Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,367
Wadau, amani iwe kwenu.
Jina Apson Mwang'onda si geni kwenye mitandao ya kijamii. Umaarufu wake haukutokana na utendaji kazi wake akiwa kwenye idara nyeti hapa nchini, la hasha. Umaarufu wake haukuonekana akiwa Mkuu wa Idara nyeti bali umeanza kujitokeza miaka miwili kabla ya Tanzania kuingia kwenye uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015.
Awali ilikuwa kama fununu tu lakini baadaye ikadhihirika kuwa nzi huyo alikuwa akiruka huku na kule kuhakikisha kuwa anaweka watu ambao wataendeleza mfumo mbovu wa kifisadi ndani ya CCM na Tanzania kwa ujumla. Hapana shaka kwamba Watanzania bado wana imani na CCM isipokuwa walichoshwa na aina ya mfumo uliotengenezwa na baadhi ya watu ambao walikuwa wanatumia fedha nyingi kupata viongozi. Matokeo yake CCM ikaanza kupoteza mwelekeo kwa vile wale wafadhili wa mfumo huo ndio waliokuwa wanaendesha chama na serikali.
Mapinduzi yaliyofanywa ndani ya chama mwaka 2007 na kusababisha baadhi ya watu kujivua magamba huku wengine wakikaidi kufanya hivyo ndiyo yaliyomshtua Apson. Apson alishtuka hasa baada ya marafiki wake wakuu ambao ni Rostam Aziz, Edward Lowasa, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na wengineo ndio waliotakiwa kujivua hayo magamba. Naam, Rostam alijivua gamba ila Lowasa akashindwa kufanya hivyo kwa ushauri wa Apson. Apson aliona kuwa ikiwa Lowasa atajivua gamba, ndoto yake ya kwenda Ikulu itakuwa imeyeyuka. Hivyo akamshauri kuwa akomae na hivyo kujikuta akisakamwa mara kwa mara na watetezi wa chama na waliochoshwa na siasa chafu ndani ya chama hicho kama vijana machachari Nape Nnauye, Paul Makonda pamoja na Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti Philip Mangula.
Ili kuonesha kuwa Apson alikusudia kumuweka mtu wake ambaye atalinda maslahi yake kutokana na ukwapuzi aliofanya akiwa Mkurugenzi ndani ya Idara hiyo, nyumba yake ndiyo iliyokuwa inatumika kufanya vikao vya kuratibu mkakati wa Lowasa kwenda Ikulu. Kama hiyo haitoshi, yeye mwenyewe akajipachika cheo cha Mwenyekiti wa Kamati ya Wezesha Lowasa aende Ikulu.
Nyumba ya Apson pamoja na Hotel ya Sea Cliff ya Dar es Salaam ndio mahala palipokuwa panatumika kupanga mikakati yote ovu pamoja na kupeana mabulungutu ya fedha ambazo zilikuwa zinatumika kuwarubuni wajumbe wa vyombo vya maamuzi ndani ya CCM kama vile wajumbe wa Halmashauri Kuu, Kamati Kuu, Sekretarieti na Mkutano Mkuu. Pia maburungutu hayo yalitumika kuhonga baadhi ya viongozi wa dini ili watumie nyumba za ibada kumnadi mwanasiasa huyo. Habari zote hizi zilikuwa zinaripotiwa humu na vijana waliojitolea kupambana na mafisadi ijapokuwa wapo waliokuwa wanabeza ukweli wa taarifa hizo.
Baada ya mkakati wa Apson ndani ya CCM kukwama na Lowasa kuchinjiwa baharini wakati wa mchujo wa kumpata mgombea Urais ndani ya chama hicho, alimshauri ahamie upinzani. Lowasa bila ya kutafakari madhara yake aliamua kujitosa mzima mzima. Mikakati ya Apson baada ya Lowasa kuhamia upinzani ilikuwa kuhakikisha wanafanikiwa kurubuni Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili waweze kuchakachua matokeo. Wapo baadhi ya Wakurugenzi wa Tume hiyo ambao waliingia kwenye majaribu ya Apson. Mfano halisi ni Mkurugenzi wa IT ambaye alitengewa burungutu kubwa.
