MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
MGONJWA aliyekuwa akiwahishwa katika Hospitali ya Wilaya Same, Ester Paresetwi (35) na gari likapinduka na kuua muuguzi na dereva amepona mara tu baada ya ajali.
Katika ajali hiyo ya gari la wagonjwa, muuguzi wa zahanati ya Kisiwani wilayani humo, Joshua Jacob (29) na dereva, Jumanne Makumbe (48) walikufa na wengine watatu walijeruhiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema jana majeruhi akiwemo mgonjwa aliyekuwa akipelekwa hospitali wanaendelea vizuri katika Hospitali ya Wilaya ya Same.
Alisema ajali hiyo ilitokea eneo la Majevu Kata ya Kisiwani wilayani Same Agosti 7 mwaka huu saa 10 jioni wakati tairi la nyuma la gari lilipopasuka, likapoteza mwelekeo na kupinduka.
Chanzo: HabariLeo
Katika ajali hiyo ya gari la wagonjwa, muuguzi wa zahanati ya Kisiwani wilayani humo, Joshua Jacob (29) na dereva, Jumanne Makumbe (48) walikufa na wengine watatu walijeruhiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema jana majeruhi akiwemo mgonjwa aliyekuwa akipelekwa hospitali wanaendelea vizuri katika Hospitali ya Wilaya ya Same.
Alisema ajali hiyo ilitokea eneo la Majevu Kata ya Kisiwani wilayani Same Agosti 7 mwaka huu saa 10 jioni wakati tairi la nyuma la gari lilipopasuka, likapoteza mwelekeo na kupinduka.
Chanzo: HabariLeo