Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,037
- 20,333
Kutokana na baadhi ya maeneo kulazimisha sheria ya “Rights to Repair” Apple imelazimika kuachia uhuru kwa watumiaji wake kurekebisha simu wenyewe au kwa mafundi ambao hawajasajiliwa. Itasaidia wateja wa Apple ambao wana uwezo wa kutengeneza simu zao wenyewe, kuwa na uhuru wa kuagiza vifaa na spare za kurekebisha simu; na Mafundi wa Mitaani kuwa na uhuru wa kusaidia watu katika kuwatengenezea vifaa vyao bila kuharibu Warranty, FaceID kugoma baada ya kubadilisha kioo Au Error Message ya kusema battery sio Genuine.
Wateja ambao watahitaji kurekebisha simu zao wenyewe, mfano kubadili Battery, Kamera au Kioo; wanaweza kucheck Apple Repair and Repair Status Check - Official Apple Support na kuagiza spare au kutazama namna ya kurekebisha simu mwenyewe.
Hii ni good news hata kwa mafundi wa mitaani ambao wanaweza kurekebisha simu vizuri.
Mabadiliko haya yataanza Mwaka 2022, naitaanza kwa watumiaji wa iPhone 12 na iPhone 13 tu. Sehemu zilizoruhusiwa kubadilishwa ni Kioo, Kamera na Battery; pia ni muhimu kuhakikisha unabadili kwa kutumia vifaa Original