Hata hivyo, mkakati huo ulikwama baada ya Mkurugenzi huyo kusimamishwa kutokana na ubadhilifu mkubwa aliofanya wakati wa ununuzi wa mashine za BVR. Apson likamshuka. Maji yakamfika shingoni. Hata hivyo hakukata tamaa. Akaingia mkenge kwa kusaka vijana wenye weledi na masuala ya IT kutoka ndani na nje ya nchi. Wakafanikiwa kuwapata vijana hao wengi kutoka Tanzania na wengine wakitoka Kenya, Ufaransa, Marekani, Canada na Korea.
Wataalam hao wa IT kwa maelekezo ya Apson wakafanikiwa kuhack mfumo wa Tume na wakafanikiwa kuingiza data zao ili kumbeba Lowasa. Pia data hizo ziliwabeba baadhi ya wabunge wa Dar es Salaam kama Halima Mdee, Saed Kubenea na John Mnyika.
Mungu si Athuman. Wasamaria wema wakatoa taarifa polisi kuwa kuna vijana ambao hawaeleweki wapo kwenye hoteli kadhaa Dar es Salaam hasa maeneo ya Sinza, Kijitonyama na Masaki. Taarifa hizo ndizo zilizofanikisha kukamatwa kwa vijana wale 191 wakiwa na laptop na simu zinazofanana. Wakatiwa nguvuni na vitendea kazi vyao kutaifishwa.
Baada ya hapo mchezo ukamalizika. Hakika Lowasa, Apson na genge lake wameumia sana kukamatwa kwa wale vijana maana ndio lilikuwa tegemeo lao la mwisho. Kutokana na kukamatwa kwa vijana wale, matakwa halisi ya wananchi yakaanza kujionesha baada ya Magufuli kushinda katika maeneo mengi hata yale ngome ya UKAWA.
Kwa sasa Apson na genge lake wanajuuta kwa upuuzi waliofanya. Hawajui wafanye nini. Lowasa amenuna. Rostam kawakasirikia kwa vile wamekula fedha zake nyingi bila ya mafanikio. Na nasikia kuwa ameapa kula nao sahani moja kwa hasara waliyomsababishia.
Hakika Mungu alikuwa na mpango wake kwa Watanzania. Tumempata Rais ambaye alikuwa anapambana na watu ambao walijiequip kwa kila hali.
Jina Apson Mwang'onda si geni kwenye mitandao ya kijamii. Umaarufu wake haukutokana na utendaji kazi wake akiwa kwenye idara nyeti hapa nchini, la hasha. Umaarufu wake haukuonekana akiwa Mkuu wa Idara nyeti bali umeanza kujitokeza miaka miwili kabla ya Tanzania kuingia kwenye uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015.
Awali ilikuwa kama fununu tu lakini baadaye ikadhihirika kuwa nzi huyo alikuwa akiruka huku na kule kuhakikisha kuwa anaweka watu ambao wataendeleza mfumo mbovu wa kifisadi ndani ya CCM na Tanzania kwa ujumla. Hapana shaka kwamba Watanzania bado wana imani na CCM isipokuwa walichoshwa na aina ya mfumo uliotengenezwa na baadhi ya watu ambao walikuwa wanatumia fedha nyingi kupata viongozi. Matokeo yake CCM ikaanza kupoteza mwelekeo kwa vile wale wafadhili wa mfumo huo ndio waliokuwa wanaendesha chama na serikali.
Mapinduzi yaliyofanywa ndani ya chama mwaka 2007 na kusababisha baadhi ya watu kujivua magamba huku wengine wakikaidi kufanya hivyo ndiyo yaliyomshtua Apson. Apson alishtuka hasa baada ya marafiki wake wakuu ambao ni Rostam Aziz, Edward Lowasa, Nazir Karamagi, Andrew Chenge na wengineo ndio waliotakiwa kujivua hayo magamba. Naam, Rostam alijivua gamba ila Lowasa akashindwa kufanya hivyo kwa ushauri wa Apson. Apson aliona kuwa ikiwa Lowasa atajivua gamba, ndoto yake ya kwenda Ikulu itakuwa imeyeyuka. Hivyo akamshauri kuwa akomae na hivyo kujikuta akisakamwa mara kwa mara na watetezi wa chama na waliochoshwa na siasa chafu ndani ya chama hicho kama vijana machachari Nape Nnauye, Paul Makonda pamoja na Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti Philip Mangula.
