani yule Dalali aliyetoweka kwa kupanda ndege baada ya kuwaaga?
b. Idara ya Usalama wa Taifa ilijua nini kuhusu Jeetu Patel na uanzishaji wa banki ya Azania wakati Bw. Patel alishawahi kufilisi moja ya makampuni yake na sheria ya Fedha ilikuwa hairuhusu mtu aliyefilisiwa kuingia katika sekta ya Fedha? Kwanini Patel alipewa exception?
c. Apson alijua nini kuhusu kitendo cha Rais Mkapa na Waziri wake wa Nishati kutumia vyeo vyao kujinufaisha na kujigawia mgodi wa Kiwira?

Je yawezekana matatizo yetu mengi ya kiusalama yametokana na uongozi wa ndugu huyu na wakati wake wa kujibu umefika ili kina RO wajifunze kutokana na makosa?
 
Huyu jamaa amekuwa tajiri wa kupindukia katika muda mfupi sana. Haijulikani alikuwa anafanya biashara gani iliyomwezesha kuwa tajiri mkubwa kiasi hicho. Kuna haja ya kuangalia utajiri wake umepatikanaje, isije ikawa alikuwa kwenye timu moja na akina fisadi Mkapa na fisadi Chenge katika mipango yao ya kuifisadi Tanzania.
 
Huyu jamaa amekuwa tajiri wa kupindukia katika muda mfupi sana. Haijulikani alikuwa anafanya biashara gani iliyomwezesha kuwa tajiri mkubwa kiasi hicho. Kuna haja ya kuangalia utajiri wake umepatikanaje isije ikawa alikuwa kwenye timu moja na akina fisadi Mkapa na fisadi Chenge katika mipango yao ya kuifisadi Tanzania.
Mie nafikiri naye tumjumuishe katika kwenda kuchukua faili lake katika tume ya maadili ili tujue kama malia laizonazo na kipindi alichotumika zilipatikana kihalali??
 
Mbona mnasema ana utajiri, kuna mifano yoyote; mimi swali langu is theoretical sijui lolote. Nimeangalia kwenye suala la TISS tu lakini naona watu wanajua yawezekana there is more than what meet the eyes!!
 
Mafaili ya Mramba, Karamagi, Magufuli, Apson, Chenge, Mkapa, Ballali, Meghji, Mzindakaya, Mkono, Yona na wengine wote waliotajwa pale mwembe yanga na Slaa yaangaliwe ili kujua ni mali zipi walizoorodhesha.
 
Mwanakijiji,

Nafikiri turudi nyuma kidogo. Tuanze kuipembua TISS na wakurugenzi wake kuanzia mwaka 1990.

Kumbuka kuwa tangu mwaka 1990, kulianza lilea wimbi la kutka uwajibikaji, lakini hakuna hatu amadhubuti zilitokea. Pia kuanza kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya.

Likaja Azimio la Zanzibar na kuundwa kwa vyama vingi kuanzia 1992, je Usalama walifanya nini na walihusika vipi?

Turudi nyuma ili tuweze pata picha kamili ya jinsi gani Usalama wa Taifa ama ulishindwa kufanya kazi za kuilinda nchi yetu kwa kila kitu na hizi hisia kuwa Usalama ni kitengo maalum cha CCM na Mafisadi.

Ikibidi inawezekana tubadili kichwa cha thread na kuwa upembuzi wa UWT 1990-2008!
 
Jamani APSON kafanya kufuru alipokuwa mkurugenzi wa Usalama ni tajiri kupita kiasi na bahati mbaya ameweka vijana wengi toka kabila la watu wa Mbeya kwenye usalama wa Taifa hii ni hatari sana kwa Taifa.

alijipatia tenda ya kujenga ukuta wa Ikulu kwa mamilio ya pesa za wananchi wakati wa MKAPA.

hivi sasa ameanzisha task force yake kuona anapatikana rais toka nyanda za juu za kusini next term.

yupo karibu sana na Luhanjo kiasi ya kwamba appointment nyingi zinakwenda kusini, kuna jamaa anaitwa Sanga kapewa Ukurugenzi kwenye LAPF mfuko mkubwa sana wa jamii na huyu Sanga alishawahi kuwa demoted kwa uifisadi.

Membe ana kazi kubwa kwani watu wa kusini wamejuinga pamoja na kuzika tofauti zao na kuhakikisha Mwandosya anakwaa urais.
kundi la kusini lina team kubwa wakiwepo kina Mwamnyange na Mboma, Mwakyembe n.k

ipo haja kutizama file la APSON.
 
