Apelekwa rumande kwa tuhuma za kumlawiti mlemavu wa akili

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,264
5,355
Mahakama ya Mkoa Kusini Pemba Chake Chake imemrudisha rumande Said Hassan Mabrouk maarufu kwa jina la Said King, mkazi wa Mtoni Chake Chake kwa tuhuma za kumlawiti mlemavu wa akili mwenye umri wa miaka 35.

Katika muendelezo wa kesi hiyo iliyosikilizwa Juni 28, 2022 mwendesha mashtaka wa Serikali Ali Amour Makame mbele ya hakimu wa Mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji Muumin Ali Juma, imedaiwa Mahakamani hapo kuwa mshitakiwa siku ya tarehe 10\05\2022 Majira ya saa 1:30 za asubuhi Mtoni Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mtuhumiwa alimlawiti mlemavu wa akili jambo ambalo ni kosa kisheria.

Shahidi nambari moja ambaye ni muathirika wa kesi hiyo ya udhalilishaji ameiambia Mahakama kuwa siku ya tarahe 10\05\2022 majira ya saa 1:30 asubuhi mtuhumiwa alimchukuwa kutoka nyumbani kwao (muathirika) na kumpeleka nyumbani kwake (mtuhumiwa) na kumuingiza chumbani kisha kumvua nguo na kumlaza kifudifudi na kumpaka mafuta sehemu yake ya siri ya haja kubwa na kumfanyia kitendo cha udhalilishaji.

“Alikuja kunichukua nyumbani na kunipeleka nyumbani kwake kisha akanitia chumbani na kunivua nguo akanilaza kifudifudi akanipaka mafuta nyuma na kunifanyia kitendo hicho na alipomaliza akanambia nisiseme nyumbani,” alieleza muathirika huyo.

Baada ya ushahidi huo kutolewa ambao uliwaacha watu vinywa wazi hakimu Muumini Ali Juma alighairisha kesi hiyo hadi Julai 12, 2022 itakaposikilizwa tena ushahidi.

Juni 28, 2022 ni mara ya nne kesi hiyo kurindima Mahakamani hapo, ambapo mara ya kwanza kesi hiyo kutajwa ilikuwa ni Mei 23, 2022, Juni 06, 2022 na Juni 14, 2022.

Chanzo: Idawaonline
 
Inna lilahi waina ilaihi rajiun, katumia nafuta gani hayo, na mgonjwa wa akili kapataje ufaham wa kutoa ushahidi, una miaka 35 ilikuwaje ukabebwa pasi na kuketa hata vurugu au kupiga kelele, mpaka unapakwa mafuta na kuingizwa uume je alikufunga kamba?mpaka ana maliza umetulia tu unaingiliwa jmn,aaah jamn waoemba vipi tena
 
Inna lilahi waina ilaihi rajiun, katumia nafuta gani hayo, na mgonjwa wa akili kapataje ufaham wa kutoa ushahidi...
Mtu kuwa mgonjwa wa akili haimanishi ndio hana ufahamu, kumbukumbu au hawezi kusimulia.

Nimekutana nao mara kadhaa.

Pia kuna wakati mgonjwa anaweza kuwa haongei kabisa au akafanya Vurugu, lakini baada ya muda unaweza kupiga nae stori vizuri tuu.
 
kulawiti ni kosa kisheria hata umfanyie shoga.

lakini huyu mgonjwa ana tatizi binafsi,
ni kama yule aliyekuwa anasimulia....
alinishika mkono namuangalia tu
akanipeleka ndani namhangalia tu
akanilaza kitandani namuangalia tu
akanivua nguo namuangalia tu
ananipaka mafuta namuangalia tu
na kuingiza namuangalia tu.
 
kulawiti ni kosa kisheria hata umfanyie shoga.

lakini huyu mgonjwa ana tatizi binafsi,
ni kama yule aliyekuwa anasimulia....
alinishika mkono namuangalia tu
akanipeleka ndani namhangalia tu
akanilaza kitandani namuangalia tu
akanivua nguo namuangalia tu
ananipaka mafuta namuangalia tu
na kuingiza namuangalia tu.
Wewe ndiye una tatizo tena kubwa kabisa. Hujui maana ya mtu kuwa ''mgonjwa wa akili''? Kwa kifupi IQ yake inaweza kuwa kama ya mtoto mdogo. Which means anakuwa na akili za mtoto, anavyoambiwa fanya hiki, na yeye anafanya kwani hawezi kupima madhara yake. Angalia wewe ndiye ukawa una tatizo binafsi la kushindwa kujua ugonjwa wa akili ukoje?
 
Duuuuh mie huwa nashangaa sana, watu wanalawiti watoto, au watu wasiohusika, mbna mashoga wako mitaani wamejaa tele, kwann wasiwafate hao?

Inakeraaaa mnoooo.
 
Mahakama ya Mkoa Kusini Pemba Chake Chake imemrudisha rumande Said Hassan Mabrouk maarufu kwa jina la Said King, mkazi wa Mtoni Chake Chake kwa tuhuma za kumlawiti mlemavu wa akili mwenye umri wa miaka 35.

Katika muendelezo wa kesi hiyo iliyosikilizwa Juni 28, 2022 mwendesha mashtaka wa Serikali Ali Amour Makame mbele ya hakimu wa Mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji Muumin Ali Juma, imedaiwa Mahakamani hapo kuwa mshitakiwa siku ya tarehe 10\05\2022 Majira ya saa 1:30 za asubuhi Mtoni Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, mtuhumiwa alimlawiti mlemavu wa akili jambo ambalo ni kosa kisheria.

Shahidi nambari moja ambaye ni muathirika wa kesi hiyo ya udhalilishaji ameiambia Mahakama kuwa siku ya tarahe 10\05\2022 majira ya saa 1:30 asubuhi mtuhumiwa alimchukuwa kutoka nyumbani kwao (muathirika) na kumpeleka nyumbani kwake (mtuhumiwa) na kumuingiza chumbani kisha kumvua nguo na kumlaza kifudifudi na kumpaka mafuta sehemu yake ya siri ya haja kubwa na kumfanyia kitendo cha udhalilishaji.

“Alikuja kunichukua nyumbani na kunipeleka nyumbani kwake kisha akanitia chumbani na kunivua nguo akanilaza kifudifudi akanipaka mafuta nyuma na kunifanyia kitendo hicho na alipomaliza akanambia nisiseme nyumbani,” alieleza muathirika huyo.

Baada ya ushahidi huo kutolewa ambao uliwaacha watu vinywa wazi hakimu Muumini Ali Juma alighairisha kesi hiyo hadi Julai 12, 2022 itakaposikilizwa tena ushahidi.

Juni 28, 2022 ni mara ya nne kesi hiyo kurindima Mahakamani hapo, ambapo mara ya kwanza kesi hiyo kutajwa ilikuwa ni Mei 23, 2022, Juni 06, 2022 na Juni 14, 2022.

Chanzo: Idawaonline
The only big difference between humans and animals is that sometimes humans are more animal than animals
 
Swali kwa Wataalamu wa Sheria;

Je Mtu aliyethibitishwa kuwa ni Mlemavu wa akili anaweza kutoa Ushahidi na ukazingatiwa Mahakamani?

Vipi kama akili zake zimemwambia kuwa Amebakwa ilhali hajabakwa? Maana wengine humu Mtaani tunawaona wakiendesha magari virtually na wanaamini kabisa kuwa wamo ndani ya gari halisi, na honi wanapiga kwa mdomo..
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom