Mkuu, tunaomba uthibitishe haya uliyoyasema. Vinginevyo tutachukulia kama mtu mwenye nia ya kuharibu brand ya JamiiForums kama taasisi na kumchafua Mwanzilishi wa JamiiForums mbele ya Jamii na Jumuia za Kimataifa.Unfortunately; kwa wale wa siku nyingi, huko nyuma tulikuwa na moderators ambao walikuwa very objective lakini siku hizi naona kuna moderators MUBYAZI kawaleta wanaoelekea kama watu wa KITENGO vile.!
Nyuzi ambazo zinakosoa serikali/ccm kwa nia nzuri ndizo zinazohamishwa na kupotezwa!!! Hii inaipunguzia hadhi yake JF. Hao watu wa kitengo wameinfiltrate ili kupata identity ya members but I believe Mubyazi analilinda hilo.
Tuomba Uthibitishe hao Moderators walioletwa kutoka kitengo ili kuchukua Identity za Watu. Kama utashindwa kuthibitisha, uachie uhuru Sheria za JamiiForums zichukue Mkondo wake.
Sheria uliyovunja ipo hapa: https://www.jamiiforums.com/threads...mwongozo-wa-ushiriki-kwenye-mijadala.1753332/
Pili, tutajie hizo nyuzi unazodai zinakosoa Serikali au CCM kupotezwa. Mfano hii thread inasifia Serikali? Ina muda gani na kwanini haipotezwi, au michango ndani yake kwanini haipotezwi. Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea
Nimeanza kuichukia CCM rasmi baada ya Serikali kuanza kuwatia ndani ndugu zangu kisa hawana pesa ya kuchangia ujenzi wa shule
Nimekerwa sana na watendaji wa Serikali huko Shinyanga hususani wilaya ya Kishapu kuanzisha michango mikubwa, ndani ya wiki mbili mkulima analazimishwa kutoa elfu 70. Mheshimiwa Rais hivi ni kweli hii ni agizo lako? Maana wanasema ni maagizo kutoka juu. Kama ndivyo ilivyo, Mimi kuanzia Leo...
www.jamiiforums.com
Serikali ya CCM haifurahi ukiwa na kiasi kikubwa cha fedha benki, unafilisiwa kwa kupewa kesi ya Uhujumu Uchumi
Salaam Wakuu, Nmeanza kuelewa kwanini Matajiri wengi wa Tanzania wanaficha fedha zao nje ya Nchi. Siwalaumu tena. Na kama hii hali ikiendelea, Benki nyingi zitatikisika kiuchumi kwani watu watasusa kupeleka hela. Zamani Watanzania wengi walikuwa hawapeleki fedha zao benki. Walikuwa...
www.jamiiforums.com
Uchaguzi 2020 - Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani
Leo Novemba 25, 2020 katibu mkuu wa CHADEMA amezungumza na vyombo vya habari makao makuu ya chama hicho eneo la Ufipa, Kinondoni mada kuu ikiwa uteuzi wa wabunge wa viti maalum ambapo uapisho wao ulifanyika jana bungeni jijini Dodoma jana. Yafuatayo ni maelezo kwenye mkutano huo kuanzia mwanzo...
www.jamiiforums.com
Uchaguzi 2020 - Viongozi wa taasisi kama Polisi na NEC kuibeba CCM dhidi ya vyama vya upinzani ni kuelewa kwamba wapinzani wakichukua serikali wataondolewa vyeo vyao
Wala sio hesabu ngumu. Ni wazi sana kwamba taasisi kama Polisi na NEC mara kwa mara zinafanya ukosefu mkubwa wa usawa dhidi ya vyama vya upinzani. Umewahi kujiuliza kwa nini? Sababu ni moja, viongozi wa taasisi hizi wanajua wazi kwamba Upinzani ukichukua serikali wataondolewa madarakani...
www.jamiiforums.com
Ubungo Interchange ni ushahidi kwamba bado Serikali ya CCM haifanyi kazi kwa ufanisi
Habari za wakati huu; Nimeandika uzi huu ili kumpa jibu la herufi kubwa kaka yangu mheshimiwa wakili msomi Paskali ambaye pia alikuwa Mtia nia Ubunge Jimbo la Kawe. Kwanza kabisa nimesikitishwa kwa msomi kama yeye kutuambia kwamba TUMPE KURA MAGUFULI KAMA SHUKRANI. Amenikera na kuniudhi sana...
www.jamiiforums.com
Ufanisi wa wafanyakazi Serikalini na nyongeza ya mishahara yao
Rais Magufuli alipoingia madarakani kitu cha kwanza alichojitahidi kurekebisha ni jinsi wafanyakazi wa serikali walivyokuwa hawawajibiki kutimiza majukumu yao; alifanya zoezi la ziara za kustukiza maofisini na kuwaadhibu wale waliokutwa na makosa. Zoezi la ziara za kushstukiza pamoja na zoezi...
www.jamiiforums.com
Tunasubiri Majibu yako.
Karibu.