Mwanakijiji,

Nafikiri turudi nyuma kidogo. Tuanze kuipembua TISS na wakurugenzi wake kuanzia mwaka 1990.

Kumbuka kuwa tangu mwaka 1990, kulianza lilea wimbi la kutka uwajibikaji, lakini hakuna hatu amadhubuti zilitokea. Pia kuanza kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya.

Likaja Azimio la Zanzibar na kuundwa kwa vyama vingi kuanzia 1992, je Usalama walifanya nini na walihusika vipi?

Turudi nyuma ili tuweze pata picha kamili ya jinsi gani Usalama wa Taifa ama ulishindwa kufanya kazi za kuilinda nchi yetu kwa kila kitu na hizi hisia kuwa Usalama ni kitengo maalum cha CCM na Mafisadi.

Ikibidi inawezekana tubadili kichwa cha thread na kuwa upembuzi wa UWT 1990-2008!

Rev nakubaliana na wewe...kuanzia kipindi hicho ndipo tumeshuudia miradi mingi ya TISS ikifa mmoja baada ya mwingine...na ufisadi wa aina nyingi.
 
Jamani APSON kafanya kufuru alipokuwa mkurugenzi wa Usalama ni tajiri kupita kiasi na bahati mbaya ameweka vijana wengi toka kabila la watu wa Mbeya kwenye usalama wa Taifa hii ni hatari sana kwa Taifa.

alijipatia tenda ya kujenga ukuta wa Ikulu kwa mamilio ya pesa za wananchi wakati wa MKAPA.

hivi sasa ameanzisha task force yake kuona anapatikana rais toka nyanda za juu za kusini next term.

yupo karibu sana na Luhanjo kiasi ya kwamba appointment nyingi zinakwenda kusini, kuna jamaa anaitwa Sanga kapewa Ukurugenzi kwenye LAPF mfuko mkubwa sana wa jamii na huyu Sanga alishawahi kuwa demoted kwa uifisadi.

Membe ana kazi kubwa kwani watu wa kusini wamejuinga pamoja na kuzika tofauti zao na kuhakikisha Mwandosya anakwaa urais.
kundi la kusini lina team kubwa wakiwepo kina Mwamnyange na Mboma, Mwakyembe n.k

ipo haja kutizama file la APSON.

Kwi kwi kwi!!!! Wakati mwingine JF mnachekesha kweli kweli.

Wacha nijaribu kuweka facts ninazozijua:

Ni kweli Mwang'onda ni mtu wa Mbeya kwa jina. Nasema kwa jina kwasababu
Apson alikuwa na uhusiano mdogo sana na mkoa wa Mbeya. Yeye kwa jina kwa muda mrefu anajulikana kama Apson Cornel, alizaliwa Tabora kwa baba toka Kyela, Mbeya na mama Mnyamwezi.

Babake Apson alienda Tabora kwenye mashamba ya Tumbaku akiwa kijana na hakurudi tena Kyela. Hata alipofariki alizikwa huko huko Tabora.

Apson alifika Kyela kwa mara ya kwanza akiwa ni mtu mkubwa. Kyela alikuta ukoo wake wote umeisha na alimkuta shangazi yake tu na akamchukua na kumjengea Mbozi.

Ameanza kujihusisha na mambo ya Mbeya hasa baada ya kuwa mkubwa hapo usalama wa taifa, ndio akaanza kujichanganya zaidi na zaidi na watu wa kwao.

Yeye makazi yake sasa ni Mbozi ambako ana shamba kubwa la kahawa nafikiri na mahindi. Kyela ana nyumba tu na biashara na rafiki zake wakiwemo mkuu wa mkoa na wale vigogo wa zamani wa jeshi la polisi.

Sasa hapo ndipo usemi wa kwamba kajaza watu wa Mbeya, napata kigugumizi kuuamini.

Tukija kwenye urais 2010. Apson alifanya double act, huku alikuwa anonyesha anamuunga Malecela kumbe kichini chini anamuunga Muungwana. Hakuwa na uhusiano kabisa na Mwandosya na mpaka sasa yeye ni kundi moja na Mwakipesile, mkuu wa mkoa wa Mbeya. Ondoa kabisa wazo la Mwakyembe na Apson, hayo ni makundi mawili ambayo ni paka na panya. Kwa taarifa tu hata
biashaya ya akina Apson pale Kyela ambayo ni hotel ya maana inaitwa Kyela Resort, Mwakyembe yuko tayari kwenda kulala nje kuliko kulala pale.

Hapo kwa mara nyingine naona facts zako sio sahihi. Mkuu usitulishe sumu, wakati waungwana wa JF wanajua ni sumu.

