Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,827
- 3,568
Wamekosea sana kumpeleka kuhojiwa kwenye kamati za vitisho na polisi kwa sababu huko ataibuka mshindi tu kwani hawataweza kujibu hoja zake. Na kwa kuwa wameshamtisha na akaonyesha ushupavu wa kutotishika atazidi kuwa maarufu.
Na wakikosea zaidi wakamuumiza popote, au hata wakimfukuza ubunge, basi hata wale ambao walikuwa hawamwamini watamwamini kwa kigezo cha kwamba serikali inatumia nguvu kulazimisha jambo ovu ndio maana hata anayelipinga wanamsulubu. Atajipatia "ushujaa" kutoka kwa kundi kubwa kuliko awali.
Kwa maoni yangu, approach sahihi kwa issue ya Gwajima kupinga chanjo ya COVID, wangempa nafasi ya kujadiliana na wataalamu wa tiba, siyo na wanasiasa. Wamruhusu kuja na wataalamu wake wanaompa hayo maelezo anayoona kuwa ni ya kitaalamu.
Wampe nafasi ya kumsikia hoja zake zote na aweke mezani evidence zote anazoona zinasupport msimamo wake, kisha watoe nafasi kwa wataalamu kuzijibu huku nao wakiweka evidence zao mezani.
Watoe fursa ya mdahalo kati ya Gwajima na wataalam wake dhidi ya serikali na wataalamu wake, mjadala uwe wa kisayansi, evidence based.
Naamini watafikia muafaka. Akishaelewa anapokosea au alipopotoshwa na 'wataalam' wake, yeye mwenyewe atarudi kwa waumini wake aseme maswali yetu yote yameshajibiwa, nimejiridhisha kuwa chanjo ni salama, nendeni mkachanjwe.
Na wakikosea zaidi wakamuumiza popote, au hata wakimfukuza ubunge, basi hata wale ambao walikuwa hawamwamini watamwamini kwa kigezo cha kwamba serikali inatumia nguvu kulazimisha jambo ovu ndio maana hata anayelipinga wanamsulubu. Atajipatia "ushujaa" kutoka kwa kundi kubwa kuliko awali.
Kwa maoni yangu, approach sahihi kwa issue ya Gwajima kupinga chanjo ya COVID, wangempa nafasi ya kujadiliana na wataalamu wa tiba, siyo na wanasiasa. Wamruhusu kuja na wataalamu wake wanaompa hayo maelezo anayoona kuwa ni ya kitaalamu.
Wampe nafasi ya kumsikia hoja zake zote na aweke mezani evidence zote anazoona zinasupport msimamo wake, kisha watoe nafasi kwa wataalamu kuzijibu huku nao wakiweka evidence zao mezani.
Watoe fursa ya mdahalo kati ya Gwajima na wataalam wake dhidi ya serikali na wataalamu wake, mjadala uwe wa kisayansi, evidence based.
Naamini watafikia muafaka. Akishaelewa anapokosea au alipopotoshwa na 'wataalam' wake, yeye mwenyewe atarudi kwa waumini wake aseme maswali yetu yote yameshajibiwa, nimejiridhisha kuwa chanjo ni salama, nendeni mkachanjwe.