Ili kuonesha kuwa Apson alikusudia kumuweka mtu wake ambaye atalinda maslahi yake kutokana na ukwapuzi aliofanya akiwa Mkurugenzi ndani ya Idara hiyo, nyumba yake ndiyo iliyokuwa inatumika kufanya vikao vya kuratibu mkakati wa Lowasa kwenda Ikulu. Kama hiyo haitoshi, yeye mwenyewe akajipachika cheo cha Mwenyekiti wa Kamati ya Wezesha Lowasa aende Ikulu.
Nyumba ya Apson pamoja na Hotel ya Sea Cliff ya Dar es Salaam ndio mahala palipokuwa panatumika kupanga mikakati yote ovu pamoja na kupeana mabulungutu ya fedha ambazo zilikuwa zinatumika kuwarubuni wajumbe wa vyombo vya maamuzi ndani ya CCM kama vile wajumbe wa Halmashauri Kuu, Kamati Kuu, Sekretarieti na Mkutano Mkuu. Pia maburungutu hayo yalitumika kuhonga baadhi ya viongozi wa dini ili watumie nyumba za ibada kumnadi mwanasiasa huyo. Habari zote hizi zilikuwa zinaripotiwa humu na vijana waliojitolea kupambana na mafisadi ijapokuwa wapo waliokuwa wanabeza ukweli wa taarifa hizo.
Baada ya mkakati wa Apson ndani ya CCM kukwama na Lowasa kuchinjiwa baharini wakati wa mchujo wa kumpata mgombea Urais ndani ya chama hicho, alimshauri ahamie upinzani. Lowasa bila ya kutafakari madhara yake aliamua kujitosa mzima mzima. Mikakati ya Apson baada ya Lowasa kuhamia upinzani ilikuwa kuhakikisha wanafanikiwa kurubuni Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili waweze kuchakachua matokeo. Wapo baadhi ya Wakurugenzi wa Tume hiyo ambao waliingia kwenye majaribu ya Apson. Mfano halisi ni Mkurugenzi wa IT ambaye alitengewa burungutu kubwa.
Hata hivyo, mkakati huo ulikwama baada ya Mkurugenzi huyo kusimamishwa kutokana na ubadhilifu mkubwa aliofanya wakati wa ununuzi wa mashine za BVR. Apson likamshuka. Maji yakamfika shingoni. Hata hivyo hakukata tamaa. Akaingia mkenge kwa kusaka vijana wenye weledi na masuala ya IT kutoka ndani na nje ya nchi. Wakafanikiwa kuwapata vijana hao wengi kutoka Tanzania na wengine wakitoka Kenya, Ufaransa, Marekani, Canada na Korea.
Wataalam hao wa IT kwa maelekezo ya Apson wakafanikiwa kuhack mfumo wa Tume na wakafanikiwa kuingiza data zao ili kumbeba Lowasa. Pia data hizo ziliwabeba baadhi ya wabunge wa Dar es Salaam kama Halima Mdee, Saed Kubenea na John Mnyika.
Mungu si Athuman. Wasamaria wema wakatoa taarifa polisi kuwa kuna vijana ambao hawaeleweki wapo kwenye hoteli kadhaa Dar es Salaam hasa maeneo ya Sinza, Kijitonyama na Masaki. Taarifa hizo ndizo zilizofanikisha kukamatwa kwa vijana wale 191 wakiwa na laptop na simu zinazofanana. Wakatiwa nguvuni na vitendea kazi vyao kutaifishwa.
Baada ya hapo mchezo ukamalizika. Hakika Lowasa, Apson na genge lake wameumia sana kukamatwa kwa wale vijana maana ndio lilikuwa tegemeo lao la mwisho. Kutokana na kukamatwa kwa vijana wale, matakwa halisi ya wananchi yakaanza kujionesha baada ya Magufuli kushinda katika maeneo mengi hata yale ngome ya UKAWA.
Kwa sasa Apson na genge lake wanajuuta kwa upuuzi waliofanya. Hawajui wafanye nini. Lowasa amenuna. Rostam kawakasirikia kwa vile wamekula fedha zake nyingi bila ya mafanikio. Na nasikia kuwa ameapa kula nao sahani moja kwa hasara waliyomsababishia.
Hakika Mungu alikuwa na mpango wake kwa Watanzania. Tumempata Rais ambaye alikuwa anapambana na watu ambao walijiequip kwa kila hali.