Hata jina la Mwang'onda kaanza kulitumia sasa labda kama njia ya kumsaidia Thom ili akubalike pale Mbeya mjini.

Hizo appointments nyingi zinatoka wapi wakati yeye sio mkurugenzi tena?

Acheni kuendeleza mambo ya ukabila hata mahali ambapo hakuna facts zozote zinazoonyesha kuna ukabila.

Hayo ya Mwamunyange siku nyingine, ila huyo mkulu hata watu wa Mbeya wanamwogopa, haingiliki, sasa mbona unataka naye kumhusisha na ukabila?

Yaani mtu akiitwa Mwa... tayari ni mkabila?
 
Nafikiri hata CCM wenyewe hawatapenda kumsimamisha mtu kama Mwandosya maana wanajua kabisa ana kashifa inanukia ya kujilimbikizi mamilioni wakati wa ununuzi wa rada na ndege ya raisi kwahiyo nafikiri mwandosya asahau swala la uraisi. hata kama wasingekuwa na ugomvi na mwakyembe.
 
na sisi wananchi tangu kipindi hicho tulikua tunafanya nini ku-address if not acting agaisnt ufisadi!?

Ule usiri uliopo kwenye uendeshaji wa idara hii nadhani unawaogofya wengi kwenda kutoa habari muhimu. Kama unaikumbuka ile ofisi ya pale station kabla haijaamishwa ndio ilikuwa sehemu ya wananchi kwenda kutoa taarifa wanazohisi zina utata...Guess what katika pita pita yangu eneo lile nilikuwa naona mlango uko wazi tuu lakini sijawahi kuona mtu anaingia wala kutoka.

Apson aliichukua uongozi wa idara wakati ikiwa imeachwa hoi na marehemu...kwa kiasi fulani alijaribu kurudisha heshima yake na kufanya changes kadhaa kuiboresha lakini as usual politics zikaingizwa the rest ndio haya tunayoyajadili kila kukicha.
 
Ule usiri uliopo kwenye uendeshaji wa idara hii nadhani unawaogofya wengi kwenda kutoa habari muhimu. Kama unaikumbuka ile ofisi ya pale station kabla haijaamishwa ndio ilikuwa sehemu ya wananchi kwenda kutoa taarifa wanazohisi zina utata...Guess what katika pita pita yangu eneo lile nilikuwa naona mlango uko wazi tuu lakini sijawahi kuona mtu anaingia wala kutoka.

Apson aliichukua uongozi wa idara wakati ikiwa imeachwa hoi na marehemu...kwa kiasi fulani alijaribu kurudisha heshima yake na kufanya changes kadhaa kuiboresha lakini as usual politics zikaingizwa the rest ndio haya tunayoyajadili kila kukicha.

Icadon, si hata pale St. Peters, Makaburini na Kijitonyama watu walikuwa wanaogopa hata kufungua midomo kwa woga?

Hata kama ungeingia anga zao kwa bahati mbaya, walikuwa wanasifika kwa kutoa kibano.

Mimi mwaka juzi nikiwa DC nilikosea njia nikaingia Pentagon, ikabdi niende getini na kuomba wanielekeze njia. Ingekuwa ni Dar iwe TISS, Lugalo au Makao Makuu jeshini, mngekuja nitembelea Muhimbili!

TISS wametawala nchi kwa kutumia vitisho, inabidi wabadili mentality hiyo!
 
Icadon, si hata pale St. Peters, Makaburini na Kijitonyama watu walikuwa wanaogopa hata kufungua midomo kwa woga?

Hata kama ungeingia anga zao kwa bahati mbaya, walikuwa wanasifika kwa kutoa kibano.

Mimi mwaka juzi nikiwa DC nilikosea njia nikaingia Pentagon, ikabdi niende getini na kuomba wanielekeze njia. Ingekuwa ni Dar iwe TISS, Lugalo au Makao Makuu jeshini, mngekuja nitembelea Muhimbili!

TISS wametawala nchi kwa kutumia vitisho, inabidi wabadili mentality hiyo!

DC na Northern Virginia hakufai kabisa....
Siku hizi pale St Peters wamekata kata miti ata jengo lenyewe linaonekana na kale kabarabara wamekawekea lami unakatiza tuu mbele ya jengo hawana noma sana sema ukisogelea geti ndio unaweza kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda.

Anwyays ofisi ya station iko chini ya kitengo cha usalama wa ndani, walikuwa wanakaribisha wananchi wote kwenda pale kutoa mawazo yao..siku hizi wameihamishia kule sea view.
 
Back
Top Bottom